Maria Sarungi: Hili la ahadi ya JWTZ kumtii Samia Suluhu sio la kawaida

Maria Sarungi: Hili la ahadi ya JWTZ kumtii Samia Suluhu sio la kawaida

Kwa jinsi alivyoongelea namna jeshi lilivyoshirikishwa kwenye miradi ya serikali na hata kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali kama ukuu wa mkoa na hususani akaongelea kuhusu ujenzi wa ukuta na ulinzi wa mgodi wa Tanzanite, utaelewa namna jeshi kwa sasa lipo strategically kwenye swala la kuweka jicho kali na hata kujihusisha kwenye kuendesha na kumiliki rasilimali za nchi, labda kwa maslahi ya nchi kijeshi na kiuchumi. Viongozi wa kiraia wanapoongozwa na mihemuko, uchu wa madaraka unaoendeshwa na maslahi binafsi kama ambavyo tumekuwa tunashuhudia namna mabilioni yanavyotumika kununua uongozi kwa baadhi ya makundi ya watu ndo unaona namna jeshi linavyochukua uthibiti na kuendesha mambo muhimu angalau kwa mlango wa nyuma.....
 
Unamtoa cdf wakati umri wa kustaafu bado alafu unaweka mwingine, huyu cheo chake kinakua kipi? Akisema hataki kustaafu kwa hiari utafanyaje? Toka historia ya jeshi inaanza hapa tz haijawahi tokea una generals 2 wote wako ofisini...
Mkuu hicho cheo si anapewa pia anaweza kuvuliwa?au hiki cheo huwa kinapatikana vip?naomba elimu hapa mkuu.
 
acha kuota nawewe.

mh suluhu tokea ameapa ni wiki moja na ushee tuko na mwili wa marehemu,ambao zoezi zima linasimamiwa na JWTZ,shughuli ya jeshi kwenye mwili wa mpendwa wetu imekwisha jana.hutona tena uliyoyaandika hapo.

itifaki ni jambo kubwa,ukileta ujuaji unavuruga kila kitu.
Ila kama umeangalia seating arrangement kuna mjeda yupo karibu sana na siti ya rais, achana na adc wake...hiyo ni uncommon..
 
Kwa jinsi alivyoongelea namna jeshi lilivyoshirikishwa kwenye miradi ya serikali na hata kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali kama ukuu wa mkoa na hususani akaongelea kuhusu ujenzi wa ukuta na ulinzi wa mgodi wa Tanzanite, utaelewa namna jeshi kwa sasa lipo strategically kwenye swala la kuweka jicho kali na hata kujihusisha kwenye kuendesha na kumiliki rasilimali za nchi, labda kwa maslahi ya nchi kijeshi na kiuchumi. Viongozi wa kiraia wanapoongozwa na mihemuko, uchu wa madaraka unaoendeshwa na maslahi binafsi kama ambavyo tumekuwa tunashuhudia namna mabilioni yanavyotumika kununua uongozi kwa baadhi ya makundi ya watu ndo unaona namna jeshi linavyochukua uthibiti na kuendesha mambo muhimu angalau kwa mlango wa nyuma.....
Hata hivyo jeshi halitakiwi kupewa mamlaka ya kiraia siku zote. Next time hatokuwepo muadirifu kama Mabeyo utapata matokeo kama Nigeria, Pakistan, Egypt na Myanmar zinavyoongozwa. Kule Pakistan unakuta jenerali mstaafu wa kikosi cha mizinga ndio anateuliwa kuongoza shirika la umeme, very incompetent kwenye hiyo sekta.

Jeshi liwe mfumo kama UK walivyo. Hakuna kuhusika na uraia hata kidogo na kuna ufanisi katika hili.
 
Mkuu hicho cheo si anapewa pia anaweza kuvuliwa?au hiki cheo huwa kinapatikana vip?naomba elimu hapa mkuu.
Sawa anapewa, ila unamvua alitaka fanya coup d'etat au kuna sababu nyingine ya msingi? kum-demote general kuwa luten general sio kazi rahisi kama unavyoongea hapa, lazima uwe na sababu ya msingi..
Kumvua tu ili kuweka mtu wako bila ya kuwa na sababu ya msingi labda kafanya mutiny au ame plot coup d'etat sababu nyingine haina mashiko...i dont think madame president is this dumb...
Kama ni kumtoa mabeyo ni asubiri afikishe umri wa kustaafu kisha ataweka mtu wake! Cdf sio kama igp...
 
seating arrangements ya jana kwa wote tulioangalia LIVE inatosha kuonyesha Taifa nani wako nyuma ya Urais wa Mh Samia
Ile hotuba ya CDF ni warning ya wote walioficha kifo cha Rais ili “wapindue” serikali !!!! ni ONYO !!
TPDF inaenda kusimamia reforms ndani ya IDARA YA USALAMA SOON

Brig Ibuge a TPDF man ndio anasimamia affairs za ikulu na sio Bashiru
Kumbukeni alishahamishiwa Foreigh kama Katibu Mkuu lakini toka samia wa samaki ameingia yeye ndio anaonekana right hand kila mahali mara nyingine kama role ya mkuu wa itifaki na “Katibu mkuu kiongozi”
na mara zote katibu mkuu kiongozi amekalishwa nyuma kule kama wageni waalikwa wengine .. show zote ndani ya ikulu mnajua sasa nani anasimamia
wale ambao bado hawaelewi waendeleee kujaribu waone!!!!
Mkuu wa majeshi muda wote alikuwa anakaa jirani Mh Rais badala ya kukaa na wakuu wengine wa vyombo vya ulinzi na usalama! Means bado Jeshi linaendesha show hadi "idara" zinyooke!
 
Na kwa Nini CDF aeleze kitu ambacho wote tunajua kuwa ndio wajibu wake ...msisitizo wa Nini!! ???
Utakua ndio mara ya kwanza kusikiliza hotuba kutoka katika vyombo vya usalama mwaka 2019 wakati wanaapisha maafisa wapya Arusha CDF alitoa kauli hiyo mbele ya JPM. Si kitu kipya at all ingekua kinyume chake ingekua mada ya mjadala.

By the way utii wa vyombo vya usalama ni kwa kauli ni vitendo. Na tukisema utii ndio principle namba moja katika mafunzo ya jeshi.
 
Sawa anapewa, ila unamvua alitaka fanya coup d'etat au kuna sababu nyingine ya msingi? kum-demote general kuwa luten general sio kazi rahisi kama unavyoongea hapa, lazima uwe na sababu ya msingi..
Kumvua tu ili kuweka mtu wako bila ya kuwa na sababu ya msingi labda kafanya mutiny au ame plot coup d'etat sababu nyingine haina mashiko...i dont think madame president is this dumb...
Kama ni kumtoa mabeyo ni asubiri afikishe umri wa kustaafu kisha ataweka mtu wake! Cdf sio kama igp...
Ok..lakini kwa kuwa cheo anapewa na raisi hivyo hivyo raisi akiamua anamvua,,sema huenda ikawa chanzo cha matatizo mengine.
 
Cha kwanza atambue kuwa huyu mama ni kaimu Rais na sio raisi wa kupigiwa kura katika uchaguzi. Hivyo kila mtu anakuwa anamtilia mashaka sababu kuingia kwake katika hii nafasi ni matokeo ya kifo cha aliyekuwa raisi kamili kimamlaka.

Shaka na hofu ni vitu vya lazima kuwapo pale mwanamke anapopewa wadhifa mzito na wenye majukumu mengi kama haya sababu inajulikana wazi kabisa hizi kazi za uongozi wanawake miaka hii wanaziingia kwasababu ya propaganda za kimagharibi za haki sawa ila kiuhalisia si kazi wanazoweza kuzifanya kwa umakini na umahiri wa hali ya juu......
 
Ukiona baba wa familia anasema mimi ni baba ujue kuna kitu hakipo sawa..Kauli ya mama kusema mimi ni Rais tena mwenye maumbile ya mwanamke na kurudia kwa msisitizo ili hali wote tunajua kuwa ni hivyo ujue kuna kitu kipo nyuma yake na kuna kundi linampinga

Jana Mabeyo kaongea kitu ambacho kipo kikatiba ....ni jukumu lao kumtii Amiri Jeshi Mkuu weather aongee au akae kimya...kwa nini kasema....meaning kuna watu waliokuwa wanapewa ujumbe kuwa wasithubutu kufanya ujinga kwa mama yetu as Jeshi litatimiza wajibu wake wa kumtii

Refer hotoba zote zimetamka tamko la Rais alilotoa Dodoma na kuahidi kumpa ishirikiano...Rais kaongea vingi ikiwemo upendo na ushikamano but heading imekuwa ile statement .....kwa hiyo ni kama wanampa uhakika kuwa wapo nae pamoja na wanatambua nafasi yake
 
Hana mume, hana ndoa, hana watoto, umri umeenda hapati attention ya usichana maana kashakuwa mama.

Haya ndio madhara kwa mwanamke ya kupita ujana bila kujenga mahusiano ya ndoa na kuwa na familia bora ya baba, mama na watoto.

Mtu anakuwa kama kichaa hafikirii sawa.
 
Maelezo haya ya CDF, licha ya kutufurahisha Watanzania , lakini kuna mengi nyuma ya pazia.
Mkikumbuka Mama Samia akienda kuapishwa alisindikizwa Ikuu na CDF na si UWT.
Hili linaeleza mengi.

UWT tayari walikuwa compromised au inawezekana hawakuweza kulidhibiti kundi lililokuwa linataka kumwengua Mama Samia kuchukua madaraka.

Haya yanatokea duniani.
Mao Tse Tung kiongozi wa China alipofariki mwaka 1976, walijitokeza makada wake wanne waaminifu na maarufu waliojaribu kuteka madaraka, akiwemo mke wake wa tatu(The Gang of Four).
Makada hao walidhibitiwa na kukamatwa hatimaye walipelekwa mahakamani na kuhukumiwa kunyongwa.

Kiongozi aliyeingia madaraka alikuwa baba wa uchumi wa China sasa hivi, Deng Hsiao Ping.

Tujifunze kwa wenzetu.
Sasa hapa kwetu inabidi hilo "Gang of Four" kwanza liwe exposed, na pili liwe purged.

JWTZ wamefanya a commendable job ya kudumisha katiba na tukumbuke kuwa sisi raia hatujui, lakini JWTZ ina Idara yake ya Usalama ambayo iko vizuri sana.
 
Back
Top Bottom