Tetesi: Marufuku ya kuzidisha abiria ili kupambana na Corona, Daladala zimeanza kugoma Dar es Salaam

Tetesi: Marufuku ya kuzidisha abiria ili kupambana na Corona, Daladala zimeanza kugoma Dar es Salaam

Wakuu,

Serikali imepiga marufuku daladala kusimamisha na kujaza abiria, taratibu ambao haukuzoeleka sana haswa kwa jiji la Dar.

Mimi nikiwa mmoja wa wamiliki wa daladala hizi naishauri Serikali mambo machache haswa katika kipindi hiki cha mpito kwakuwa Serikali imesema daladala itakayosimamisha abiria itapigwa faini laki Tisa au gerezani miaka miwili ifanye hivi ili kubalance situation.

Mfano daladala ikitoka mbezi hadi Temeke umbali wa kilomita 37 Kila abiria analipa 600 na daladala moja inasiti za abiria 26 hadi 22 akifika temeke anakuwa anapata 15600tsh hadi 13200tsh ambapo kwa umbali huo gari inaweza kutumia lita 5 ambapo ambapo ni sawa na tsh 11000.

Sasa Kama gari hadi inafika Temeke imekusanya 15600 za nauli ukitoa mafuta 11000tsh inamaana daladala hi itabakiwa na 4600.

Sasa kwa namna hii je huyo dereva atapataje hesabu na posho yake ya kila siku, bado kuna zile pesa za kupigia kiwi za jamaa zetu wale aliosema mkuu ambapo kwa siku nzima huenda zikafika 10000 tena hizi huwa hazinaga ubishi lazima utatoa tu.

Ushauri wangu, Serikali ipunguze bei za mafuta kwa daladala zote ikiwezekana iwe na vituo vyake vya mafuta na maduka yake maalumu ya vipuri pia Serikali itafute muda ikae na wadau husika lakini sio kufanya maamuzi bila kushirikiana na wadau watakaoteseka ni wananchi wakawaida wanategemea magari haya.
gomeni hakuna shida...
 
Ukiona biashara hiyo hailipi acha fanya mengine yenye maslahi mkuu, watu waambukizane korona kisa nyie kupata hela?
hawa watu wa daladala wana tamaa sana asee, kila wakati wao wanataka super profit hata wakati wa majanga, hawajui kusoma alama za nyakati kabisa...
 
Mkuu sio lazima iwe mbezi--- temeke,

mimi naenda g.lamboto---ubungo,
Kituo cha kwanza kuanza kushusha ni buguruni. Ukitoka hapo ni stand ya mkoa!

Natumia mafuta ya tsh. 13,000. ( Kwenda tu)

Level seat ni abiria 42 nauli ni 500. Napata 21,000 tu.

Labda kwa bahati baada ya kushuka watu, wapande wengine 10(ni wengi sana!)
Nitakuwa na jumla ya tsh. 26,000×10 (trip ninazoenda kwa siku. Nikikomaa sana naenda 12. Ambazo ni =312,000.

Pia kuna mida ya mchana abiria sio wengi.

Matumizi kwa wafanyakazi 3 kwa siku tsh. 20,000.
Kubrash viatu 10,000.
Mafuta 130,000.
Hesabu ya gari 140,000.
Kulaza gari na kuliosha 7,000.
Jumla ni 307,000.

312,000 kutoa 307,000!?

Kama serekali inawajali wanyonge wanaotumia usafiri wa uma, ingeangalia namna nzuri ya kufidia hasara inayotokea ili wanyonge waendelee kupata huduma ya usafiri.

Vinginevyo daladala zitashindwa kujiendesha na zote zitapaki"

Sent using Redmi Y2
Nimekuelewa mkuu lakini naomba kuuliza; bus mfano Eischer ukilinunua jipya unaweza kulitumia kwa muda gani?
 
Kwa utaratibu huu itakuwa vigumu sana. Biashara ya dalal dala ni ngumu sana. Mfano hapo Mwanza dalala kwa kawaida inatoza Tshs.400 kwa tripu na nyingi zina viti vya abiria 15 kwahiyo kama ni level seat itachukua abiria 15 @ 400 = 6000 na kwa siku inaenda safari 20 yaani kwenda safari 10 na kurudi safari 10 na hivyo Tshs.6000x20 Tshs.120,000. Mafuta kwa siku ni kama lita 30x2260 = Tshs.67,800, Hela ya Tajiri kila siku Tshs.50,000. Hela ya wale wajamaa Tshs.5,000, Hela ya dereva na tingo Tshs.20,000, Mafuta kwa siku inayofuata Tshs.67,800. Hvyo gharama yote kwa siku ni Tshs.210,000. Mapato kwa siku ni Tshs.120,000 - 210,000 (-90,600) ambayo ni hasara. Kwa utaratibu huu itabidi Serikali ikae chini na Wadau wote wanaohusika na usafiri ili muafaka upatikane.
 
Wamiliki punguzeni hela ya makusanyo ya siku.
Pia bei ya mafuta ipunguzwe ili tuweze kufikia malengo.
 
...Tatizo linakuwa kwa abiria was vituo vya njiani!
Wakiifuata sheria hiyo basis abiria wengi was vituo vya katikati hawatasafiri...ushahidi kamili kuwa mabasi bado in machache sana jijini...!!!
Level seat kwa daladala za Dar mmh haiwezekani, kuna kipindi walileta hii sheria ila iligonga mwamba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uganda wamepiga marufuku kwa wiki 2 usafiri wa umma,boda boda na mambo kama hayo.
 
Sasa Kama daladala zikijaza bado raia wanapelea kusafiri hii SI italeta tatizo upya?,au ratiba zibadilike,daladala zianze kazi saa Tisa usiku mpaka saa Saba usiku na nauli ipande kidogo,maana level seat kea nauli ya Sasa,watu watapack magari tu
Mkuu kwa dar, daladala zinakesha , zipiga kazi 24 hours, labda kwa mikoani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunasubiri tamko moja tu la kila atulie nyumbani kwake hakuna kutoka nje/kuzurura hili la kuzuia msongamano kwenye madaladala kulikontroo ni vigumu
 
Unaenda mjini kufanya Nini?
Vyuo vimefungwa,shule zimefungwa.

Level seat kwa daladala za Dar mmh haiwezekani, kuna kipindi walileta hii sheria ila iligonga mwamba.
 
Back
Top Bottom