Maumivu ya kufukuzwa kazi hayaelezeki

Pole sana kula Panadol
 
Ungeeleza KAZI ulikuwa unafanya kitengo Gani?

Je haki zako zimezingatiwa?

Je taratibu za kukufuta KAZI zilifuatwa?


Je kosa lipo ukilifanya?

Hayo ni MUHIMU kuyajibu ili watu wajue wanaanzia wapi kukupa USHAURI.
 
Aiseee sijui niongee nini hapa ila ni mwaka sasa umepita tangu nmekutana na hilo tatzo, tulikua kikundi cha watu watano wote tukaondolewa kwenye ofisi nzuri tu yani kwa pamoja.
Ubaya ni kwamba mimi ni mwenzngu mmoja tulifanya kazi hyo kwa miezi 11 tu kwahyo tunafukuzwa tukiwa hatujakaa vzuri kiuchumi. Mateso tuliyopitia me na yule jamaa hayasimuliki aiseee ilitubidi tufanye kazi yyte inayopita mbele yetu hasahasa za ujenzi(Saidia fundi) ilhali tumetoka kwenye ofisi ilyokua inatulipa 800k+ kwa mwezi daahh, Nashukuru kwa sasa nipo stable lilikua ni jambo la kupita tu lile kwa mda mfupi.
 
Mfyuuu muone chogo lile...

Nakujengea ndani ndani ili ukae kwa kutulia sio unaleta leta videmu vyako... unanijua nilivyo mkali.
Mi kuleta videmu uwongo ila na mi nataka uhuru wangu humo ndani mi binadamu sio roboto...

Kuna mda nachoka nahitaji kupumzika sasa πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Yalinikuta miezi 3 ilio pita.

Japo mm sikufukuzwa, ila kampuni ilitangaza hasara, huku ikitoa notice ya kupunguza nusu ya wafanyakazi Γ· watakao baki watapunguziwa mshahara kwa nusu.

Halii hii ilinitesa kwa siku 2 za kwanza baada ya hapo, nikapiga moyo konde nika updates CV nikaangalia kampuni zangu 3 nikatuma. Baada ya wiki tu nikawa nishaitwa interview, na baada ya wiki nikawa nishapata kazi sehemu nyingine.

Ila kiu kweli, kwa sasa nafanya kila njia nijiandae na hyo hali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…