Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Hilo swali la kwanza ni la kinafiki sana, kuna miradi mingapi imekua implemented Tanzania Bara na haijawahi kuulizwa mbona Zanzibar haipo.! Msingi wa hilo swali ni personal attacks na si linginelo.
Swali hili msingi wake ni hiyo exeption ya Bandari ya Zanzibar. Huwezi ukasema DP Wedi apewe bandari zote nchini za Bahari na Maziwa kasoro za Zanzibar, halafu utegemee watu waache tu wasijiulize
 
Case closed
Wote mnaoleta hoja mfu kuhusu mkataba wa uwekezaji baina ya Tanzania na Dubai mna uelewa finyu wa mambo.

Msitusumbue na nyuzi zenu hapa
 
Kwa hiyo kuendeleza bandari ni kwa manufaa ya mwekezaji tu? Je, baada ya 'ukomo' wa mkataba, Tanzania isingependa kubaki kunufaika na miundombinu itakayoachwa na mwekezaji? Kwa nini utaje faida anazoangalia mwekezaji tu, na sio pia za nchi inayohost? Kwani Tanzania haitaki kuachiwa bandari ya Zanzibar ikiwa nzuri ya kisasa hata kama ilikuwa haimlipi mwekezaji?
 
Huyu anampiga Dr. Rigemeleza Nshala, mtu ambaye ana Master Degree ya Mikataba ya uwekezaji wa kimataifa katika chuo kikuu namba moja Duniani yaani Havard, na pia ni Nshomile
 
1. Zanzibar hawataki bandari za kisasa kupokea mizigo yao? Mbona wanapanua bandari? Soma link hiyo uone kuwa nao wanahitaji upanuzi na ufanisi. Inaingia akilini kweli kuwa bandari zooooooooooote za Tanganyika zibinfishwe kuwa bora na za kisasa mwekazaji aziacheza zanzibar. Mizigo kwani inaenda na kutoka nchi ulizozitaja?

2. Kwahiyo unasema Assad aneza kuwa expert witness kwa vile hakuna ownership ya knowledge?

3. kama hakuna discrepancies/inconsistencies katika ushahidi huwa hakuna kesi. Hivyo ilibidi ajibu upotofu huo!
Kubadirika huko niko angelikujibu.......kma Prof!


 
Kuhusu bandari za zanzibar Makamo wa pili wa Raisi wa Zanzibar mhe Hemed anasema wamekubaliana masula ya Bandari kila upande usimamie Bandari zake ndio maana zanzibar wana ZPC yaani Zanzibar port coparation na huko bara wana TPA Tanzania port Athority
 
Jukumu la msingi la kumiliki na kuendeleza bandari ni la Tanzania mwenyewe, sio muwekezaji. Huwezi kumlazimisha muwekezaji awekeze wapi maana uwekezaji ni subject na return on investment. Kwa sasa, muwekezaji hakuona manufaa ya kiuwekezaji ya haraka kwa kuwekeza Bandari ya Zanzibar.

Na hilo liko wazi kwq mambo mengi tu. Kwani Zanzibar hawataki kuwa na mabasi mazuri kama ya shabiby, mbona hakuna hata muwekezaji mmoja wa mabasi huko Zanzibar? Kwani Zanzibar haitaki kuwa na viwanda vya mbolea? Mbona hakuna hata kiwanda kimoja cha mbolea huko!

Kwani Zanzibar haitaki kuwa na SGR? Mbona hakuna uwekezaji wa SGR huko? Simply business returns ndizo zinaeleza wapi muwekezaji afanyike tofauti na public projects ambapo Serikali ukipendezwa nayo inaweza kufanya popote.
 
Kama Bandari ni suala la muungano basi inaonyesha wameshaliondoa walipokuwa wanajadili kero za muungano maana Makamo wa pili wa Raisi wa Zanzibar mhe Hemed anasema wamekubaliana masula ya Bandari kila upande usimamie Bandari zake ndio maana zanzibar wana ZPC zanzibar port coparation na huko bara wana TPA Tanzania port Athority
 
Maswali ya kipumbavu na ya kitoto,umeambiwa mara kadhaa Kuna sheria 2 tofauti za Mamlaka ya Bandari Zanzibar na Tanzania Sasa sijui unatakaje Bandari za Zenji ziwepo.

Pili kwani unampangia Mwekezaji choice yake?
 
Pamoja na makubaliano haya ya umiliki, sababu ya msingi kabisa uwekezaji katika Bandari za Zanzibar kwa msingi ya uwekezaji wa DPW haulipi. Simple ni hivyo tu, mengine yote ni chenga tu.
 
Nadhani hujanielewa mkuu. Your opportunities may not be my opportunities. Wewe unaweza kuwa na viwanja viwili mapinga Bagamoyo na postal, na vyote unatafuta muwekezaji aviendeleze. Investors wanaweza kuvutiwa zaidi na kiwanja cha postal kuliko mapinga kutokana na manufaa ya kiuwekezaji atakayoyaona, japo wewe unataka I mapinga pia pendelezwe. Simply hivyo.

Hivi hata wewe kwa akili ya kawaida tu kama mfanyabiashara, utashusha mega ships Zanzibar halafu walaji wako DRC? Seriously? Ili upate nini?
 
Heshima hujengwa kwa muda mrefu lakini kwenye kuiharibu, ni siku moja tu.
Hata hiyo heshima usikute ni nyie wenyewe tu ndio mliyompa ila yeye hakuwa anazingatia kuhusu heshima, mfano sasa hivi wenye kushabikia huo mkataba wa bandari watakuwa wanampa heshima kwa anayoongea.

Mwisho wa siku unakuta kumbe ni shobo zenu tu ila yeye ana bifu zake na kuangalia masilahi yake.
 
asante sana. Huyu hana hoja, hoja zake zinaegemea tunamlaumu nani...
 
kuna kaharufu fulani kwa mbali nakaona kwenye hili...
 
Hivi ni kwa nini mawakili wa CCM na wa CHADEMA wasifanye debate ya wazi kwenye TV na kila mtu awaone wanacho bishaniwa kwenye hili suala la bandari?
 
Issue hapo ni dini ,anayetuhumiwa ni dini yetu lazima tumsitiri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…