Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Mara yangu ya kwanza kukutana na malaika(1987)

Za masaa wana JF.

Leo nimeona ni vyema kuwaletea kisa kilichonitokea mwaka 1987 nikiwa kidato cha tano huko Ilboru secondary school. Nilikuwa nikisikia tu habari za malaika kwenye ibada za kidini.

Siku hiyo niliamka usiku kwenda kusoma darasani kama kawaida yangu, yapata saa nane za usiku. Hakukuwa na mtu yeyote darasani bali mimi tu. Wakati naendelea na kubukua ghafla ukatokea mwanga mkali mbele yangu. Ukaniangazia, niliingiwa na hofu na kuanza kutetemeka. Mara nikasikia sauti ya binadamu ikitoka kwenye mwanga ule. Ikiinita jina langu David, David usiogope tazama hapa.

Nilijawa na nguvu na kukaza macho yangu kuutanzama ule mwanga. Ghafla nimuona kiumbe afananae na mwanadamu rangi yake ya silver inayong'aa sana. Mdomo wangu ulikuwa mzito nilishindwa kuongea. Yule kiumbe alinisogelea na kuniambia "Nimekuja kukupa siri ya ulimwengu" Ndipo kiumve hicho kilinigusa kidevu changu, nilihisi kupigwa shot ya umeme. Akaendelea kusema mimi ni malaika, nimekuja kujidhilisha kwako. Ndipo mwili wangu wote ulianza kutetemeka. Alinishika na nikajikuta nipo katika eneo ambalo sijawahi kuliona ni zuri sana.

Akaniambia hapa ndipo huja watu wanapokufa duniani. Alinionesha watu mbalimbali waliokufa, walikuwa pale wakiwa na furaha. Nilimuona mwalimu wangu wa Hisabati kidato cha pili aliyekufa kwa ajali ya gari. Nilimuona akiwa na furaha.

Malaika huyo aliniambia usiogope kuhusu kifo maana ni sehemu ya ukamilisho.

Ni mambo mengi mno niliyapata siku hiyo. Kwa leo naongelea haya tu. Mpaka sasa malaika mbalimbali huwa wanakuja. Nimeshawazoea na tunaongea nao mambo mengi tu.

Nitakuja kuwaeleza namna yetu sisi tulivyofungwa kwenye kifungo cha hapa duniani. Na namna gani ya kuuona ulimwengu wote.

Asante kwa sasa.
Wenu mtiifu D.
Dah sijui lakini ila kuna makanisa huwa wanasema Yesu anajifunza kiswahili
 
Kijana wa kiume punguza GUBU. Otherwise amia upande wa pili.
Naskitika sana mwelekeo wa huu uzi.. hasa kutokana na majibizano yenu! Busara ni kumwacha mwenye uzi amalize kisha utoe maoni/hitimisho/dukuduku lako.

Wakati mwingine badala ya kuuvuruga kama hivi.. hebu anzisha uzi wako ukielezea kwa mtazamo wako kama ulivyo funuliwa

Asante
 
Soma post zake za mwishoni utamwelewa. Hanamini kwamba hakuna lolote linaloweza kumshinda MUNGU, na kwamba kuna mambo MUNGU hawezi kufanya ikiwemo kutibu baadhi ya magonjwa. Anaamini God's power is limited.Period
Yaani unalazimisha nimuelewe kama unavyotaka wewe? Watu Bwana......................!
 
Naskitika sana mwelekeo wa huu uzi.. hasa kutokana na majibizano yenu! Busara ni kumwacha mwenye uzi amalize kisha utoe maoni/hitimisho/dukuduku lako.

Wakati mwingine badala ya kuuvuruga kama hivi.. hebu anzisha uzi wako ukielezea kwa mtazamo wako kama ulivyo funuliwa

Asante

Jamaa anajifanya mjuaji sana empty set kabisa huyu
 
Huna ujualo juha wewe, labda kama waga unaonana na malaika kupitia meditation kitu ambacho ni mind game not really.
 
Acha kula mabaki ya Cannabis almaarufu kama Kushabu mkuu itakuathili kisaikolojia Ipo siku uta jump ghorofani Kwa kujiona ni Moja ya Avengers character utakufaaaaa,
Wake up c'mon boooy!
😁😁😁
🤣alafu ndo nko hp nakula hayo hyo sadali mzgo umekata
 
Tangu 1987 ndio Leo unakuja jamvini?ulikua wapi siku zote?labda malaika waliohasi mbinguni.

Anyway usitumie mabaki ya cannabis yatakurusha juu sio mchezo.
 
Kuna wakati huwa nahisi humu kuna viumbe vingine sio watu,Venus star una uhakika wewe sio ndio malaika mwenyewe kweli?
 
Mm nilikutana na Malaika wangu Waswanu bar - dodoma mwaka Jana mpaka leo tunaishi kwa furaha
 
Umetokewa na nn tena MTU wetu ww hata ukushtuka aliposema Mungu na shetani wakiungana uleta amani sasa uyo jini kashasema Mungu na shetani awajaungana kimawazo huoni kuwa ilo lijamaa n lishetani maana linaongea pumba nyingi eti mawazo ya Mungu na shetani yakiungana ... Ww jamaa shtuka ulikopelekwa uyo jini anapajua yy ila sio paradiso apo man ww shtuka mwovu uyooo mkemee kwajina la Yesu au unda timu ya kufunga na kusali uyatimue..
 
Haya mambo ni halisia kabisa.

Kwa mara ya kwanza Mwaka 2012 nikiwa chuo mwaka wa pili tulikuwa na huduma ya kuhubiri Mangaka Mtwara nikiwa katika hali ya utulivu mkubwa,nimejawa hali ya upendo kwa watu wote yaani niliomba msamaha wa kweli kwa watu wote nilio wakosea pia nikawasamehe watu walionikosea,kwakifupi nilikuwa huru sana.

Ulikuwa usiku wa saa sita nikiwa katika hali ya maombi,nilitokewa na mtu ambaye sijawahi muona kabla akiwa amevalia mavazi meupe na amejaa hali ya upendo usio kifani,ki ukweli nilijisikia amani ya moyo ambayo sijawahi iona kabla.Kwasauti ya upendo aliniambia fanya kazi yangu.

Kwakweli kesho yake tulikuwa na huduma ya kuwaombea watu mbalimbali wenye shida nilikuwa na nguvu ambayo sijawi kuwa nayo kabla,ilifika hatua hata kwa kumpulizia pumzi mtu aliyekuwa na nguvu za giza na alifunguliwa wakati huohuo.Niliogopa kiasi kwani awali nilikuwa siamini kuwa hayo mambo yanawezekana.

Nilichojifunza kutoka mwaka ule, ili uweze kuwasiliana na Mungu kupitia malaika wake kwa njia ya Yesu Kristo,inahitaji uwekezaji wa hali ya juu,vitu muhimu unavyotakiwa kuwa navyo ni;
1.Upendo wa kweli yaani uwasamehe watu wote walio kukosea pia omba msamaha kwa watu walio kukosea(Moyo usio na mawaa )
2.Tenga mda wa kuongea na Mungu wako na nguvu iliyoko ndani yako...hakuna jambo kubwa au zuri linalo patikana kirahisi rahisi.
3.Sehemu kubwa ya maombi yako iwe kuwaombea watu wengine wenye uhitaji mfano wagonjwa,masikini,yatima,wajane na watumishi yaani wachungaji,mapadre,mashehe wanaofanya kazi zao katika mazingira magumu.
4.Kuwa mnyenyekevu.

Nguvu za Mungu zipo, changamoto kubwa ni sisi kuwa na mambo mengi ndani ya mioyo yetu ambayo ni vigumu kutukutanisha na nguvu za Mungu na Mungu mwenyewe mfano,wivu,fitina,kukosa upendo, ubinasfi,zaidi ya yote kuchukia mafanikio ya watu wengine.
 
Za masaa wana JF.

Leo nimeona ni vyema kuwaletea kisa kilichonitokea mwaka 1987 nikiwa kidato cha tano huko Ilboru secondary school. Nilikuwa nikisikia tu habari za malaika kwenye ibada za kidini.

Siku hiyo niliamka usiku kwenda kusoma darasani kama kawaida yangu, yapata saa nane za usiku. Hakukuwa na mtu yeyote darasani bali mimi tu. Wakati naendelea na kubukua ghafla ukatokea mwanga mkali mbele yangu. Ukaniangazia, niliingiwa na hofu na kuanza kutetemeka. Mara nikasikia sauti ya binadamu ikitoka kwenye mwanga ule. Ikiinita jina langu David, David usiogope tazama hapa.

Nilijawa na nguvu na kukaza macho yangu kuutanzama ule mwanga. Ghafla nimuona kiumbe afananae na mwanadamu rangi yake ya silver inayong'aa sana. Mdomo wangu ulikuwa mzito nilishindwa kuongea. Yule kiumbe alinisogelea na kuniambia "Nimekuja kukupa siri ya ulimwengu" Ndipo kiumve hicho kilinigusa kidevu changu, nilihisi kupigwa shot ya umeme. Akaendelea kusema mimi ni malaika, nimekuja kujidhilisha kwako. Ndipo mwili wangu wote ulianza kutetemeka. Alinishika na nikajikuta nipo katika eneo ambalo sijawahi kuliona ni zuri sana.

Akaniambia hapa ndipo huja watu wanapokufa duniani. Alinionesha watu mbalimbali waliokufa, walikuwa pale wakiwa na furaha. Nilimuona mwalimu wangu wa Hisabati kidato cha pili aliyekufa kwa ajali ya gari. Nilimuona akiwa na furaha.

Malaika huyo aliniambia usiogope kuhusu kifo maana ni sehemu ya ukamilisho.

Ni mambo mengi mno niliyapata siku hiyo. Kwa leo naongelea haya tu. Mpaka sasa malaika mbalimbali huwa wanakuja. Nimeshawazoea na tunaongea nao mambo mengi tu.

Nitakuja kuwaeleza namna yetu sisi tulivyofungwa kwenye kifungo cha hapa duniani. Na namna gani ya kuuona ulimwengu wote.

Asante kwa sasa.
Wenu mtiifu D.
Alinena nawe kwa lugha gani David?
 
Za masaa wana JF.

Leo nimeona ni vyema kuwaletea kisa kilichonitokea mwaka 1987 nikiwa kidato cha tano huko Ilboru secondary school. Nilikuwa nikisikia tu habari za malaika kwenye ibada za kidini.

Siku hiyo niliamka usiku kwenda kusoma darasani kama kawaida yangu, yapata saa nane za usiku. Hakukuwa na mtu yeyote darasani bali mimi tu. Wakati naendelea na kubukua ghafla ukatokea mwanga mkali mbele yangu. Ukaniangazia, niliingiwa na hofu na kuanza kutetemeka. Mara nikasikia sauti ya binadamu ikitoka kwenye mwanga ule. Ikiinita jina langu David, David usiogope tazama hapa.

Nilijawa na nguvu na kukaza macho yangu kuutanzama ule mwanga. Ghafla nimuona kiumbe afananae na mwanadamu rangi yake ya silver inayong'aa sana. Mdomo wangu ulikuwa mzito nilishindwa kuongea. Yule kiumbe alinisogelea na kuniambia "Nimekuja kukupa siri ya ulimwengu" Ndipo kiumve hicho kilinigusa kidevu changu, nilihisi kupigwa shot ya umeme. Akaendelea kusema mimi ni malaika, nimekuja kujidhilisha kwako. Ndipo mwili wangu wote ulianza kutetemeka. Alinishika na nikajikuta nipo katika eneo ambalo sijawahi kuliona ni zuri sana.

Akaniambia hapa ndipo huja watu wanapokufa duniani. Alinionesha watu mbalimbali waliokufa, walikuwa pale wakiwa na furaha. Nilimuona mwalimu wangu wa Hisabati kidato cha pili aliyekufa kwa ajali ya gari. Nilimuona akiwa na furaha.

Malaika huyo aliniambia usiogope kuhusu kifo maana ni sehemu ya ukamilisho.

Ni mambo mengi mno niliyapata siku hiyo. Kwa leo naongelea haya tu. Mpaka sasa malaika mbalimbali huwa wanakuja. Nimeshawazoea na tunaongea nao mambo mengi tu.

Nitakuja kuwaeleza namna yetu sisi tulivyofungwa kwenye kifungo cha hapa duniani. Na namna gani ya kuuona ulimwengu wote.

Asante kwa sasa.
Wenu mtiifu D.
Yaani hawa Malaika nimewasika weeee!! tangu nikiwa na miaka 13 na sasa ni mtu mzima nimejitahidi weeee niwaone wapi lkn bado mnanitamanisha mweee!!...skia David siku akija huyo Malaika mwambie nime mmiss sana yaani mie nimuone tu!!
 
Haya mambo ni halisia kabisa.

Kwa mara ya kwanza Mwaka 2012 nikiwa chuo mwaka wa pili tulikuwa na huduma ya kuhubiri Mangaka Mtwara nikiwa katika hali ya utulivu mkubwa,nimejawa hali ya upendo kwa watu wote yaani niliomba msamaha wa kweli kwa watu wote nilio wakosea pia nikawasamehe watu walionikosea,kwakifupi nilikuwa huru sana.

Ulikuwa usiku wa saa sita nikiwa katika hali ya maombi,nilitokewa na mtu ambaye sijawahi muona kabla akiwa amevalia mavazi meupe na amejaa hali ya upendo usio kifani,ki ukweli nilijisikia amani ya moyo ambayo sijawahi iona kabla.Kwasauti ya upendo aliniambia fanya kazi yangu.

Kwakweli kesho yake tulikuwa na huduma ya kuwaombea watu mbalimbali wenye shida nilikuwa na nguvu ambayo sijawi kuwa nayo kabla,ilifika hatua hata kwa kumpulizia pumzi mtu aliyekuwa na nguvu za giza na alifunguliwa wakati huohuo.Niliogopa kiasi kwani awali nilikuwa siamini kuwa hayo mambo yanawezekana.

Nilichojifunza kutoka mwaka ule, ili uweze kuwasiliana na Mungu kupitia malaika wake kwa njia ya Yesu Kristo,inahitaji uwekezaji wa hali ya juu,vitu muhimu unavyotakiwa kuwa navyo ni;
1.Upendo wa kweli yaani uwasamehe watu wote walio kukosea pia omba msamaha kwa watu walio kukosea(Moyo usio na mawaa )
2.Tenga mda wa kuongea na Mungu wako na nguvu iliyoko ndani yako...hakuna jambo kubwa au zuri linalo patikana kirahisi rahisi.
3.Sehemu kubwa ya maombi yako iwe kuwaombea watu wengine wenye uhitaji mfano wagonjwa,masikini,yatima,wajane na watumishi yaani wachungaji,mapadre,mashehe wanaofanya kazi zao katika mazingira magumu.
4.Kuwa mnyenyekevu.

Nguvu za Mungu zipo, changamoto kubwa ni sisi kuwa na mambo mengi ndani ya mioyo yetu ambayo ni vigumu kutukutanisha na nguvu za Mungu na Mungu mwenyewe mfano,wivu,fitina,kukosa upendo, ubinasfi,zaidi ya yote kuchukia mafanikio ya watu wengine.
Vipi mkuu, alitumia lugha gani kuwasiliana na wewe..?
 
Hahaha... huyo malaika BOYA KABISA... akija tena mwelekeze aache utaahira.
Dogo!! usifanye masihara na haya mambo weeye hivi!! akikutokea hapo si utabaki unajamabajamba tu??...na hatutakuona humu tenaaa!!....huo uzima ndo unakupa kiburi hayaweee!!
 
Back
Top Bottom