Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Maswali kwa Profesa Musa Assad kuhusu mkataba wa Bandari

Upo sahihi mkuu lakini kwa mfumo wa Tanzania wizi hautaisha, niambie mara ya mwisho tangazo la ajira za bandari, TANAPA, BOT, Ikulu, mambo ya nje n.k uliona lini? je watu hawaajiriwi hizo sehemu? jibu ni kwamba sehemu nono zote wamewekwa watoto wa kubwa na ndugu, pia wanafundishwa wizi tangu siku ya kwanza, wezi wa kubwa Tanzania ni wale wanafunga tai na kulindwa na vyombo vya dola 24hrs badala ya kukamatwa. Hakuna namna acha yaibe mpk sisi wananchi tupate akili tuyakatae haya majangili
Bado ninatofautiana nawe kabisa mkuu 'Benjamin'.
Mimi ninaamini kabisa kwa dhati ya moyo wangu, kwamba haya matakataka tunayoyaona na kuyafanya kuwa ndiyo kawaida ya maisha yetu, inawezekana kabisa kuyapunguza sana (hata kama si kuyamaliza kabisa).

Ni swala la kupata viongozi sahihi tu wenye dhamira ya dhati kufanya hivyo.

Michina ni mijitu mizi sana ile. Nchi ile inao watu bilioni na zaidi..., huko kwao hawafanyi mambo kama unayoyaeleza hapo juu. Hawa watu wanapokuja hapa, wanatabia za kutaka kukwapuakwapua kila kitu, kama meno ya tembo, n.k..
Hata inafikia kwenye baadhi ya nchi, wachina wenyewe wamejiwekea polisi wao na jela zao, ili kuwadhibiti mijizi yao.

Hizo nchi za huko Mashariki ya mbali, tunakoambiwa uchumi wao unaenda vizuri, na kupata maendeleo ya haraka.
Usidhani hata mara moja kwamba hawana mijizi huko, hata kwenye serikali zao, lakini wamejiwekea taratibu za kuwabana hawa washenzi.
Hapa kwetu, CCM yenyewe ndiyo inayorutubisha yote hayo uliyoyaeleza kwenye andiko lako hapo juu.
Kwa hiyo, waTanzania wanajua kabisa wapi pa kuanzia, kuondoa uozo huo uliouelezea vizuri sana wewe hapo juu.

Bila kuwashughulikia CCM, usitegemee mabadiliko yoyote.
 
CCM hawashindwi ,kama walimvuta Karamagi na kuanza kuiponda TICTS yake vipi kwa Prof Assad?
 
Assad yupo sahihi 100%. Hivi jf nani kawaambia Shivji ni mwanasheria? Mnaota kweli
 
Mkuu
Hili la DPW limekwisha chacha hata liungwe namna gani halitakuwa na ladha ya kuvutia. Mhe. Rais amekwishashauriwa na Wasomi, Wazee wenye busara kama mzee Butiku na Mzee Kinana na Katibu Mkuu wa CCM wameshauri kuwa kama kuna kasoro zirekebishwe ili tusonge mbele. Sauti ya wengi ni sauti inayotoka kwa Mungu. Hata hukumu ikitoka kuwa Serikali imeshinda, hili suala bado mbichi sana.
Mkuu hii Ni sauti ya koryo Rorya ama?
 
Kw
Sasa Do world ikawekeze Bandari iliyo kisiwani? Nchi gani inategemea kusafirisha mizigo yake kupitia ZANZIBAR?
Kwani zanzibar hakuna mizigo? ya kutoka nje kwenda outside world
 
Hilo swali la kwanza ni la kinafiki sana, kuna miradi mingapi imekua implemented Tanzania Bara na haijawahi kuulizwa mbona Zanzibar haipo.!

Msingi wa hilo swali ni personal attacks na si linginelo.
Hakuna mradi wa Muungano ambao utafanyika Bara bila kuhusisha Zanzibar. Una mfano tu udahili na mikopo kwa wanafunzi vyuo vikuu kwa Bara lazima wazanzibar wapo; mikopo wazanzibar watapata huku na ananafasi pia ya kupata kule kwao
Viwanja vya ndege kimataifa vile vile. Labda toa mifano ya miradi hiyo ya Muungano ambayo ilifanyika huku Bara tu
 
Baadhi ya majibu ya maswali yako haya hapa:

Profesa Issa Shivji anasema Mkataba huu ni treaty yaani mkataba baina ya nchi na nchi na nchi hiyo ni Tanzania na nchi nyingine ambayo ni ngumu kusema kama ni nchi au la.

Ila kuna jambo ambalo limejitokeza katika hilo maana katika treaty lazima kuwepo nipe na nikupe baina ya wawili katika mkataba. Hilo halipo bali haki zote amepewa Dubai huku wajibu wote amepewa Tanzania bila haki. Yaani mkataba umekuwa uwekezaji ingawa unaitwa ni mashirikiano. Ila ushirikiano huo si wa kijumla bali ni wa bandari na mwekezaji ametajwa ni DP World siyo wawekezaji wa kijumla wa kuhesabika kwa namba makampuni au wafanyabiashara kutoka Dubai.
View attachment 2712719
asante kwa ufafanuzi
 
Nimemsikia huyu mwanasheria wa Ujerumani. Anasema huu Mkataba tunaoujadili sasa ni wa Host Government Agreement (HGA). Wenzangu mmeuona huo mkataba nimetafuta sijauona. Umeingiwa lini halikuwa mazungumzo ya HGA yalikuwa yakisubiri kuridhiwa kwa IGA?
search humu utaopata, upo sana JF
 
Yani haya ndio maswali kweli unamuuliza professor? Kweli nchi hiibimejaa wajinga wengi mkiambiwa mna uelewa mdogo mkubali tu.
 
Haya siyo maswali ya kujibu Professor Assad. Hata sisi wanafunzi wake tunaweza kukujibu vizuri kabisa.

Jibu kwa swali la Kwanza.
Bandari ya Zanzibar haipo kwasababu muwekezaji hana interest na Bandari hiyo kutokana na Investment Plan yake. Hajaona faida ya kuendeleza Bandari ya Zanzibar huku akijua biashara ipo Rwanda, Zambia, Malawi, DRC, Burundi na mikoa ya mbali. Hiyo mizigo atayoishushia Zanzibar itaenda wapi? Hivi hili nalo linahitaji muende mahakamani nyie wapinga maendeleo.

2. Jibu kwa swali la pili
Japo kuna mgawo wa kitaaluma lakini hakuna ownership of knowledge. Yeyote anaweza kuelewa chochote.

3. Jibu kwa swali la tatu
Hakuna hoja ya maana ndio maana professor Asad hakuna haja ya kujibu upotofu. By the way, hoja zenyewe zimekuwa zikibadilika siku hata siku na kutokana na mtu na mtu. Wako wanaosema mkataba, wako wanaosema mgeni asipewe nafasi ya kufanya uwekezaji katika Bandari, wako wanaosema watanzania tuna uwezo, mitaji na teknolojia. Yaani vurugu mechi.
Professor Asad amekuwa smart kwa kugusia upotoshaji unaofanywa kwenye maeneo machache hususan umiliki na matumizi ya ardhi.
Nimeshangaa sana jamaa kakaa chini haya ndio maswali kweli anamuuliza professor?
 
Swali hili msingi wake ni hiyo exeption ya Bandari ya Zanzibar. Huwezi ukasema DP Wedi apewe bandari zote nchini za Bahari na Maziwa kasoro za Zanzibar, halafu utegemee watu waache tu wasijiulize
Sasa bandari ni suala la muungano? Hivi nyie watu mnajua mnachokitetea au mnajiropokea tu?
 
Wamekubaliana wapi na lini na kwa utaratibu upi. Katiba iko wazi kwenye namna ya kuondoa mambo ya muungano. Ni jambo linalofanyika bungeni kwa kura theluthi mbili kutoka Zanzibar na Tanganyika kukubali. Sasa hilo limefanyika lini kuliondoa jambo la bandari katika mambo ya muungano?
asante kwa ufafanuzi
 
Nimesoma andiko lako kuwa watu HAWANA UELEWA ndiyo maana wanakataa mkataba wa DP World. Nomba kwa manufaa ya wengi ujibu hoja hizi mbili tu. Kumbuka wewe ni "national Figure" in academics, tamko lako linaamsha maswali)

1. Kama mkataba una manufaa , kwanini bandari za Zanzibar hazipo? (kizuri kweli uache kula na ndugu zako Zanzibar, uwape jirani?)

2. Wewe si mwanasheria (unaweza ukawa na uelewa kidogo wa sheria za uhasibu and the like). sasa authority ya kusema akina Shivji, Lugemeleza, Lisu, Mwabukusi, Madeleka na wengine hawana uelewa katika International treaties unaitoa wapi?

3. Mbona hujajibu hoja kwa hoja ambazo hao niliowataja hapo juu wanazilalamikia? Umetoa blanket answers kama za Joseph Kasheku Msukuma, Kitenge, Wasira na watu kama hao. Kama msomi you need to be specific when answering questions...kama ilivyokuwa ukiwataka wanafunzi wako wajibu



Yani ulivyohusisha bandari ya Zanzibar tu nikajua ww ndio walewale Kila cku mnaambiwa Bandari haipo ktk masuala ya Muungano
 
Back
Top Bottom