SI KWELI Marekani na DRC wakubaliana katika mikataba ya madini adimu na ulinzi

SI KWELI Marekani na DRC wakubaliana katika mikataba ya madini adimu na ulinzi

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Serikali ya Marekani na DRC wamekubaliana kwamba marekani itaruhusiwa kuchimba madini adimu maeneo ya mashariki ya DRC wakati huo Marekani itatoa vifaa vya ulinzi, tekinolojia ya kijeshi kwa jeshi la DRC .

aidha pia kulinda maeneo ya kimkakati ndani ya DRC.

Hayo yamejiri baada ya Rais wa DRC Felix Etiene Tshisekedi wa Mulumba kukutana na maafisa wa Marekani na kuwekeana mikataba kadhaa ya ushirikiano sambamba na kuwaondoa waasi wote ndani ya DRC.

IMG-20250306-WA0008.jpg
 
Tunachokijua
Kwa sasa, Marekani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) bado hawajasaini makubaliano mapya rasmi kuhusu madini. Hata hivyo, kuna mazungumzo yanayoendelea kati ya pande hizo mbili kuhusu uwezekano wa mpango wa kubadilishana madini kwa msaada wa kiusalama.

Mpango huu uliopendekezwa unahusisha mashirika ya Marekani kupewa haki za uchimbaji na usafirishaji wa madini muhimu, huku Marekani ikitoa msaada wa kiusalama, mafunzo, na vifaa vya kijeshi kwa jeshi la DRC. Hata hivyo, mazungumzo haya bado yapo katika hatua za awali, na hakuna mkataba rasmi uliosainiwa.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imethibitisha kuwa wako wazi kwa kushirikiana na DRC ili kuhakikisha maendeleo ya rasilimali zake za madini kwa njia inayowajibika na yenye uwazi.

Kwa hivyo, ingawa mazungumzo yanaendelea, hakuna mkataba rasmi kati ya Marekani na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuhusu uchimbaji wa madini na msaada wa kiusalama kwa sasa.
Wamarekani wamemuhakikishia kwamba watailinda Congo milele? Au alindwe yeye tu kipindi Cha uongozi wake then akitoka ngoma ibaki pale pale? Alichokifanya sio njia ya kutatua mgogoro wa hapo Congo bali ni ujinga mtupu.

Congo haijapata kiongozi mwenye uchungu na nchi yake, That' why sijaona kiongozi mwenye lengo la kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa migogoro Kila anae ingia ikulu anatafuta namna ya kujilinda binafsi
 
Ameamua hasa na kuufutilia mbali mkataba wa Lemela ulitaka kuwatambua watusi na kuwpa nafasi za ajira nyeti ingawa alichelewa lakini walioingia wanakiona cha mtema kumi nl hasa familia zao
Wakongo wako sahihi kuwakataa watutsi, huo ni ushindi mkubwa sana wakati wanaendela kupambana kuweka utulivu kwenye nchi yao. Tena wapambane hadi watoke kabisa warudi kwao Rwanda.
 
Hiyo inaitwa tukose wote.
DRC watakosa madini.
Rwanda watakosa madini.
Marekani watapata madini, DRC watapata amani pengine na maendeleo kidogo.
Hapo Tshekedi anataka kuwakomoa watutsi na kama ameona hakuna option nyingine basi kwa kiasi fulani yuko sahihi maana Rwanda ikiwa na uchumi mkubwa amani ya DRC itaendelea kuzorota kwahiyo anaona bora watoe madini kwa mmarekani yachimbwe kihalali na walipe kodi kuliko kuchimbwa kihuni na Rwanda yakauzwe nje halafu pesa ikaendeleze maisha ya watutsi huku wakongo wenye nchi yao wakiteseka.
 
Serikali ya Marekani na DRC wamekubaliana kwamba marekani itaruhusiwa kuchimba madini adimu maeneo ya mashariki ya DRC wakati huo Marekani itatoa vifaa vya ulinzi, tekinolojia ya kijeshi kwa jeshi la DRC .

aidha pia kulinda maeneo ya kimkakati ndani ya DRC.

Hayo yamejiri baada ya Rais wa DRC Felix Etiene Tshisekedi wa Mulumba kukutana na maafisa wa Marekani na kuwekeana mikataba kadhaa ya ushirikiano sambamba na kuwaondoa waasi wote ndani ya DRC.
Haya ndugu; "Kuhani" ameshaingia madhabahuni; tukae kimya. "Ibada" itaanza sio muda mrefu. Wanakwaya anzisheni nyimbo hapo chap'.😀😀
 



Lini ulisikia wamevamia nchi ya watu kuiba rasilimali?
Kwahiyo kuvamia na kuiba rasilimali ndiyo criteria pekee unayoitumia katika kuhitimisha uadui?

Btw, chalenji ndogo tu, hapo mlangoni tu pa kuingilia nchini mwako yupo mzungu? Huko Serengeti wamasai wanahamishwa kwaajili ya nini?

Unajaribu kusafisha kaniki ukitaraji litakuwa jeupe. Hayo majitu unayoyasifu hata wewe mwenyewe hayakupendi hata uishi msikitini ukiswali masaa 24
 
Bwana Mulumba kalamba galasa zito sana pale. Hiyo vita haitakaa iishe mpaka pale marekani watakapojaza akiba ya madini hayo huko kwao. Wamefanya mambo haya kwingi tuu duniani. Kwa kufanya hivyo, DRC imekaribisha mauaji ya kikatili zaidi kutokea na makundi mengine hata ya kigaidi sasa yataibuka pale. Sisi majirani tujipange na uharibifu huu kwa jirani.
 
Unampa marekani madini wewe unapewa vifaa vya ulinzi

ALIETULOGA WAAFRICA AISEE
Congo kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe, nchi haina umoja sio kama Ukraine ; Tshekedi anapata wapi ujasiri wa kuingia mkataba wa kuwapa marekani haki ya kuchimba madini tena sehemu zinazomilikiwa na M23?
Tshekedi anakuwa kibaraka wa marekani kama Mobutu ; hawezi kudumu atapinduliwa muda si mrefu.
 
Ndio maana humshangaa MTU anaechukia waarabu,adui wa mtu mweusi ni mzungu
Wewe ndo hujui jinsi gani waarabu wanabagua watu weusi heri mzungu au mchina kuliko mwarabu...utumwa ulianzishwa na wao hadi leo bado wanaendelea kuhasi wanaume weusi na kuwafanya watumwa..
 
Back
Top Bottom