Mawaziri Selemani Jafo na Dotto Biteko watunukiwa PhD ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

Mawaziri Selemani Jafo na Dotto Biteko watunukiwa PhD ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)

jafo kipindi cha mwendazake, kuna mzee alimbananisha arudishe pesa za ujenzi alikuwa ni mkandarasi

wakati anamhoji mzee kajitupa chini kazirai, sema alichoharibu yule mzee alipeleka mikono mfukoni huku kazimia,

jafo nae kashtuka ,kakomaa nae tuu mzee amka bhana, rudisha pesa. Akatoa agizo huyu mzee akiamka mumkamate aeleze ni wapi amepeleka pesa.
 
Mwambie huyo jamaa...hajui na ni mbishi hatari...huyo hata masters hana...nimemjibu hat haelewi maskini ya Mungu ubishi tu wa wabongo hat kama kitu hajui.
Wewe mwenye masters mbona unaonekana ngumbaru tu hapa!
Yaani hivyo vitu vichache ulivyokariri unaamini ndio kila kitu, umeshamaliza elimu yote iliyoko ulimwenguni? Umejifungia kwenye kashimo kako hako unajiona mjanja sana!
 
Huu sasa ndio u-snitch kabisa! Hizi mbona ni studies mbili tofauti zenye uwezekano wa kufanana variables chache tu? Study populations ni tofauti. Respondents ni tofauti. Hata research questions na methodology lazima ziwe tofauti, kwa kutazama title tu. Daudi Biriye amechunguza hizo factors katika wilaya moja nchini Kenya, wakati Dr Jafo amechunguza "mediating role of management" katika kushughulikia hizo factors kwa Tanzania nzima, na huenda hata factors zenyewe hazifanani.
Acheni wivu jamani.
Which Management is mediating?
 
Kuna kautamaduni kameibuka ka kuchukia watu wanaofanya bidii na kufanikiwa katika kazi, biashara, masomo au hata maisha kwa ujumla.

Ukipata cheo watasema umependelewa, ukifanikiwa kibiashara watasema ni freemason una misukule dukani, ukifanikiwa kielimu utasikia mara hii si lolote si chochote amefoji tu! Acheni hizo. Acheni wivu.

Kama na nyie mnataka kuwa 'doctor' kasomeni. Mwenzenu Jafo amebukua pale UDOM huku akiendelea na majukumu yake ya uwaziri, na leo anatunukiwa PhD yake.

Kuna jitu nimeona huko limeshaenda kufukua huko mitandaoni linadai hiyo thesis ya Jafo inafanana na ya nani sijui wa huko Kenya! Hivi, kati yako wewe wa madongo kuinama na maprofesa wa UDOM, ni nani mwenye uwezo wa kutambua kuwa thesis iko sahihi au la?

Unaamini kabisa kuwa unaweza kuwakosoa maprofesa waliomsimamia Jafo hadi leo anapomalizia defense?

Narudia: acheni wivu. Kama jambo huliwezi sema "siwezi", usiseme "haiwezekani". Jafo ameweza, wengine igeni, jifunzeni.

Hongera sana Selemani Jafo, PhD.
Niliposoma maelezo haya, nimeamini akili haikutoshi au una matatizo ya ufahamu. Unaamini kabisa UDOM ina maprofesa ambao ni wakubwa sana, wanajua sana hawawezi kutoa digrii za kishenzi, ni wataalamu sana! Huijui UDOM na hujui elimu ya vyuo vikuu na hujui elimu za wanasiasa.
 
tumemlipa sasa Phd yake kupitia Dk Msukuma...mwingine akipata Phd nasisi tunampeleka Kibajaji....mkiongeza Kishimba naye anakula Phd ...mkizingua tena Mbowe naye anakula Phd..
 
Niliposoma maelezo haya, nimeamini akili haikutoshi au una matatizo ya ufahamu. Unaamini kabisa UDOM ina maprofesa ambao ni wakubwa sana, wanajua sana hawawezi kutoa digrii za kishenzi, ni wataalamu sana! Huijui UDOM na hujui elimu ya vyuo vikuu na hujui elimu za wanasiasa.
Kwa kusema hayo kuhusu chuo chetu cha UDOM unataka kutuaminisha nini? Kwamba wale madaktari waliohitimu UDOM na sasa wanahudumu katika mahospitali nchi nzima hawafai? Hujafa hujaumbika ndugu, utakabwa na mfupa wa samaki au utapata ajali ya bodaboda uvunjike kidevu ukakutane na madaktari kutoka UDOM halafu tuone kama utaendeleza matusi yako. Unamaanisha wale waalimu waliohitimu UDOM na sasa wanafundisha katika mashule nchi nzima, ya serikali na ya binafsi, unatuambia hao hawafai? kwani wanao wanasoma wapi mwenzetu, au bado kinda hujapata familia? Unataka kutuambia wale wanasheria waliohitimu UDOM na sasa wanahudumu katika mahakama zetu kama mawakili, waendesha mashitaka na mahakimu, kwamba ni wa hovyo? Utapata kesi hivi karibuni ukakutane nao. Usijiamini sana, hujui kesho yako. Acha dharau.
 
Kwa kusema hayo kuhusu chuo chetu cha UDOM unataka kutuaminisha nini? Kwamba wale madaktari waliohitimu UDOM na sasa wanahudumu katika mahospitali nchi nzima hawafai? Hujafa hujaumbika ndugu, utakabwa na mfupa wa samaki au utapata ajali ya bodaboda uvunjike kidevu ukakutane na madaktari kutoka UDOM halafu tuone kama utaendeleza matusi yako. Unamaanisha wale waalimu waliohitimu UDOM na sasa wanafundisha katika mashule nchi nzima, ya serikali na ya binafsi, unatuambia hao hawafai? kwani wanao wanasoma wapi mwenzetu, au bado kinda hujapata familia? Unataka kutuambia wale wanasheria waliohitimu UDOM na sasa wanahudumu katika mahakama zetu kama mawakili, waendesha mashitaka na mahakimu, kwamba ni wa hovyo? Utapata kesi hivi karibuni ukakutane nao. Usijiamini sana, hujui kesho yako. Acha dharau.
Usiombee watu mabaya ili umuhimu wako uonekane. Wengine tunaona ubaya na udhaifu wako kila siku! Jilani yangu hapa kijijini anatibu magonjwa sugu na hajawahi kupitia UDOM yako.
 
Basi Sawa!2025 atakuwa lecture huku Kisarawe tunakwenda na Mpendu.By wa Ukae.
 
Usiombee watu mabaya ili umuhimu wako uonekane. Wengine tunaona ubaya na udhaifu wako kila siku! Jilani yangu hapa kijijini anatibu magonjwa sugu na hajawahi kupitia UDOM yako.
Usifananishe sangoma na wataalamu waliohakikiwa
 
Mawaziri wawili wa Tanzania, ni miongoni mwa wahitimu 42 waliotunikiwa shahada ya udaktari wa Falsafa (Phd) katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).
Mawaziri hao ni Waziri wa Madini, Dotto Biteko na Selemani Jafo ambaye ni Waziri katika Ofisi ya Rais Muungano na Mazingira.

Wawili hao wametunikiwa shahada hizo katika mahafali ya 12 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga leo Alhamis Desemba 16, 2021.

Wametunukiwa shahada zao na Mkuu wa Chuo hicho, Dk stergomena Tax. Kiongozi mwingine aliyetunikiwa shahada ya uzamivu ni Mbunge wa Dodoma Mjini, Antony Mavunde ambaye ametunikiwa shahada ya uzamivu ya umahiri ya mahusiano ya kimataifa.

Awali, Dk Stergomena alisimikwa kuwa mkuu wa chuo hicho baada ya kuteuliwa na Rais, Samia Suluhu Hassan Juni, mwaka huu, baada ya aliyekuwa mkuu wa chuo hicho, Balozi John Kijazi kufariki dunia Februari, mwaka huu.

Hongera sana mawaziri najua haikuwa rahisi
Pamoja na majukumu yenu mazito ya uwaziri lakini mmeweza kuhitimu masomo yenu
 
Mawaziri wawili wa Tanzania, ni miongoni mwa wahitimu 42 waliotunikiwa shahada ya udaktari wa Falsafa (Phd) katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).
Mawaziri hao ni Waziri wa Madini, Dotto Biteko na Selemani Jafo ambaye ni Waziri katika Ofisi ya Rais Muungano na Mazingira.

Wawili hao wametunikiwa shahada hizo katika mahafali ya 12 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Chimwaga leo Alhamis Desemba 16, 2021.

Wametunukiwa shahada zao na Mkuu wa Chuo hicho, Dk stergomena Tax. Kiongozi mwingine aliyetunikiwa shahada ya uzamivu ni Mbunge wa Dodoma Mjini, Antony Mavunde ambaye ametunikiwa shahada ya uzamivu ya umahiri ya mahusiano ya kimataifa.

Awali, Dk Stergomena alisimikwa kuwa mkuu wa chuo hicho baada ya kuteuliwa na Rais, Samia Suluhu Hassan Juni, mwaka huu, baada ya aliyekuwa mkuu wa chuo hicho, Balozi John Kijazi kufariki dunia Februari, mwaka huu.

Hongera sana mawaziri wetu najua haikuwa rahisi
Pamoja na majukumu yenu mazito ya uwaziri lakini mmeweza kuhitimu masomo yenu
 
PhD za mchongo zimekuwa nyingi sana.

Tukiwaambia waonyeshe thesis zao utakuta ni zakubumba bumba tu wala hazina impact yoyote hapa nchini hata kwa ngazi ya kijiji tu.
 
Back
Top Bottom