Mapya yaibuka ofisa TRA anayedaiwa kujiua hotelini

Kufuatia kifo cha ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Arusha, Richard Walalaze aliyedaiwa kujiua kwa kujirusha kutoka ghorofani, familia ya marehemu imeibua mpya baada ya kuuona mwili wake katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Bombo na kufuatilia mahali ulipokutwa mwili huo hotelini.

Familia hiyo imesema haiamini kama kweli alijirusha na kueleza kuwa kifo chake kinatia shaka na kubainisha kuwa imejikuta ikiwa na maswali mengi yasiyo na majibu, hivyo inasubiri taarifa ya uchunguzi wa mwili itakapotolewa na Serikali.

Msemaji wa familia hiyo, kaka wa marehemu, Godfrey Walalaze, ambaye ni mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki amesema hayo akiwa katika Hospitali ya Bombo na kubainisha kuwa mazingira ya kifo cha ndugu yao yanatia shaka iwapo ni kweli alijirusha kutoka ghorofani au la.

"Tumeuchunguza mwili tunapata shaka, sababu ukiacha kovu kichwani, mwili wote hauna mchubuko wala hakuna kiungo chochote kilichovunjika, lakini hata pale hotelini ulipokutwa mwili na michirizi ya damu inatupa maswali mengi mno," alisema Walalaze.

Kitenge Updates
 
RIP na ile nyumba yako nzuri ambayo umetumia miaka 10 kuijenga na kuishi kwa miaka 1 sasa ni mali halali ya wife wako uliyeishi nae miaka 2.
Yatafumuka mengi. Kaka mtu anasema mdogo wake hajawahi kuoa. Wewe wasema kaacha mke aliyeishi naye kwa miaka miwili. Sasa hili linaleta maswali mengi kuhusu nini hasa kilitokea.
 
Gorofa 2 mtu kufa labda Afanye kama anaogelea adive kichwa kitangulieee.. Otherwise its a murder case not suicide sema bongo ndo imeishaa hiyoo!! Na kishindo cha kujitupa hakuna mtu yeyote aliesikia kweli kwa yale mazingira ya ile hotel.
Usipime mzee secondary tulimuwekea dau mkomavu moja aruke ghorofa moja...akatua kwa miguu lakini tulibeba kwenye taxi hadi kwao..
 
Na sio mtume m au Musa ,hongera

Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
 
Miaka 35 Ana ajira hajaoa basi shida
 
Hii ndio inaitwa Forensic Investigation?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…