Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Jibu la Profesa Assad limeumiza mioyo ya jamaa waliowekeza kwenye upotoshaji mwingi na ubaguzi wa chini kwa chini.

Bandari ya Zanzibar ilishafanyiwa uwekezaji mwaka mmoja kabla ya hii ya huku bara. Bandari ya mpigaduru ilipata mwekezaji na mpaka muda huu atakuwa pengine keshaanza kazi. Pia DP World ni mmiliki wa mali zilizopo DRC na Rwanda hamiliki chochote kule Zanzibar hivyo hana sababu ya kuitaka bandari yao.

Kaongea kama mwanazuoni na katoa maoni ya jumla baada ya mwandishi wa habari kumuuliza maswali, sawa sawa na hao wengine walivyoyatoa maoni. Na hiki alichokisema sio mara ya kwanza kwake kukitamka anapohojiwa na waandishi wa habari, ni kweli kielimu tupo chini sana. Uwezo wa taasisi zetu inakuwa na matokeo duni kwa sababu ya utendaji mzima kuwa duni na hakuna anayejali.

Na pia ni kweli bandari zetu zinapungukiwa katika maeneo hayo aliyoyataja, haihitaji kuwa mbobezi wa sekta fulani kuona kuwa usomi wetu mwingi umejaa ubabaishaji. Na huyu na CAG mstaafu ameongea kwa uzoefu wake wa jumla wa sekta nyingi alizozifanyia ukaguzi.


Prof Assad kuongelea upungufu wa bandari, anayo mamlaka hayo kwani ni mojawapo ya taasisi alizozikagua mara nyingi na pia akawa anatoa muhtasari wa kazi ya ukaguzi iliyofanyika.

Kuyapokea maoni ya kitaalam aliyoyatoa wakati ule akiwa CAG hakuna tofauti yoyote na kuyapokea maoni hayo hayo anayoyatoa leo hii akiwa mstaafu.

Anayo mamlaka ya kimaadili ya kuikosoa jamii yetu kwa uzoefu alionao kama mhasibu mbobezi.
Acha kukwepa hoja! Hajajibu vipengele vya Lisu et al . Tulitaka aoneshe ukomo mkataba, adadavue maana ya exclusive land rights za DP world (kuwa akitaka ardhi ya St Josephs Cathedral pale lazima apewe (asipopewa anakupeleka ISCD) ni nini etc etc.....hajagusa hayo
 
[emoji441]🪗[emoji447]. Ama kweli ,,ooohh[emoji441][emoji441]

Maradhi yote uguwa [emoji441][emoji441]

Lakini kuchacha [emoji441][emoji441]

Usiombeee[emoji441][emoji441][emoji447][emoji447].


NJAA MBAYA Sana [emoji1787][emoji1787]
 
Huu ndo usomaji mbaya wa mkataba huo.
Tunakwenda vema kabisa. Niwekee kifungu cha ardhi , bandari zote kipengele na exclusive rights portion tukijadili hapa tuone kama kuna usomaji mbaya

Exclusive right​

In Anglo-Saxon law, an exclusive right, or exclusivity, is a de facto, non-tangible prerogative existing in law (that is, the power or, in a wider sense, right) to perform an action or acquire a benefit and to permit or deny others the right to perform the same action or to acquire the same benefit. A "prerogative" is in effect an exclusive right. The term is restricted for use for official state or sovereign (i.e., constitutional) powers. Exclusive rights are a form of monopoly.
Exclusive rights can be established by law or by contractual obligation, but the scope of enforceability will depend upon the extent to which others are bound by the instrument establishing the exclusive right; thus in the case of contractual rights, only persons that are parties to a contract will be affected by the exclusivity
 
Acha kukwepa hoja! Hajajibu vipengele vya Lisu et al . Tulitaka aoneshe ukomo mkataba, adadavue maana ya exclusive land rights za DP world (kuwa akitaka ardhi ya St Josephs Cathedral pale lazima apewe (asipopewa anakupeleka ISCD) ni nini etc etc.....hajagusa hayo
Mkataba una vipengele 31 ulitaka aguse kila kipengele kwa muda wa chini ya saa moja wa mahojiano na mwandishi wa kituo cha runinga?.

Ukomo upo kwenye project contracts hauwezi kuwepo kwenye mkataba uliopita bungeni. Mkataba una mawanda [scope] na kila eneo linamkataba tofauti wenye ukomo tofauti.

Kwa taarifa tu hao DP World watakwenda kuongeza uwezo wa vyuo vyetu vya bandari kina DMI. Anakwenda kumiliki asilimia nane tu ya eneo zima la bandari, hawezi kulitaka eneo St Joseph Cathedral kwani sio sehemu ya hiyo asilimia nane ya ardhi ya bandari.
 
Haya siyo maswali ya kujibu Professor Assad. Hata sisi wanafunzi wake tunaweza kukujibu vizuri kabisa.

Jibu kwa swali la Kwanza.
Bandari ya Zanzibar haipo kwasababu muwekezaji hana interest na Bandari hiyo kutokana na Investment Plan yake. Hajaona faida ya kuendeleza Bandari ya Zanzibar huku akijua biashara ipo Rwanda, Zambia, Malawi, DRC, Burundi na mikoa ya mbali. Hiyo mizigo atayoishushia Zanzibar itaenda wapi? Hivi hili nalo linahitaji muende mahakamani nyie wapinga maendeleo.

2. Jibu kwa swali la pili
Japo kuna mgawo wa kitaaluma lakini hakuna ownership of knowledge. Yeyote anaweza kuelewa chochote.

3. Jibu kwa swali la tatu
Hakuna hoja ya maana ndio maana professor Asad hakuna haja ya kujibu upotofu. By the way, hoja zenyewe zimekuwa zikibadilika siku hata siku na kutokana na mtu na mtu. Wako wanaosema mkataba, wako wanaosema mgeni asipewe nafasi ya kufanya uwekezaji katika Bandari, wako wanaosema watanzania tuna uwezo, mitaji na teknolojia. Yaani vurugu mechi.
Professor Asad amekuwa smart kwa kugusia upotoshaji unaofanywa kwenye maeneo machache hususan umiliki na matumizi ya ardhi.
Umewajibu vizuri sana. Tatizo wengi wanaojadili wako upande wa wanaopinga kila kitu. Hivi huyo anayepinga anaweza kumlinganisha Prof. na Madeleka? Mnamjua vizuri? Ulinganisho wao ni sawa na Tembo - Prof na sisimizi au mdudu mdogo zaidi ya sisimizi-Madeleka!!
 
Huu ndo usomaji mbaya wa mkataba huo.
What is an example of an exclusive right?
In relation to property, an exclusive right will, for the most part, arise when something tangible is acquired; as a result, others are prevented from exercising control of that thing. For example, a person may prohibit others from entering and using their land, or from taking their personal possessions.
 
Mkataba una vipengele 31 ulitaka aguse kila kipengele kwa muda wa chini ya saa moja wa mahojiano na mwandishi wa kituo cha runinga?.
ndiyo maana nimesema ametoa blanket answers, petty ones without going to the core of the mkataba and read between lines
 
Tunakwenda vema kabisa. Niwekee kifungu cha ardhi , bandari zote kipengele na exclusive rights portion tukijadili hapa tuone kama kuna usomaji mbaya

Exclusive right​

In Anglo-Saxon law, an exclusive right, or exclusivity, is a de facto, non-tangible prerogative existing in law (that is, the power or, in a wider sense, right) to perform an action or acquire a benefit and to permit or deny others the right to perform the same action or to acquire the same benefit. A "prerogative" is in effect an exclusive right. The term is restricted for use for official state or sovereign (i.e., constitutional) powers. Exclusive rights are a form of monopoly.
Exclusive rights can be established by law or by contractual obligation, but the scope of enforceability will depend upon the extent to which others are bound by the instrument establishing the exclusive right; thus in the case of contractual rights, only persons that are parties to a contract will be affected by the exclusivity
Linaweza kuwepo hilo neno katika sentensi ya maneno kama WILL au MAY, maana nzima ya sentensi husika ikawa imebadilika.
 
ndiyo maana nimesema ametoa blanket answers, petty ones without going to the core of the mkataba and read between lines
Alichokisema kwa ufupi ndio ufafanuzi unaopotoshwa humu jukwaani. Kwamba tunapoteza muda kwenye negativities badala ya kujikita katika kujadili maana nzima ya mkataba ambayo ni chanya kwenye uchumi wetu.
 
Ukomo upo kwenye project contracts hauwezi kuwepo kwenye mkataba uliopita bungeni. Mkataba una mawanda [scope] na kila eneo linamkataba tofauti wenye ukomo tofauti.
Hapana ukomko unatokana na IGA kuwa shghuli zitakapoisha. sasa swali ni shughuli gani? Shughuli ni kuendesha bandari zote. sasa shughuli za bandari zinaisha lini?
Usidanganywe na say kujenga Gati mbili au kumi, yes hiyo itaisha, lakini shghuli za bandari zinaisha?
To crown it all, Kupakia na kushusha mizigo kunaisha?
 
Uislam zaidi ya taaluma
Hili ndilo jibu halisi. Watu wamezama kwenye dini kiasi ambacho wanapata upofu wa kuona kosa linalofanywa na muislam mwenzao. BTW ni kile awamu ambayo muislam anakuwa rais, mara zote huwa wakipata changamoto ya kukosolewa hukimbilia kwenye kivuli cha dini na kuita wana-dini wenzao kuwatetea. Hili suala la bandari limeshakuwa ni kama waislam vs wakristo, kisa tu wahusika ni waarabu, na rais yuko happy lionekane hivyo. Wengi wanaounga mkono ni waislam. Yaani wao wanadhani kwa vile ni waarabu basi inatosha na hakuna sababu ya kuangalia mkataba.
 
Jukumu la msingi la kumiliki na kuendeleza bandari ni la Tanzania mwenyewe, sio muwekezaji. Huwezi kumlazimisha muwekezaji awekeze wapi maana uwekezaji ni subject na return on investment. Kwa sasa, muwekezaji hakuona manufaa ya kiuwekezaji ya haraka kwa kuwekeza Bandari ya Zanzibar.
Mwekezaji hakuona umuhimu wa Zanzibar, kwamba na wenye nchi yao nao hawakuona umuhimu wa kumlazimisha mwekezaji ili wanufaike!?
 
Mwekezaji hakuona umuhimu wa Zanzibar, kwamba na wenye nchi yao nao hawakuona umuhimu wa kumlazimisha mwekezaji ili wanufaike!?
Ingekuwa uwekezaji unalazimishwa sidhani kama tungekuwa na watoto wanaomaliza vyuo kubaki bila ajira mitaani. Hivi huko vyuoni mlienda kusomea ujinga? By FaizaFoxy
 
Hapana ukomko unatokana na IGA kuwa shghuli zitakapoisha. sasa swali ni shughuli gani? Shughuli ni kuendesha bandari zote. sasa shughuli za bandari zinaisha lini?
Usidanganywe na say kujenga Gati mbili au kumi, yes hiyo itaisha, lakini shghuli za bandari zinaisha?
To crown it all, Kupakia na kushusha mizigo kunaisha?
IGA haina nguvu zaidi ya kutambulisha biashara pale bungeni, yenye nguvu ni hii mikataba ya kibiashara HGA.

Elewa maana pana ya bandari kisasa sio kwa zile maana za karne iliyopita, bandari kuimiliki kwa sasa kunamaanisha masuala yote ya kilogistiki kuanzia kule mzigo unapopakiwa mpaka unapomfikia mteja kwenye nchi yake.

DP World anao uwezo wa kuifanya shughuli hiyo kwa maana ya kuwa na miundo mbinu ya kisasa, uelewa wa kutosha wa biashara yenyewe na mengine mengi.
 
Linaweza kuwepo hilo neno katika sentensi ya maneno kama WILL au MAY, maana nzima ya sentensi husika ikawa imebadilika.
This is not an expert /legal definition of exclusive rights. WILL and MAY , SHALL can not change the base root meaning of the word...nenda kwenye interpretation of laws act.....
Huwezi kuwa na mkataba unasema Steven may have exclusive rights kama mnaingia say mkataba wa kukodisha shmba . Huwezi kukubali clause kama hiyo!
sasa hawa wa kwetu walikubali uchafu kama huo
 
wenye nchi yao nao hawakuona umuhimu wa kumlazimisha mwekezaji ili wanufaike!?
Wenye nchi zanzibae, bali hakuna wenye nchi Tanganyika? You are crazy (sorry rafiki, sina maana ya tusi)
 
This is not an expert /legal definition of exclusive rights. WILL and MAY , SHALL can not change the base root meaning of the word...nenda kwenye interpretation of laws act.....
Huwezi kuwa na mkataba unasema Steven may have exclusive rights kama mnaingia say mkataba wa kukodisha shmba . Huwezi kukubali clause kama hiyo!
sasa hawa wa kwetu walikubali uchafu kama huo
Huwezi kuita uchafu kwa kuchambua kipengele kimoja tu cha mkataba. Uchambue wote kipengele baada ya kipengele ndio utakuwa na haki ya kuuita uchafu.

Hii ni fani ya watu wanaoisomea miaka na miaka vyuoni, huwezi kuita uchafu eti kwa sababu hauyapendezi matakwa yako.
 
Ingekuwa uwekezaji unalazimishwa sidhani kama tungekuwa na watoto wanaomaliza vyuo kubaki bila ajira mitaani. Hivi huko vyuoni mlienda kusomea ujinga? By FaizaFoxy
Acha kutembelea nyota ya member mwenzako, jitegemee. Yaani mwekezaji asilazimishwe kwa jambo la maslahi la taifa? Kwa hiyo asilazimishwe kuajiri baadhi ya wafanyakazi wazawa kwa kazi wanazoziweza, hata akiamua kuja na vibarua waarabu iwe sawa tu?
 
Back
Top Bottom