Mavazi ya Mchungaji Tony Kapola yachunguzwe

Nadhani wanaendana na ulokole mpya maana ukiangalia kwa America

Pastors vijana huwa wanavaa kawaida sana, na hata baadhi ya singers wana tatoo.

Kwa hiyo wanaiga tu au la ndio tuite standards za ulokole mpya.
wengi wenye tattoo ni za enzi za ujanani
 
Kanisa lina partner? Hiyo 20M anatoa ya nini? Na vipini anauza vya nini
 
Kapola anajua kwenda na beat na ni moja ya pastors wanaolijua neno vizurii...kiukweli ni milionea mkubwa miaka 3 ijayo! acha ale madhabauni waliosoma wakale maofisini..
 
Kijana mdogo mnataka awe anavaaa masuti muda woteee??? au yale manguo ya kumwagaaaa...
 
Kapola anajua kwenda na beat na ni moja ya pastors wanaolijua neno vizurii...kiukweli ni milionea mkubwa miaka 3 ijayo! acha ale madhabauni waliosoma wakale maofisini..
Kwani mbona nasikia naye kasoma rural development kwanini anashindwa kuajiriwa badala yake anakula pesa za akina mama maskini?
 
Kwani mbona nasikia naye kasoma rural development kwanini anashindwa kuajiriwa anakula pesa za akina mama?
kwani wew ukiajiriwa na serikali utalipwa mshahara kwa hela za kina nani??? kama sio kodi za vibibii na mama zetu wanaotafuta juani...
 
Kijana mdogo mnataka awe anavaaa masuti muda woteee??? au yale manguo ya kumwagaaaa...
Kwa hiyo mchungaji kuvaa kihuni wewe unaona sawa? Atawakanyaje wale waumini wanaovaa ovyo?
 
Kwa hiyo mchungaji kuvaa kihuni wewe unaona sawa? Atawakanyaje wale waumini wanaovaa ovyo?
kuvaa jeans ni uhuni??? au lini kavaa mlegezo?? lini kavaa hereni??? wew kama ni mzee baki na uzee wako acha vijana waishi kisasa...
 
kwani wew ukiajiriwa na serikali utalipwa mshahara kwa hela za kina nani??? kama sio kodi za vibibii na mama zetu wanaotafuta juani...
Kwanini sasa asitafute ajira ili allipwe kodi za kila mtu badala ya kutegemea sadaka za akina mama tu?
 
Kwanini sasa asitafute ajira ili allipwe kodi za kila mtu badala ya kutegemea sadaka za akina mama tu?
wew kama umeajiriwa endelea kupiga kaziii...kila mtu na uwezo wake wa kujiongeza kama umeamua kusubiri laki 3 mwisho wa mwezi endelea kusubiri.
 

Simfahamu huyo Tony.ila mahubiri ya utajirisho ndiyo yanayoharibu imani za wengi

Iko hiv naona hatari ya watu kuasi imani ya kikristo hapo baadaye kidogo.
mfano mtu umemwambia afunge atoe sadaka ili kuondoa laana sijui ya mababu inayosababisha asiwe na mafanikio.

huyu mtu akifanya hivyo mara mbili tatu halafu asione matokeo isipokuwa anaona wewe mchungajaji unabadilisha magari mapya kila siku, anageneralize wachungaji wote ni matapeli

Turudi kule kwenye injili za wazee wetu akina kulola,kuhubiri habari za uzima wa roho siyo wa mwili peke yake.

Finally,tusome bible kwa msaada wa Roho Mtakatifu.Ili hata kiongozi wako wa kiroho akiingia chaka/akipotosha unamwacha mwenyewe huko.Yaani imefika mahali huwezi tofautisha Ibada na sessions za akina Mauki(motivational speakers).

Principle Mhimu,ni hivi sadaka yoyote lazima Roho matakatifu atakuongoza,utatoa kwa kutanguliza kumpenda Mungu toka ndani mwako.Na si ya moja kwa moja kwamba kwamba ukitoa tu sadaka basi mambo yananyooka ,viko vigezo na masharti mengine mengi ambayo hayazungumzwi sababu haya vutii.mfano kuacha kabisa dhambi.Wengi wanasahau kwamba Mungu hashawishiwi na aina ya sadaka ili kukubariki
Wengi wanazungumzia sadaka wanakurudishaga agano la kale ,watakuelezea kuhusu Ibrahimu kumtoa isaka(kwamba mtoe isaka wako) .Wanachosahau ni kwamba Ibrahimu aliambiwa na Mungu mwenyewe.kwanini wao hawataki wewe usubiri maelekezo ya Mungu,kwamba utoe sadaka gani na uipeleke wapi.Ukitoa sadaka kwa lengo la kupata kitu huo ni mchango wako kwa ajili ya kumtunza huyo mhubiri jambo ambalo siyo kitu kibaya,ila siyo kusingizia eti Mungu kasema.kuna zile sadaka za kiutaratibu wa kimadhehebu,nyingi ya hizo ni michango tuu ya kutunza shughuli za kanisa ni mhimu kufanya hivyo ili huduma za kikanisa ziendelee.na kwa makanisa ya watu binafsi hizo hizo wazoita sadaka ni fedha tuu wanakusanya kwa ajili ya kuzitumia watakavyo.

Ndiyo maana wengi wa wahubili binafsi wameingia kwenye kitu kinaitwa "CuLT" sijui tafsiri yake hasa .ila hii ni aina ya ulaghai wa kuteka fikra za watu kwa ustadi mkubwa sana hasa wanawake na kuwaaminisha matokeo ya miujizi ilihali ni "FAKE".nadhani mmeshaona wahubiri wanawachapa waumini,wengine wanalishwa majani,wengine wanakaliwa na nabii na mambo ambayo kwa hali ya kawaida ni ya kushangaza.

Boton line,Mambo ya Mungu yanaenda Kwa "Akili na kwa Roho" ukiacha kimoja umeliwa
 
wengi wenye tattoo ni za enzi za ujanani
Kuna hao lakini pia kuna vijana wa sasa. Concept kubwa ipo kwa wengi kuona kuwa Mungu anaangalia ndani zaidi kuliko nje ndio maana wanaamua kuvaa wanavyotaka .. Ni sawa na Gospel ya Rose Muhando ilivyoanza, wengi walimkosoa kuwa anacheza kupita kiasi naye akajibu kuwa daudi alicheza hadi nguo zimvuka..

Kwa hiyo hapo utaona kwa sasa, jila mtu anaangalia kifungu cha bible kinachomhalalishia anachokipenda, then anaishi nacho
 
tuliqmbiwa tutawatambua kwa matendo hatujaji ila tukiona matendo ya kigaigai bas hakika mtu huyo ni mgaigai
 
Mchungaji kijana avae mavazi yanayofaankuvaliwa na mtu wa nafasi ya uchungaji.

UKWELI Huwa umenyooka, haupindi.
 
Ndugu yako yupo njema sana! Kuna kitu ananufaika zaidi ya waumini wenzie? [emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…