Marekani kupigana vita na China 2025, Jenerali wa Marekani bw. Mike

Marekani kupigana vita na China 2025, Jenerali wa Marekani bw. Mike

Huwa naona it's very likely Marekani kuanzisha vita na China kuliko kuanzisha na Urusi
Chumi mbili kubwa duniani zinazotegemeana ziamue kupigana kisa Taiwan au ?....

Na vilevile uwezekano wa China kuishambulia Russia ni mkubwa kuliko kuishambulia Marekani.
Hiyo hiyo China huiona Urusi kama mshirika inapowakabili wamagharibi vipi Sasa imshambulie ?.....japo waliwahi kuzozana mipakani enzi za Ussr hivyo lolote linawezekana.
 
Jenerali wa jeshi la anga la marekani Bw. Mike Minihan ameliandikia ujumbe jeshi la marekani kuwa tayari kwa ajili ya kupambana na China mwaka 2025.

Vyanzo vya habari:
View attachment 2499957View attachment 2499958View attachment 2499959View attachment 2499960View attachment 2499961

Swali kutoka kwa lieutenant katika jeshi la marekani hili hapa :
View attachment 2499962
Maswali yangu:
1. Ipi ni athari kubwa ya ujumbe wa jenerali huyu kwa marekani na China ?

2. Yapi ni matokeo ya ujumbe huu katika siasa za kimataifa kati ya China na Marekani ?

3. Je tutegemee kuona mgogoro mkubwa katika Indo- Pasific ?

: Karibuni kwa maoni yenu na maswali ya ziada.
Nowadays people think Russian roulette is a safe game to play
 
Jenerali wa jeshi la anga la marekani Bw. Mike Minihan ameliandikia ujumbe jeshi la marekani kuwa tayari kwa ajili ya kupambana na China mwaka 2025.

Vyanzo vya habari:
View attachment 2499957View attachment 2499958View attachment 2499959View attachment 2499960View attachment 2499961

Swali kutoka kwa lieutenant katika jeshi la marekani hili hapa :
View attachment 2499962
Maswali yangu:
1. Ipi ni athari kubwa ya ujumbe wa jenerali huyu kwa marekani na China ?

2. Yapi ni matokeo ya ujumbe huu katika siasa za kimataifa kati ya China na Marekani ?

3. Je tutegemee kuona mgogoro mkubwa katika Indo- Pasific ?

: Karibuni kwa maoni yenu na maswali ya ziada.
Hawa jamaa wapo a head of us wanachokisema ndicho na ndio maana unaona Europe wanawaangalia kama Masia wao maana hii vita ya Ukraine walisha itabiri miaka zaid ya Ishirini nyuma German hakutegema vita hii. End
 
Maana yake ni kuwa Marekani hawana mpango wa vita na Urusi kwahiyo Ukraine aendelee kuwalilia hao ndugu zake wa Ulaya, hata Zele akija congress kubutubia sisi Marekani tumefocus zaidi na bwana Xi.

Kitaalam ukraine amejiingiza cha kike!
 
1. Russia alisema atakayemsaidia Ukraine atakutana na mkono mzito, kila leo misaada inaenda Ukraine. Kwanini Russia asimchape US?

2. Biden alisema Russia akiivamia tu Ukraine wanalipua bomba la mafuta, na ni kweli US aliripua hilo bomba.

US tusimchukulie wa mchezo mchezo. Mtu ambae kila kona ya dunia yupo ameweka base, na takribani miaka 50 sasa kila mwaka ana vita na operations kibao anazifanya, jamaa yupo vizuri.

Sasa hivi amekiwasha huko Ukraine. Na bado vile vile alikuwa tayari kukiwasha Taiwan dhidi ya China. Nitajie mjinga gani hapa duniani anaweza akawa na guts kama hizi?.

Leo hii Iran, S.Korea pawake moto, unafikiri Russia anaweza kunyanyua miguu yake kuwasaidia hao? Lakini US anaweza akapambana huko Ukraine, Taiwan pia akapeleka misaada, na bado uko Korea au Japan kukinuka akapeleka misaada na majeshi kupambana.

Nenda google, bajeti ya ulinzi ya US, chukua bajeti za ulinzi z UK German France, China, Russia, Canada n.k zijumrishe kwa pamoja na hawafiki nusu ya bajeti ya ulinzi jamaa.
Nadhani swala la ukubwa wa bajeti ya wizara ya ulinzi una sababu zake.

Sidhani kama U.S.A ana uwezo wa kusimamia zaidi ya vita tatu zinazo husisha mataifa makubwa licha ya kuwa sipuuzii nguvu zake za kijeshi alizo nazo.
 
Hayo ni maoni binafsi ya huyo General. Kasema hisia zake zinamtuma hivyo, foreign policy haiendeshwi na hisia za mtu mmoja hata angekuwa ndiye Rais wa Marekani.
Na China hawashangai juu ya hilo, nani asiyejua jeshi la Marekani linajipanga kuikabili China. Kila mwaka Pentagon hutoa assessment na kuelezea advancement ya jeshi la China. China hawakurupuki kwenye sera zao za kigeni, wanaonekana wapole kwa nje ila muda wao kuonyesha ubabe bado.

Huwa naona it's very likely Marekani kuanzisha vita na China kuliko kuanzisha na Urusi. Na vilevile uwezekano wa China kuishambulia Russia ni mkubwa kuliko kuishambulia Marekani.
Inverse thinking.

China hata siku moja hawezi pigana na USA ndani ya miaka hii 20. Bado wanategemeana sana.

Na USA sio mpuuzi kiasi hicho kuanzisha vita na China, usije ukadhan USA kushadadia vita ya urusi basi wanapenda vita, wale jamaa huwa hawapotezi hata risasi, ukiona wameshoot basi jua wana lengo lao. Jiulize hii vita ya Urusi nani kaja kupata benefit kuliko yyt yule?

Tumia akili kdg, ni kpnd cha vita ya urusi tu ndipo EUR na USD zikafikia parity kitu ambacho hakikuwahi kutokea miaka mingi sana, Nguvu ya USD ikaongezeka ikatawala currencies zote hadi japam watu wakaanza kuinunua USD kwa 150 Yen, isingekua japan kushangaza dunia na policy yao mpya ya uchumi december mwaka jana basi usd ingebaki mbabe wa YEN pia.

Kuna mifano mingi kukuonesha USA kagain zaidi kwenye hio vita zaidi ya nchi yyt ile, na cha kushangaza hajapoteza kitu cha maana sasa ukilinganisha na nchi za ulaya ambazo kdg wananchi wao waandamane kisa njaa na kuanza kula vyakula vya mbwa.

Juzijuzi tu hapa china wamelift tena covid ban lkn USA akaanza kupiga kelele kwamba itakuza inflation rate tena, unajua sababu ya hilo?

Tukirudi kwa Urusi na CHINA hio vita unayosemea haina maana sababu vita inahitaji 'motivation', ww usije kudhan watu wataamka wapigane tu. Haya, nipe motivation ya china kumpiga urusi ndan ya hii miaka ya karibuni.

Turudi kwenye note ya huyo general, hivi unajua hata raisi hana uwezo wa kudeclare war USA? sembuse huyo general na uzee wake. Hata raisi akitaka kudeclare war anapitisha shauri senate then senate wanapiga kura.

The crux is USA will never lose a bullet
 
Hawa jamaa wapo a head of us wanachokisema ndicho na ndio maana unaona Europe wanawaangalia kama Masia wao maana hii vita ya Ukraine walisha itabiri miaka zaid ya Ishirini nyuma German hakutegema vita hii. End
Swala la Taiwan na China ni swala la muda sana miaka mingi iliyo pita lakini uwezekano wa U.S.A kupigana na China mwaka 2025 kuhusu hilo swala hapo ndipo pa msingi sana alipo zungumza general. Uwezekano huo Je utatimia ?
 
Maana yake ni kuwa marekani hawana mpango wa vita na urusi kwaio ukraine aendelee kuwalilia hao ndugu zake wa ulaya, hata Zele akija congress kubutubia sisi marekani tumefocus zaidi na bwana Xi.

Kitaalam ukraine amejiingiza cha kike!
Hatari sana hawa mabwana wa U.S.A vita kwao ni biashara hiyo 2025 itakuwa zamu ya Taiwan.
 
Chumi mbili kubwa duniani zinazotegemeana ziamue kupigana kisa Taiwan au ?....


Hiyo hiyo China huiona Urusi kama mshirika inapowakabili wamagharibi vipi Sasa imshambulie ?.....japo waliwahi kuzozana mipakani enzi za Ussr hivyo lolote linawezekana.
Kweli mkuu possibility ya China kupigana na Russia au U.S.A kupigana na China au U.S.A kupigana Russia naona ni ndogo sana kutokana na sababu mbalimbali pia tusisahu hapa duniani lolote linaweza tokea na kuuacha ulimwengu mzima na mshangao.
 
Hatari sana hawa mabwana wa U.S.A vita kwao ni biashara hiyo 2025 itakuwa zamu ya Taiwan.
Ndio maana Mandela alisisitiza sana tupige kitabu sababu hawa jamaa vichwa vyao ni 5g

Saivi wanatuambia habari ya kuacha fossil fuels eti zinaiharibu sana dunia kana kwamba wao wanaijali sana dunia, kumbe wameshagundua mbadala wa hizo fossil fuels wanataka watupige T.K.O

Waingereza walipambana kuutokomeza utumwa sio kwamba walitupenda sana ama walitujali sana au kutuonea huruma la hasha! Historia inasema ilikuwa ni T.K.O kwa mfaransa.

Tuwapelekeni watoto wetu shule jamani!
 
Ndio maana Mandela alisisitiza sana tupige kitabu sababu hawa jamaa vichwa vyao ni 5g

Saivi wanatuambia habari ya kuacha fossil fuels eti zinaiharibu sana dunia kana kwamba wao wanaijali sana dunia, kumbe wameshagundua mbadala wa hizo fossil fuels wanataka watupige T.K.O

Waingereza walipambana kuutokomeza utumwa sio kwamba walitupenda sana ama walitujali sana au kutuonea huruma la hasha! Historia inasema ilikuwa ni T.K.O kwa mfaransa.

Tuwapelekeni watoto wetu shule jamani!
Kweli mkuu hawana mabwana ni smart sana bila kutumia akili ya ziada katika kupambana nao hakuna kitu cha faida tutavuna.
 
Kweli mkuu hawana mabwana ni smart sana bila kutumia akili ya ziada katika kupambana nao hakuna kitu cha faida tutavuna.
tungekuwa na akili kama za kwao wakati tunamkimbiza idi amini kule uganda leo hii tugekua tunashindana na sauzi naija na misri, tukatumia hasira na jazba tukavuna heshima ila njaa ikabaki palepale.
 
tungekuwa na akili kama za kwao wakati tunamkimbiza idi amini kule uganda leo hii tugekua tunashindana na sauzi naija na misri, tukatumia hasira na jazba tukavuna heshima ila njaa ikabaki palepale.
Kweli mkuu vita ni hesabu kali sana za kiuchumi, Trump alitaka kutumia mihemko kuanzisha vita na Iran lakini bunge likapinga amri hiyo kwetu huku hilo lingewezekana
 
Wakati wanapigana sisi huku tulime sana viazi na ndizi, tuzikaushe ziwe crips tukawauzie waheshimiwa masoja. Ndo kaelimu kangu ka la saba kameishia hapo!
 
Sitaki kuamini kama US hajipangi ipasavyo kwa Taiwan. Na hii itakuwa tofauti kabisa na kule kinachotokea Ukraine. Hii huenda ikawa ni piga nikupige, China ni lazima akubali ardhi yake pia imwage damu. Lazima vyuma vitue Hong Kong.

Hiki ni kipindi ambacho ambacho Taiwan atajisuka sana kiulinzi eneo la anga na majini. Marekani hanaga show mbovu kwenye masuala ya hujuma kama hizi.
Kuna simulation ilifanyika
US atapoteza Carrier 2. Ila atafanikiwa mpiga China
 
Haya mataifa makubwa ya kikomunisti yana tabia za kumega ardhi, nchi ndogondogo zinajihami mno dhidi yao.

Hapo Taiwan kuna siku kitawaka tu. Na hii kwa namna zote Taiwan ameshajiandaa, usipojiandaa kwa kutafuta washirika wa kuwa karibu yako kuna siku watakuvamia na watachukua eneo lako.
Waliwahi hongkong sababu ya kuwa karibu
 
Ni kweli kabisa kuwa China ana wakati mgumu kuhusu swala la Taiwan, lakini je tiafa la marekani hali fahamu madhara ya kuanzisha vita na taifa la kinyuklia ?
Mimi kwangu mbinu ya wao kuwauzia silaha Taiwan ni bora zaidi kuliko wao kushiriki hio Vita kwa taifa la kinyuklia wewe una onaje ?
Nuke ni dettarent tu
 
Wakati wanapigana sisi huku tulime sana viazi na ndizi, tuzikaushe ziwe crips tukawauzie waheshimiwa masoja. Ndo kaelimu kangu ka la saba kameishia hapo!
Hapa ndipo napowaza je serikali imejiandaa vipi na huo mgogoro unao tegemewa kuzuka baina ya haya mataifa mawili makubwa ya kiuchumi duniani huo mwaka 2025 ? Yasije kujirudia kama haya ya Ukraine na Russia na athari zake kwetu ?

Kumbuka hii itakuwa kati ya U.S.A na China wote wameshikilia uchumi wetu kwa asilimia kubwa.
 
Back
Top Bottom