Maswali na Majibu kuhusu Kitabu cha Mohamed Said

Maswali na Majibu kuhusu Kitabu cha Mohamed Said

Cool running unaongea na mtu mzima tena mwenye busara sana kuliko unavyomfikiria. Ni vyema kama unaitaji elimu maneno yenye muelekeo ya kupotosha au kejeli yakaepukwa ili kuendeleza mjadala huu. Mimi nipo kitambo katika mjadala huu nafuatilia kwa makini na sipendi ufungwe bali nataka niendelee kupata ujuzi wa historia ya nchi yangu.

CHAMVIGA,

Tatizo liliopo si kwamba yakua,Bwana Mohamed Said ati "anakimbia" masuali/hayawezi kuyajibu au mie nataka asiulizwe/asijibu,hasha abadan!

Itakua tunakwenda kinyume kabisa na dasturi za taaluma,ati sisi kuzuia mwangine asijibu masuali ya kitaaluma!? Duuh!

Hivi kimantiki weye hujiulizi...yakua huyo "Bwana Mdadisi" mwenyewe ameshatujuza hapa yakuwa,yeye na Bwana Mohamed Said ati "wanafahamiana" kiundani,na pia wanawasiliana kwa e'mails!?

Sasa tujiulize ni kipi kilichowafanza Wanataaluma hawa waili wenye kufahamiana na kuwasiliana,ati washindwe kupanga au kufikia muafaka baina yao,wa jinsi gani ya kujibizana/kuhakiki shughuli zao za kitaaluma!?

Kwanini huyo Udadisi hakuona haja ya kumfahamisha Bwana Mohamed Said ati hiyo dhamira yake "njema" alonayo ya kuhakiki hicho kitabu...na pia kumuomba/kumtaarifu yakua baada ya hapo majawaba yako yoote nitayachapisha rasmi au nitayaweka mitandaoni-JF,ili Wasomaji wangine nao wakusome na kupambanua/kujiamulia ukweli au "upotoshaji" wako!?

Sisi soote tunafahamu history ya machafuko ya lugha,khasa matusi,kebehi,tashtit na chuki zilizomo humu-JF takriban penye thread/s zoote zinazomukhusu Bwana Mohamed Said...na hata Udadisi pia amekiri kufahamu hili!

Sasa,ndipo sisi wangine tunapojiuliza yakua...hiyo dhamira njema ya huyo "Bwana Mdadisi",haikuwezekana popote pale au kwa njia nyangine,shuruti amletee mwenzie msuto/cross examination humu-JF,ilihali anafahamu madhila na tafrani zitakazotokea kwalo!?

Mie binafsi najitolea kuchapisha kwa gharama zozote zile na kuzigawa copies zoote bure,kijarida cha majawaba cha hayo masuali ya Udadisi kutoka kwa Bwana Mohamed Said...ikiwa tu yatapelekwa kwa tartib za muafaka na staha za kitaaluma!

Pana wakti huyo huyo Udadisi,naliona baadhi ya post/s humu akilalama kiduchu yakua hajapatapo access ya makabrasha ya Sykes Family!? Sasa hajiulizi kwanini ilihali yeye ni mwanataaluma/mtafiti "alobobea"!?

Nimeona kwenye mojawapo ya bayana zenye hayo aitayo ati ndo masuali yake ya "kitaaluma" huyo Udadisi...anauliza je Bwana Kondo Kipatwa ndo kweli aliweza kuwa Mwafrika wa awali kuwa na Radio hapo Tanganyika kabla ya Paul Bomani au George Kahama!?

Sasa kama yeye anayo majawaba tafauti au ana watu wangine kumbe akiwafahamu wa huko mabara,ambao walokua ndo wenye hizo radio za awali kwanini asituwekee hapa jamvini!?

Naona pia Udadisi ameweka hiyo link ya Sheikh Mtoro Bin MwinyiBakari,labda kuzidi kumchachafya Sheikh Mohamed Said!?...sasa anawafahamu family/vizazi vya huyo Bwana,ambao waliopo mpaka kesho hapo nchini ni akina nani...na vyeo/shughuli zao Serikalini!?

Huyo hakuna direct historical evidence yakua ati Sheikh Mtoro Bin MwinyiBakari alikua na Radio hapo Dunda wala Bwagamoyo mjini wakti ule!

Huyo Ngongo,ni mstaarabu kiduchu...lakini kinachomharibia kwa Sheikh Mohamed Said ni hizo lugha zake za "ki-Arusha"/za kihuni! Na pia ninakhis labda ana allergy na "Wazee wa Gerezani"/Kariakoo!?...mtafanzaje jamaa zetu,na ukweli ndo huo yakua wao walitangulia kufika...na pia ndo Wanamji!? Daah! Teeh! Teeh! Teeh!

Pana mangi ya kunena...lakini nakwacha maana vijisughuli vimenikinza hapa kibaruani!

Ahsanta.
 
Ndugu gombesugu nilidhani tumeshalimaliza hili suala. Kwa kweli dhamira/nia yangu ni safi kabisa. Hakika mimi ni muumini wa kisomo/elimu ya wazi. Huu mjadala ningeufanya peke yangu na Mzee Mohamed Said kwa njia ya barua pepe tungekosa michango ya watu wengine. Huu ni mjadala wa wazi wa kuiboresha historiografia yetu.

Hapa nilitegemea wajuvi wa historia kama wewe muwe mnachangia kwenye hizo nukuu za kitabu chake, ama kuzishibisha kwa rejea zingine, majina ya wahusika wengine, wasifu au visa mkasa zaidi. Na mkifanya hivyo inatusaidia hata watafiti wanagenzi kama mimi kuzifuatilia na kutimiza azma ya Mzee wetu Said ya kuiweka wazi historia iliyoweka pembezoni.

Tusiogope. Tuvumiliane. Tujadiliane.
 
Ndugu gombesugu nilidhani tumeshalimaliza hili suala. Kwa kweli dhamira/nia yangu ni safi kabisa. Hakika mimi ni muumini wa kisomo/elimu ya wazi. Huu mjadala ningeufanya peke yangu na Mzee Mohamed Said kwa njia ya barua pepe tungekosa michango ya watu wengine. Huu ni mjadala wa wazi wa kuiboresha historiografia yetu.

Hapa nilitegemea wajuvi wa historia kama wewe muwe mnachangia kwenye hizo nukuu za kitabu chake, ama kuzishibisha kwa rejea zingine, majina ya wahusika wengine, wasifu au visa mkasa zaidi. Na mkifanya hivyo inatusaidia hata watafiti wanagenzi kama mimi kuzifuatilia na kutimiza azma ya Mzee wetu Said ya kuiweka wazi historia iliyoweka pembezoni.

Tusiogope. Tuvumiliane. Tujadiliane.


Bwana Udadisi,

Nimekusoma na niwia radhi japo kiduchu,kama unakhis nimetumia lugha yenye khitilaf!?

Ni kweli usemayo,yakua ni wajibu wetu soote kujaribu kurekebisha historia ya nchi yetu...ilotaka kuwekwa kando/kufichwa na wachache wenye dhamira/nia potofu kwa Taifa hili.

Tajitahidi nipatapo fursa kiduchu,kupitia hapa jamvini na kujaribu kusherehesha japo kiduchu.

Lakini,mie wala si mtaalamu wala mbobefu kwayo,zaidi yenu wenzangu!...nakhis itakua umenitendea haki mno nduguyo,ikiwa utaniruhusu niendelee kuwa mtazamaji/msomaji wenu mtiifu.

Shukran na tupamoja!

Ahsanta.
 
13. "Dr Mutahangarwa was the first African to qualify as a medical doctor" (p. 104)

14. "This [emotional farewell speeh which Nyerere delivered on 5th November, 1985, to Dar es Salaam Elders, an exclusive group of Muslim townsmen who had supported him since the founding of TANU] was one of the very rare occassions at which Nyerere talked publicly about his beginnings and it was the first time he had mentioned Abdulwahid's name in public associating him with his own history and that of the party" (p. 110)

"In his farewell speech Nyerere paid tribute to Muslim elders who supported him during the struggle in spite of his religion, but he played down the role of Abdulwahid and TAA as a political organisation" (p. 110-111)

15. "Nyerere did not have any political experience worth mentioning at that time [1952]" (p. 111)

16. "As a Christian, Nyerere knew that he could never hope to build a political base in Dar es Salaam environment of the 1950s where politis assumed strong Muslim characteristics" (p. 112-113)

17. "Abdulwahid confided with the TAA executive that having the most educated African in the land would strengthen its leadership and portray a good image before the eyes of the colonial government and the United Nations Visiting Mission" (p. 113)

18. "The election was by a show of hands. [Denis] Phombeah who was in charge of the Arnatouglu Hall was the returning officer. Phombeah asked both Abdulwahid and Nyerere to go out of the hall for the voting to begin. The whole week before voting Phombeah was making rounds campaigning for Nyerere. But there was no need of doing that; the TAA inner circle of Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz and Rupia had already decided to make Nyerere president of the Association and the election was a mere formality...Abdulwahid 'lost' the election - the first loss in his whole political career - and Nyerere won by a very small margin" (p. 113-114)
 
Yote ya nini haya?

Mzee wangu hawa wala wasikuumize kichwa....kama wanaona ulichoandika kwenye kitabu chako sio sahihi, watoe vitabu vyao waweke historia yao wanaohisi ni sahihi...

Mimi ninacho kitabu chako na naheshimu mtu yeyeto anayetoa kitabu.....hao nao watoe vyao tusome tuone
 
Mzee wangu hawa wala wasikuumize kichwa....kama wanaona ulichoandika kwenye kitabu chako sio sahihi, watoe vitabu vyao waweke historia yao wanaohisi ni sahihi...

Mimi ninacho kitabu chako na naheshimu mtu yeyeto anayetoa kitabu.....hao nao watoe vyao tusome tuone

Mnyepe,
Ahsante sana nakushukuru sana.

Umenisaidia pakubwa kwa kuwaambia hawa ndugu zetu kuwa ikiwa wanaona
mimi nimeandika uongo wao waandike ukweli.

Mimi nimewapa ushauri huu mara kadhaa tena kwa hakika ya nafsi yangu.
Hadi leo wamebaki hapa JF kunibughudhi nyuma ya pazia jembamba ati niwape
ufafanuzi.

Kimambo na Temu wameandika historia ya Tanzania.
Hamna kitu na wala hakuna aliyewauliza.

Ukweli ni kuwa hasad inawala nyoyo zao.

Vile walivyodhani kuwa Nyerere ndiye kila kitu wamekuta ni vingine kabisa
na walivyokuwa wanaaminishwa.

Hiki ndicho kinachowachoma.
Mimi nimeamua kukaa kimya kwani ilm ya ubishani haina baraka.

Hivi ndivyo nilivyofunzwa na maalim wangu Sheikh Haruna Allah amlipe.

Akisema soma na somesha kuwapa watu faida kwani ilm ni amana na amana
ni kitu kilichowekezwa mwenyewe akija sharti umrejeshee amana yake.

Mimi hapa JF niko tayari kueleza yote ninayojua kuhusu historia ya uhuru kama
walivyonifunza wazee wangu na kadri nilivyopata katika utafiti wangu.

Lakini ninapoona mtu kaja na lingine huwa najiweka pembeni.
 
Kimambo na Temu wameandika historia ya Tanzania.
Hamna kitu na wala hakuna aliyewauliza.

Temu na Kimambo hawajaandika historia ya Tanzania, wamehariri kitabu chenye sura zilizoandikwa na waandishi wengi

Kitabu ambacho tunaweza kusema ni cha historia ya Tanzania ni cha John Iliffe, yeye hayupo JF hivyo hatuwezi kumuuliza

Hapa hatujaja kubishana, tumekuja kujadiliana ili kuboresha uandishi na utafiti wa historia ya Tanzania/Tanganyika/Zanzibar
 
Mzee wangu hawa wala wasikuumize kichwa....kama wanaona ulichoandika kwenye kitabu chako sio sahihi, watoe vitabu vyao waweke historia yao wanaohisi ni sahihi...

Mimi ninacho kitabu chako na naheshimu mtu yeyeto anayetoa kitabu.....hao nao watoe vyao tusome tuone

Hakuna mtu katika mjadala huu aliyesema kitabu cha Mohamed Said sio sahihi, tafadhali rejea tena mtiririko wa mada
 

Kwa jinsi ulivyo mdadisi wa ukweli, naomba ufanye hivyo...nasema hivi sababu naona unaweza, pili waandishi wa Tanzania huoni vitabu vyao kwenye maktaba za nchi jirani kama zambia, Zimbabwe, Malawi na Botswana...

Waandishi wengi wamejikita kwenye riwaya za kipuuzi....
 
Temu na Kimambo hawajaandika historia ya Tanzania, wamehariri kitabu chenye sura zilizoandikwa na waandishi wengi

Kitabu ambacho tunaweza kusema ni cha historia ya Tanzania ni cha John Iliffe, yeye hayupo JF hivyo hatuwezi kumuuliza

Hapa hatujaja kubishana, tumekuja kujadiliana ili kuboresha uandishi na utafiti wa historia ya Tanzania/Tanganyika/Zanzibar

Mdadisi,
Kama kweli una nia ya kuboresha nakushauri kaboreshe kitabu cha Historia ya
TANU kilichoandikwa na Chuo Cha Kivukoni.

Ninapomweleza mtu kuwa TANU Tanganyika ilizungumzwa kati ya Abdu Sykes
na Chifu Kidaha Makwaia mwaka wa 1950 kwenye chakula cha jioni nyumbani
kwa Abdu, wewe unataka kuboresha kitu gani?

Au ndiyo hiyo TANU kajanayo Nyerere?
Unataka unifunze mimi historia ya wazee wangu?

Mimi ni muhali sana kujua historia ya wazee wako vipi wewe uijue ya watu
wangu kiasi cha kutaka uisahihishe?

Niwie radhi na kubali uamuzi wangu sina haja ya kujadili hili na wewe.
Ukipenda andika pitio la kitabu changu na sema lolote upendalo.

John Iliffe kafanya hivyo, James Brenan kafanya hivyo, Jonathan Glassman
kafanya hivyo.
 
Kwa jinsi ulivyo mdadisi wa ukweli, naomba ufanye hivyo...nasema hivi sababu naona unaweza, pili waandishi wa Tanzania huoni vitabu vyao kwenye maktaba za nchi jirani kama zambia, Zimbabwe, Malawi na Botswana...

Waandishi wengi wamejikita kwenye riwaya za kipuuzi....

Shukrani mkuu, na huu mjadala ni wa kunisaidia kufanya hivyo; majibu ya Mzee Mohamed Said yatanisaidia sana ili nimnukuu vizuri kwenye tasnifu ninayoiandika na ambayo nategemea kuichapisha kama kitabu
 
Last edited by a moderator:
Mdadisi,
Kama kweli una nia ya kuboresha nakushauri kaboreshe kitabu cha Historia ya
TANU kilichoandikwa na Chuo Cha Kivukoni.

Ninapomweleza mtu kuwa TANU Tanganyika ilizungumzwa kati ya Abdu Sykes
na Chifu Kidaha Makwaia mwaka wa 1950 kwenye chakula cha jioni nyumbani
kwa Abdu, wewe unataka kuboresha kitu gani?

Au ndiyo hiyo TANU kajanayo Nyerere?
Unataka unifunze mimi historia ya wazee wangu?

Mimi ni muhali sana kujua historia ya wazee wako vipi wewe uijue ya watu
wangu kiasi cha kutaka uisahihishe?

Niwie radhi na kubali uamuzi wangu sina haja ya kujadili hili na wewe.
Ukipenda andika pitio la kitabu changu na sema lolote upendalo.

John Iliffe kafanya hivyo, James Brenan kafanya hivyo, Jonathan Glassman
kafanya hivyo.

Mzee wangu tuko pamoja, mimi ni mwanagenzi tu, ninaposema kuboresha historia simaanishi kitabu chako - namaanisha azma/nia ya kitabu chako kama ambavyo umeilezea kwa ufasaha kabisa katika utangulizi/kifungua pazia i.e. kuweka sawa mambo ambayo ama yalifichwa makusudi kabisa au yalisahauliwa bila kujua.

Hao waandishi wote uliowataja hapo wameandika vipengele tu vya historia ya Tanzania, ndio maana, kwa mfano James Brennan sasa anaandika historia ya Kambona ambayo nayo kwa kiasi kikubwa ni historia iliyowekwa pembezoni. Bado hatujapata mtu ambaye amejaribu kuandika historia yote ya Tanganyika kama John Iliffe, kwa kweli ametuachia changamoto kubwa sana.

Kama ujuavyo, Isaria Kimambo yeye kaandika zaidi kuhusu historia ya Wapare na kuna mijadala mingi tu inayohoji baadhi ya maandishi yake hasa kuhusu Upare ya Kusini ambayo inaonekana aliiandika kwa mtazamo wa Upare ya Kaskazini.

Mimi nitaendelea kusoma kitabu chako kwa tuo huku nikiweka nukuu zinazoniletea utata humo, sasa nimeshsvuka ukurasa wa 100; ukiona vyema kuchangia vizuri, ukiacha basi labda wapo wengine watanisaidia. Ila kaa ukijua mimi sina nia wala uwezo wa kukufundisha historia ya wazee wako wa Dar es Salaam/Tanganyika, kama wewe ni mlima mimi ni kichuguu tu, na kama wewe ni bahari mimi ni kijito tu.
 
Mdadisi,
Kitabu hicho kimechapwa 1998.

Unakuja na maswali 2014.
Kukisoma huo ni uamuzi wako.

Nachokuomba tufanyiane staha.
Heshimu msimamo wangu.
 
Back
Top Bottom