Mawakili wamkataa Jaji Biswalo, wamuandikia barua Rais Samia

Mawakili wamkataa Jaji Biswalo, wamuandikia barua Rais Samia

Nilidhani wana fact kumbe hear say! Ushahidi ukiwa wa wazi na upo sahihi wamfungulie mashitaka sio kukurupuka na barua za kishabiki.
Ushahidi wao ni baada ya Rais kutamka generalities. Hawa 2 walihukumiwa makosa ya jinai wana chuki binafsi, kikawaida hela za serksli hulipwa kwa wahasibu zikakaa kwenye strongroom au safe hazikai nyumbani kwa DPP.
 
Waanika tuhuma dhidi yake, wataka zichunguzwe.

View attachment 2505238
Hivi watu wa usalama wa taifa huwa wanakuwa wapi mpaka tuhuma kama hizi kubwa zinapotokea katika ofisi nyeti za umma!? Hivi sheria iliyopelekea kuamzishwa kwa TISS, na uwepo wao katika kila idara nyeti ya serikali inatusaidia nini kama Taifa endapo kama karibu katika kila sehemu nyeti kuna upigaji, rushwa, ubadhirifu na ufisadi wa kutisha!?

Waziri mwenye dhamana ya utawala bora, Je! Uwepo wa ofisi yake yenye utitiri mkubwa wa wafanyazi ambao wapo chini yake, wenye dhamana kubwa ya kuwa "watching dogs" kwa rasirimali za nchi, hivi huwa wanakuwa wapi pale uozo wa kutisha unapotokea na kuliingiza taifa katika hasara kubwa!?

Kibaya zaidi habari za ubadhirifu huwa zinakuja na kuanza kufahamika kwa umma zikiwa zimechelewa sana, lakini jambo la kushangaza ni kwamba, hata zikiwekwa wazi viongozi wenye dhamana ya nidhamu kwa wahusika nao huanza kulalamika tu badala ya kuwachukulia hatua stahiki za kinidhamu. Kuna kila haja ya kujenga taasisi imara ya urais, ambayo inawajibika na haisiti kuchukua hatua stahiki kwa wanadhirifu, kuliko kuishia kutumbua, kuhamisha na kulalamika.

Inaudhi sana kusikia sijui mara zipo familia 12 ambazo hazigusiki, ambazo shughuli zao za kilimo zinaleta athari kubwa katika mabonde ya Usangu na Ruaha Kuu. Mara utasikia watu fulani wakiguswa nchi itatikisika, mara kiongozi fulani wa juu anahusika katika kashfa fulani, n.k.
 
Ushahidi wao ni baada ya Rais kutamka generalities. Hawa 2 walihukumiwa makosa ya jinai wana chuki binafsi, kikawaida hela za serksli hulipwa kwa wahasibu zikakaa kwenye strongroom au safe hazikai nyumbani kwa DPP.
Yamkini umeongea kwa kujifurahisha tu!
Kama unakumbuka vizuri report ya Cag ilitamka wazi kwamba awali kulikua hakuna Sheria yoyote iliyotungwa na bunge kwa ajili ya kukusanya hizo fedha za plea bargain! Ilitungwa baadae kwa hati yabdharura! That's why fedha hizo zilibaki bila kutumiwa kabisa kwa sababu hakukua na Sheria zinaoongoza matumizi yyake.

Baada ya taarifa hiyo ya Cag wahuni wakanza kuzichezea!

Swali kwako tatizo likeshagundulika Kuna uhuni umefanyika! Je tukae kimya kwa sababu kina Tito tunahisi Wana chuki binafsi au tuchukue hatua kwa kuwa Sheria na kanuni za utumishi wa umma zimekiukwa kwa maslahi mapana ya Taifa letu?

Kila Jambo likiibuliwa ambalo linaathiri ustawi wa taiffa tukilichukulia kwa angle ya chuki binafsi Kama Taifa tutapiga hatua? Hasa kwenye suala la uadilifu kwa waliopewa dhamana?
Adios
 
Huyo taahira madeleka ni wa kumsikiliza kweli??
 
Nani alimteua kuwa jaji, tuanzie hapo kwanza
Kaisome katiba ya JMT IBARA YA 110 NA ILE YA 118 jitahidi uwe unasoma soma sio unauliza maswali Kama mtoto mdogo, kasome jaji mkuu anapatikanaje, majaaji wa Mahakama kuu wanapatikanaje na majaji wa Mahakama ya Rufani wanapatikanaje na baada ya hapo kasome namna ya kumuondoa jaji katika nafasi yake kwa sababu ya kushindwa kutumiza majukumu yake kwa ugonjwa au tabia mbaya kinyume na kanuni za utumishi wa umma na Mahakama kwa ujumla!

Ukishasoma utakua na maarifa ya kutosha kujadili hoja hii!

Kama katiba huna ingia playstore au istore download "katiba ya Tanzania"

Usiwe unapenda vitu rahisi rahisi tu hapa Ni GT platform lazima uwe knowledgeable on the subject matter , ukiona Jambo linakuzidi umri na thinking capacity liache Kuna jukwa la uhusiano mapenzi na urafiki Kuna Uzi unaitwa ulishawahi kula tuda kimasihara?
 
Ushahidi wao ni baada ya Rais kutamka generalities. Hawa 2 walihukumiwa makosa ya jinai wana chuki binafsi, kikawaida hela za serksli hulipwa kwa wahasibu zikakaa kwenye strongroom au safe hazikai nyumbani kwa DPP.
Ndio waje na ushahidi usio tia shaka... kauli za wanasiasa unazifahamu hawachelewi kuzikana au zikatolewa ufafanuzi kwamba hakua na maana hiyo. In court of law we are dealing with facts not assumption.
 
Kumuondoa Jaji ndio kuna hatua za kufuata mpaka kuunda Tribunal Board ifuate mchakato wote ila kumuondoa Jaji Mkuu hakuna mchakato wowote wa kufuata. Ibara ya 118 ya Katiba iweka wazi hapo.
Hata hivyo ibara ya 110 ya katiba yetu bado inatoa madaraka makubwa kwa Rais kuamua kumuacha kazini au kumfuta kazi,
Katiba yenyewe pia haimlazimishi Rais kuunda time ya kijaji, inasema "akiona inafaa" na hakuna wa kumuuliza, Sasa hapa utaona madaraka makubwa ya Rais katika kuamua Hilo! Ndio Mana katiba mpya Ni muhimu kumpunguzia Rais haya madaraka, ikitokea Judge Ni swahiba wake aweza kuamua kukaa kimya tu!
Kwa hiyo bado Rais ana uwezo wa kumuondoa jaji bila 'tribunal board' akiona inafaa ?...
 
Aliyeibua hiyo kashfa ndiye anaandikiwa tena barua kubembelezwa achukue hatua!

Komaeni hadi VP Mpango anaweza asichomoke hapa!
 
Nashauri hiyo tume ya Haki Jinai iliyo teuliwa na Mh. Rais ichunguze pia tuhuma nzito zinazo elekezwa kwa huyu Jaji kwani tuhuma dhidi yake ni nzito na kamwe hazifai kupuuziwa kwani zina haribu taswira ya mahakama kwa kiasi kikubwa sana.

Lakini pia ni wakati muafaka wa Tume hiyo ya Haki Jinai kuchunguza taratibu nzima za upendekezwaji wa majina ya Majaji ili kuepuka kuteua Majaji wasio wadilifu wenye kashfa nzito. inaonekana wazi kuna tatizo kubwa sana tena sana.
 
Sema tu kwa vile ni Tanzania.
Jaji haondolewi kizembe sehemu nyinginezo.
Jaji kuweza kuondolewa ni lazima kuwepo na malalamiko dhidi yake. Hiki kinachoendelea ndiyo utaratibu wenyewe. Kitakachofuata baada ya hapa, ni kuundwa kamati ya majaji ya kumchunguza. Majaji hawa watatoka mahakama kuu na nchi nyingine za Jumuiya ya Madola. Hayo yatafanyika akiwa amesimamishwa.

Tuhuma zikidhihirika atafukuzwa, na taratibu za kushtakiwa zitafuata.
 
Back
Top Bottom