Marekani akiwekewa vikwazo na China maana yake China iache kuuza bidhaa zake Marekani, kwa mwaka China inauza zaidi ya dola bilioni 400 kwa Marekani. Kwa hiyo China wawe vilaza waache kupata bilioni 400 kwa mwaka wabaki kwa Russia kupata dola bilioni 50 kwa mwaka, hii ni 1 ya 8.
Wakati huo China ikose patents zote za Marekani. ZTE ilipigwa sanctions na Marekani mpaka leo hatuoni simu zake, Huawei ilipigwa sanctions mpaka ikafungua biashara ya kufuga nguruwe ili kutosheleza profits. Patents za teknolojia ya simu nyingi ni za makampuni ya Marekani. Hata TCMS wataambiwa hakuna kuuza microchips kwa China wala Russia, Samsung Electronics mnayoona hii Marekani ikitaka ipotee sokoni ndani ya miaka minne inaweza potea. Ukipiga marufuku wasitumie foundry tech ya US kutengeneza chips zao za Exynos, au kufanya outsourcing ya chips kutoka kwa Qualcomm ya Marekani. Kwahiyo Samsung nao watachagua upande wa Marekani kuliko China na Russia.
China akishindwa kuzalisha zaidi kwa ajili ya kuuza Marekani atapunguza mahitaji ya gesi na mafuta kutoka Russia na kwingineko, hapo Russia anapunguza mapato, soko la mafuta duniani linashuka uchumi wa OPEC wote unaporomoka na dunia kwa ujumla inaingia mdororo wa uchumi. Marekani inaweza zalisha mapipa milioni 15 ya mafuta kwa siku ukijifanya unaikomoa, kwa siku inatumia mapipa milioni 19 hizo nne zinazokosa kwenye mlinganyo inatafuta hata Libya inawahonga wanaiuzia extra.
Kampuni kama Boeing zinaacha kufanya kazi China na Russia. Pia Dell, HP, Apple, Sony, etc. GPS inafungwa wabaki na GLONAS zao na BeiDou ambazo sio reliable na hazina global support. Android system inafungwa na iOS tuone ni Mwafrika gani ataanza kujaribisha systems ambazo hajawahi sikia. Facebook, WhatsApp, Twitter, Instagram zinafungwa kwao na kwa vifaa wanavyotengeneza. Warusi wabaki na VKontakte (ambayo najua 98% ya wabongo hawajawahi hata kuisikia) na Wachina wabaki na kina WeChat, Weibo na TikTok. Ukiachana na TikTok ni nani duniani hapa atataka aache hizo nyingine atumie VKontakte au Weibo na WeChat?
South Korea, Japan, UK, Germany, France, Australia, Italy, Spain, Canada zitasimama na Marekani. Israel na Switzerland wanaweza chagua kuwa neutral, Waarabu vigeugeu kupindukia watasoma upepo ila wengi watakuwa upande wa Marekani. Yani Qatar aache kuwa upande wa Marekani ambako kila giant aliyeko kule anajiweza na gesi hana, aende kushiriki na China ambako Russia anamuuzia gesi kwa fujo?