Masikini, wavivu na watu wenye roho mbaya walikuwa wakifurahia hatua za Magufuli kuturudisha kwenye UJAMAA

Kuanzia Nyerere mpaka sasa ni unyonyaji na ufukarishaji.


Vyama vya Ushirika vimekufa, majirani zetu kenya wamejifunza kwetu ushirika, sasa hivi vyama vya ushirika ke vina nguvu kubwa sana kiuchumi.

Nyerere angeacha vikastawi tz tungekuwa wapi?

Nyerere ilitakiwa achukue mazuri ya wakoloni ndio aendelee nayo.Yeye aliacha hata mazuri ya wakoloni
 
Hakuna kipindi nilikuwa mzalendo kwa nchi yangu kama kwenye utawala wa JPM nlikuwa na wivu na nchi yangu hatari. Kila aliyehujumu choxhote nlikuwa mkali as if ananiibia mimi
 
Ndo mda pekee nlianza kufanya kazi za ofisi hadi usiku bila kuchoka. Ila sasa ikifika saa tisa na usu naondoka wjether imeisha ama la
 
Wewe mbuzi nini? Fanya kazi na utakula kwa jasho lako. Wewe kaa hapo fuga tu kucha huku ukiomba matajiri wafilisiwe ili wewe ule
Una ma-emotion sana
We ni mwanamke?

Jitulize kabla ya kuongea na mtu
 
upo Sawa mkuu lakini tujadili hili la nyongeza ya Kima cha chini asilimia 23% je yule mzalendo aliweza kuongeza Ata senti 5 jibu ni hapana alishindwa

je ajila kipindi cha huyu mzalendo zilikuaje jibu ni holaaa

ukija kweny point ya vitu kupanda bei huu ni mfumuko wa dunia nzima kweny Biashara Kuna demand and supply kitu kikiwa hadimu obviously kita kua na thamani
unajua uzalishaji ulipungua kwa asilimia ngapi kipindi cha Korona? bidhaa nyingi na chakula tunategemea kuingiza kutoka nje Leo unalalamika Unga kununua 2000Tsh per kg je unajua viuatilifu mbegu mbolea na madawa tunaagiza nje na vyote vimepanda bei kutoka na athari za Korona? ujajua mfuko mmoja wa mbolea ni 130k bado unataka mkulima auze debe 5000 Tsh.?
vip kuhusu kupanda bei kwa mafuta kutokana na mgogoro wa Russia? na unajua bidhaa zote Zina tegemea mafuta kwenye transportation mafuta yakiwa juu na bidhaa nyingine lazima zipande bei mkuu je Tanzania tuna visima vyetu vya mafuta? hahaha jibu unalo

OK vitu vingine tumia uhalisia vipi kilimo cha msimu huu kulikua na uzalishaji wa kutosheleza.? jibu ni nope kwa sababu tunategemea kilimo cha msimu wa mvua je huko kwenu hamkulia mvua hamna? jibu unalo vitu vingine tusitumie chuki tumia logic mkuu
 
Yaani masikini halafu uelewa mdogo. Ni bora ya mchawi mwenye digrii moja au Phd. Maskini sisi tuna mambo kweli
Huo mstari wa kwanza uelewa mdogo na uchawi ndani yake mnakoma si ndugu wala jirani wote vibano mnavipata
 
Mwenyewe una utajiri gani? Vibajaji viwili na banda unajiweka kundi la tajiri😂. Magufuli aliungwa mkono na wasomi na watu wako vizuri tu sio unawaita maskini.
Mnajidai kupenda ubepari wakati wala sio ubepari mnafanya ila kufanya magendo kuibia umma na kutumikia maslahi ya ubeberu wa kimataifa. Kwa msingi huo kamwe nchi haiwezi kuendelea.
Isitoshe itikadi rasmi ya ccm ni ujamaa na kujitegemea. Ccm ilishabadili mkakati jinsi ya kujenga ujamaa. Badala ya kutumia sekta ya umma sasa ni kutumia sekta binafsi.
Ili kufanikiwa sekta binafsi lazima kudhibitiwa na serikali. Kilichotokea kikawa tofauti Ikawa sekta binafsi kudhibiti serikali kutokana na ufisadi wa viongozi.
Jpm alirejesha hali kuelekea nchi kujenga ujamaa kwa kudhibiti sekta binafsi.
Sasa fisadi na wapiga dili mnafurahia hali ya sekta binafsi kudhibiti serikali kurejea.
 
Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule kiongozi muovu bila damu kumwagika.
tukuone basi wewe ukitajirika kwa kupiga hela ya umma. Huyo muovu lake kubwa ilikua kupambana na ufisadi serikalini, kukusanya kodi na kusimamia miradi ya maendeleo. Kama wewe uliona ni uovu bila shaka utakua mtu fisadi.
 
Thus alishindwa,sekta binafsi ndio nguzo ya uchumi.Ujamaa ubakie kwenye mgawanyo wa huduma za Jamii na sio kwenye msingi wa uzalishaji.
 
Hakuna kipindi nilikuwa mzalendo kwa nchi yangu kama kwenye utawala wa JPM nlikuwa na wivu na nchi yangu hatari. Kila aliyehujumu choxhote nlikuwa mkali as if ananiibia mimi
hukuawai kuwa mzalendo unajua maana ya uzalendo ww? kupenda nchi na sio mtu nachukua watu wa dizaini yako walio jipa uzalendo wakizani mfalme ni mungu ataishi milele ungekua mzalendo ungeonesha saiz jinsi unavyo fanya iyo Kazi ambayo ulikua unafanya mpaka usiku ili ulete tija na kuongeza ufanisa wazalendo wapo mpakani hawalali ili wewe ulale Salama huu ujinga nimeusoma kwako Zaid ya Mara moja (sorry kama nimetumia lugha mbaya no hard feelings dude)
 
Kipindi cha magu niliusika kwenye ujenzi wa majengo ya hospital ela ilikuwa on time ushindwe wewe na uvivu wako, now tangu mwezi wa sita tunazungushana pesa as if hazipo hadi zimerudi kisa kuombana rushwa na maengineer,procurement officers na uzembe wa DED yaan hadi kero.

Nashangaa hili bandiko lako kuna uwezekano mkubwa utakuwa wapenda shortcuts sana
 
Wajinga sana hawa watu.
Brain washed personel
 
Wewe ni ndezi sababu hasa watu tuliompendea Magufuli ilikuwa ni kuleta usawa. Haijalishi mlimchukia kiasi gani ila kila mtu aliefanya kazi alikuwa anaiona hela na kulikuwa na boost ya watu kufanya kazi hasa wa hali ya chini.

Huduma za kijamii zilikuwa zina tija hata ukienda maofisi ya serikalini ulikuwa unasikilizwa na kutatuliwa shida zako kwa wakati. Nidhamu ya kazi ilirejeshwa.

Msichanganye ubepari mnaotetea ni wizi na ubadhirifu wa mali za umma. Yani kwakuwa mlibaniwa mianya ya kudokoa ndio mnamuita Magufuli mjamaa sijui dikteta. Huo ujinga utawatesa kwa sababu tunahitaji kiongozi mwenye calibre ya Magufuli kututoa hapa tulipo. Gari imekwama bila 4-wheel drive!

Sahizi mmeruhusiwa ku edit mikataba kujiwekea 1O% maana boss hafatilii, tozo kibao, semina na warsha za kujiachia mnaandikia tu. Huku mtaani hali tete wanyonge wamefanywa wanyonge kweli kwa inflation za hali ya juu.
 
Zamu ya masikini kuisoma namba kupitia gharama za maisha na vitu bei juu, maana mlitucheka Sana sisi matajiri na wapinzani tulipokuwa tukishughulikiwa. Eti mnasema mbona wapinzani kina Lisu, Mbowe, zitto wapo kimya vitu bei juu, pambaneni na hali zenu , maana hata na sisi tulipokuwa motoni tukiteswa mlikaa kimya.
 
Jamaa walichukia sababu hio hela ya rushwa ilikuwa ngumu kuipata, yani walilazimika kuishi kwa mishahara tofauti na kwa JK ambako mtu mwenye nafasi alikuwa anafisadi hadi analewa na mipesa. Anaishi maisha yasio yake kwa kutesa wengine ila kwao freshi. Huu ndio ujinga wanahisi ni ubepari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…