Mawakili wa Mbowe waache maswali yasiyo na msingi, ulizeni maswali ya maana mteja wenu aachiwe haraka

Nadhani hujaelewa kuwa hii ni kesi ndogo ndani ya kesi kubwa.

Hapa kinachotafutwa, ni je maandishi ambayo Polisi wanadai ni maelezo ya watuhumiwa, yapokelewe mahakamani kama kielelezo kwenye ushahidi, au yatupiliwe mbali.

Ndiyo maana katika kesi hii ndogo, husikii wakimwongelea Mbowe. Watuhumiwa wameeleza kuwa walilazimishwa kusaini maelezo yaliyoandaliwa na Polisi. Na katika maelezo hayo, Polisi wanadai kuwa waliambiwa na watuhiwa kuwa walikuwa wameandaliwa na Mbowe kufanya ugaidi. Nje ya maelezo hayo, Polisi hawana kielelzo kingine wala ushahidi wa kuthibitisha kuwa Mbowe amewahi kufanya mipango ya ugaidi.

Mawakili wa Mbowe wapo makini sana, na maswali yote yanayoulizwa, kwa anayejua sheria, na kinachotafutwa, ni ya msingi sana.
 
Mkuu sheria isikie tu,unasema wanasema wanauliza maswali ya kijinga??wewe kweli ni hamnazo umessoma fani hii ya sheria??nijibu hilo kwanza sheria ni pamoja na technic za kuwin kesi mapema iwezekanavyo.
Mifano ya hayo maswali japo juu ndiyo inaweza kumchomoa Mbowe katika kesi hii mapema zaidi kuliko baadhi ya maswali wanayokomalia Mawakili wake.

Niweke wazi mtazamo wangu. Tofauti na wengi mnavyodhani (wanaompinga au kumtetea), Mbowe hawezi kuhukumiwa kwa kesi hii. Nimewahi kuandika humu kwa nini nadhani amekamatwa in the first place na nini ni game plan ya Serikali.
 
Mtuhumiwa mlimkamata akiwa anakunywa supu au anatembea? tayari swali hilo la wakili msomi halafu baada ya jibu hakuna kinachofuata yaani alikuwa na maana gani kuuliza swali kama hilo
Wewe ndugu yangu, inaonekana hujui chochote kabisa maswali ya sheria. Wewe ni mtupu. Tumia hii kesi kujipatia japo elimu ndogo ya mambo ya sheria.

Hilo swali huelewi lililenga nini.

Wakati wa ushahidi, cha kwanza ni kwa hakimu au jaji kujua mtoa ushahidi kama anatakiwa kuaminika au kupuuzwa. Kama shahidi mmoja akisema waliwakamata watuhumiwa wakinywa sumu, na mwingine akasema waliwakamata wakiwa wanatembea barabarani, kitakachodhihirika ni kuwa mashahidi ni waongo, siyo watu ambao ushahidi wao unastahili kupewa uzito.
 
Labda walikuwa wanatembea huku wanakunywa supu! Utani pembeni, huo mkanganyiko una maana na faida gani kwa Mbowe katika kesi hii?
Ndugu yangu wewe huelewi kitu kabisa. Tulia. Kama ni shule, wenzio wapo Darasa la 7, wewe upo chekechea. Hata namna ya kukuelewesha inakuwa ni ngumu. Angalao ungekuwa na basics, ingekuwa rahisi kukuelimisha. Maswali hayo, ambayo kwa sababu ya umbumbumbu, unayaona hayana maana, ni ya msingi sana, ndiyo maana wakati fulani mawakili wa serikali wanaomba kurudia kumwuliza tena maswali shahidi wao, ili angalao ku-neutralize majibu yanayoufanya ushahidi wa shahidi wao upuuzwe na jaji kutokana na uthibitisho wa wazi kuwa mashahidi wao ni waongo.
 
Hayo ndiyo maswali wazee wakubambika makesi walikuwa wamejiandaa kujibu Nini? PGO Kwanza iwakae kichwani mtajua utu na umafya. Wale wakurupukaji utawajua na wangine wamekula mawe Kama mvua huko Malawi. Tatizo ni Ishu. Pesa achana nayo. Supu igaramie sio kufungua bank mfukoni kwa watu.

Hata maaskari wengine wamechoka kuonea raia kwa kulazimishwa. Maaskari wengine wana ubinadamu, sio wote.

Pongezi kwa askari kuwa wawazi kabisa kuhusu PGO.
 
Mtuhumiwa mlimkamata akiwa anakunywa supu au anatembea? tayari swali hilo la wakili msomi halafu baada ya jibu hakuna kinachofuata yaani alikuwa na maana gani kuuliza swali kama hilo
Soma nje ya box pia mkuu,maswali hayo yanalenga kumpima shahidi kama anaongea ukweli na anakumbuka kilichotokea,next time tulia na shirikisha ubongo wako kwenye maamuzi
 
Mkuu, usidhani sikuelewi au sijui unachokisema. Nadhani tofauti yetu ni mtazamo wa kwa nini kesi hii imefunguliwa in the first place. Kwa jinsi mawakili wanavyokalia maswali ya namna hii, ndiyo adhma ya serikali inapotimia, ambayo kwa upande wangu nadhani ni kumtoa tu Mbowe kwenye ulingo wa siasa kwa muda fulani. Hawana nia ya kumfunga Mbowe, hilo mimi naamini kabisa.

Waachane na preliminary examinations hizo, kama maswali ya msingi kama niliyosema hayawezi kuulizwa wakati huu, waipe pressure serikali na upande wa mashitaka kwa kuomba kesi iende kwenye trial na judgement haraka halafu wakayaulize haya maswali huko. Hilo litawavuruga zaidi maana nia ni kuipeleka kesi taratibu kwa jinsi inavyowezekana.
 
Mtuhumiwa mlimkamata akiwa anakunywa supu au anatembea? tayari swali hilo la wakili msomi halafu baada ya jibu hakuna kinachofuata yaani alikuwa na maana gani kuuliza swali kama hilo
Alitakatu ajiridhishe kama hataunajielewaelewa.asije kupoteza muda na nguvu
 
Mnataka hivyo ili mvute pumnzi kwa uhuru,kwa kuwa mnanyima wengine uhuru,hasa kwa madai ya katiba mpya na uhuru wa kufanya siasa.
 
wanahangaika na PGO badala ya POTA
 

aisee hamna kitu unajua pumzika utazame yanayoendeles.
maswali kwa mashahidi yanabase kwenye facts na sio kwenye assumptions.
 
Nyie Ni vilaza,afande Kingai alisema waliwakamata watuhumiwa wakiwa wanakunywa supu, shaidi mwingine anasema waliwakamata wakati wakiwa wanatembea, Sasa ulitaka waulizwe kuhusu wewe kwanini mtoto wa haramu!!!!
Kama ungekuwa wakili mahiri ungejiunga na jopo la mawakili. Hujii lolote. Kanywe K-Vant tu maana hill ndo unaliweza!
 
Nyie Ni vilaza,afande Kingai alisema waliwakamata watuhumiwa wakiwa wanakunywa supu, shaidi mwingine anasema waliwakamata wakati wakiwa wanatembea, Sasa ulitaka waulizwe kuhusu wewe kwanini mtoto wa haramu!!!!
Mwishoni wakili wa serikali anauliza- watu uliowakamata wako hapa mahakamani
shahidi- Ndiyo
wakili wa serikali- unaweza kuwa tambua
shahidi- ndiyo
wakili wa serikali- nenda kamguse kila mtuhumia na kutaja jina lake
shahidi- anaenda na kuwagusa watuhumia wote kwa usahihi
Mawakili wasomi wasio na UTU wao wanahangaika na PGO na character assassination
 
Ili wakati mwingine waifuate pgo na sii kumkomoa yeyote ilmradi.
 
Bado kesi ya hyo maswali haijaanza. Kwasasa kesi ni ya kuteswa/kutokuteswsshahidi. Baasi
 
Mtuhumiwa mlimkamata akiwa anakunywa supu au anatembea? tayari swali hilo la wakili msomi halafu baada ya jibu hakuna kinachofuata yaani alikuwa na maana gani kuuliza swali kama hilo
Jaji tayari analo jibu. Maana shahidi wa kwanza kasema walikuwa wana kunywa supu wapili kasema walikuwa wana tembea. Wakati shahidi wa kwanza na wa pili walikuwa pamoja..
 
... great thinker; great presenter! Wewe umejibu hoja kwa ufasaha na kwa lugha rahisi na ya kueleweka! Thank you.
 
kesi yenyewe ya kubumba na kuchonga. kamwambie dpp aifute
 
Acha kujikweza kuhusu fani ambayo hujui lolote!! Unadhani wangekuwa wanauliza maswali yasiyohusu kitu Jaji angewaruhusu?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…