Masheikh wakiamua kuingiza siasa kila kipindi cha swala itakuwaje

Masheikh wakiamua kuingiza siasa kila kipindi cha swala itakuwaje

Chama cha CUF ndio kilikuwa Chama cha misikitini, tatizo masheikh wengi hawana elimu wamesoma Quran tu.

Baraza la maaskofu linaundwa na PhD na degree holders tu, lile ni zaidi ya baraza la mawaziri.
Ndio wale degree na PHD holders waliopata mgao kwenye escrow??😀😀😀
 
Magaidi hawana uwezo wa kuandika waraka.
Kwakua nyie mnajiona special Sana. Jamaa kasema kweli na waislam wakilianzisha bandari apewe mwarabu kwakua Ni muislam utalaumu? Hapata kalika cha msingi huu waraka hata ambao si catoliki tumeulewa na uko poa kwaajili ya maslahi ya wote Mambo ya kuingiza dini kila kitu itafikia kipindi kila dini unataka kiongozi wake hivyo huo waraka ilitakiwa urushwe tu kila mtu aupate sio kwenda kuusomea kanisani
 
Kwakulinda Mali za nchi waingize tuuuuu usimtishe mtu nguruwe weee
Kanisa na ccm ni chanda na pete hakuna mwenye huruma na watanzania tusiwe wajinga ccm tunaijua vizuli hata makanisa tunayajua vizuli hapa nikionacho ni masilahi tu
 
Huelewi ulicho andika. Sijui kama walau umesoma kabla ya kuposti. Wala hunavuzoefu juu ya hili kanisa lililo jengwa juu ya MWAMBA.
Kanisa halina urafiki na wakirito wala waisilamu wala wapagani rafiki ya kanisa ni pesa tu,ukichunguza vizuli utaona kama wanatetea watu kumbe wanatazama masilahi yao tu utaki kuamini basi sikulazimishi
 
Ubinafsishaji wa bandari kwa wageni ni siasa!!?? Kanisa linapinga ufisadi, hilo ni jukumu la kila mtanzania kuipigania nchi yake, kanisa limetimiza wajibu.
Kidogo viama viasiasa naweza kusema viko sawa kupinga sababu havija shika nchi tukaona uzuli na ubaya wao,likinkini makanisa tunayajua hayana tofaoti na viongozi wa ccm katika kujirimbikizia mali,ukitaka kuamini wewe mkirito nenda hosipitali tena umevaaa msalaba mkubwa shingoni huko hoi alafu huwe na pesa pungufu uone uzuli wa hosipitali ya kanisa
 
Ni kweli hao Masheikh hawajui vitu vingi wanaojua vitu vingi ni hao Dp world ndio maana serikali imeamua kuwapa hiyo Bandari kuwekeza
Hata kanisa halipo kumtetea mtu tofaoti na masilahi yake kweli mkataba ni mbovu lakini kanisa halina urafiki na mtu bhana bora ya lissu
 
Bro issue siyo tamko pekee, je wanahoja ya maana ya kutolea tamko?? Kwani tec wametoa tamko la kupinga uislamu? Kama masheikh wanaungana na tec kutoa tamko la kupinga mkataba wa DP itakuwa saf Sana. Hizi hoja za kuchonganisha dini ni ujinga wa juu mno. Sisi ni Watanzania,anayeuza nchi ndiyo adui wetu na si hoja za maaskofu na masheikh wala ukristo na uislamu.
Hata kkkt na sabato wamepinga waraka huo
 
Hivi kwanza siasa ni nini? Aliyewaambia huo waraka ni mambo ya siasa ni nani? Rudini shule mjifunze walau mambo madogo kama haya kuepusha aibu ndogo ndogo.
Wewe kama msomi siasa nini maanake?
 
Waislamu huwa wanakutana mara tano kwa siku katika swala na mara moja kwa wiki siku ya Ijumaa.Kiuhakika waislamu wanakutana kwa wingi katika wiki kuliko wakristo.

Masheikh nao wakiamua kuachana na hofu inayowakataza kutochanganya dini na siasa na kuanza kutoa matamko misikitini sijui kama wengine wataweza kivumbi hicho.

Kwa ujumla tamko la TEC kusoma waraka makanisani na kutekeleza leo ni kama kwamba wamejinyea na kujiingiza kichwa kichwa kwenye jambo litakalowaporomoa kutoka pale walipo.Ama wamkane padre wao au wakubali wamechokoza pasipohitajika.

Uamuzi wa NATO kuingia vitani Ukraine na ECOWAS kupeleka jeshi Niger ni sawa na kanisa katoliki kusoma waraka wa bandari makanisani mwao.
Upuuzi mtupu. Kama mashehe watakuwa wanatoa mahubiri kila wakati wa ibada yao kuikosoa serikali pale wanapoona kuwa imekosea wananchi wake wa dini zote itakuwa wanaisaidia serikali na wengi tutawashukuru.

Tatizo ni kuwa mashehe wengi wanakuwa na ujasiri pale tu wanapoona kuwa waislamu wanaonewa kama wanavyofanya sasa. Badala ya kuangalia suala zima kwa mapana yake wao wanajikita kuwatetea watu wa dini yao.

Huo ndio udini unaokatazwa. Tamko la TEC linazungumzia wananchi na sio wamisheni peke yao. Kama mashehe wana hoja za kupinga yaliyomo katika waraka huo wafanye hivyo maana wataisaidia jamii. Kisichokubalika ni huku kuacha kuzungumzia yaliyomo katika waraka na kuzungumzia dini ya waliouandika. Mtazamo huo ndio utatufikisha pabaya.

Amandla....
 
Hao wote uliowasema na huo utajiri wao walivyoupata, kwa hakika tajiri kuuona ufalme wa mbinguni ni sawa na ngamia kupita tundu la sindano ,bila sisi kula hizo chapati zao na kupikia gas zao si nao wangekuwa malofa tu sisi ndio tumewatajirisha mkuu.
Basi ndo ujue duniani kila mtu muhimu. Msomi anamtegemea asiyesoma na asiyesoma anamtegemea aliyesoma.
 
Kwa taarifa tu mtoa mada, inawezekana ukawa ni mdogo kiumri au huna taarifa za kutosha. Nitakupa matukio mawili yaliyohusisha siasa kwenye msikiti wa Mtambani pale Kinondoni Manyanya miaka kadhaa iliyopita.

Tukio la kwanza lilikuwa ni la kugomea zoezi la sensa ya mwaka 2012. Uhamasishaji ulifanyika msikitini na walihamasishana siku hiyo kutokulala majumbani kwao. Waliahidiana kuchinja ng'ombe ili watu wale. Makarani wa sensa wasikute watu nyumbani.

Tukio la pili lilihusisha hamasa za kuchagua viongozi fulani wakati wa uchaguzi wa 2015. Lilitokea hapohapo Mtambani. Kiongozi mmoja wa dini aliwahamisha wamchague mtu 'A'. Kiongozi mwingine alihamasisha wamchague mtu 'B'. Kutokana na kuyumbishwa huko, waumini walifanya fujo baada ya kuona viongozi wao wanawayumbisha.

Je, haya hayakuwa masuala ya kisiasa kwenye nyumba ya ibada?
 
Kwahiyo?? unataka kusemaje
Una hasira sana
Elimu ni bahari


Viongozi wenu hawajazuiliwa kwenda kusoma,😂
Ila PhD kuipata siyo lelemama kama kula maandazi.


Viongozi wa katoliki shule imelala kichwani
Hakuna Father kilaza hata mmoja.
 
Una hasira sana
Elimu ni bahari


Viongozi wenu hawajazuiliwa kwenda kusoma,😂
Ila PhD kuipata siyo lelemama kama kula maandazi.


Viongozi wa katoliki shule imelala kichwani
Hakuna father kilaza hata mmoja.
Sijaona point ya msingi
Phd ni ada tu watu wanashindwa mudu
Hata hao jamaa bila ufadhili wasingetoboa

Alafu usichokijua unaweza ukawa na phd na ukawa mpuuzi tu, tunao wapuuzi kibao na mnawaita wasomi
 
kuna vitu hufahamu
waislamu huswali mara 5 kwa siku, ila si mara zote wakiwa kuswali wana toa mawaidha
hizo swala zao hazichukui hata dk 5, ila ijumaa ndo hutoa mawaidha

ko hakuna jipya, hawata fanya chochote maana ni kuswali bila mawaidha
 
Sipati picha dp world angechukua mzungu kama zingekuwepo kelele dah 😄 kwa mwarabu imekua (HAPANA)

Waarabu njooni muwekeze jamani, ninyi watu wazuri, wakarimu na muna huruma, welcome aise
 
Back
Top Bottom