Mbeya: 40 Mbaroni tuhuma za wizi kwa kuingilia Mfumo wa TEHAMA

Haya mambo ya upigaji hayapo Mbeya tu bali halmashauri nyingi zinatakiwa kufanyiwiwa panel beating,na kibaya zaidi mwendo huu wa kubembelezana ni sawa na kucheza na nyani katika shamba LA mahindi.
 
Watu 40 wameiba sh milion 450 yaani kila mtu sh milion 11 tena tangu mwaka 2018 hadi sasa ni miaka mitano
Kugawa milion 450,000,000÷40= 11,125,000 kwa kila mmoja.
Kwa mwaka 11,250,000÷5= 2,250,000
Yaani kwa mwaka kila mtu aliiba 2,250,000.
Kwa mwezi 2,250,000÷12=187,500
Hivi nayo mnaita ufisadi ndani ya nchi hii iliyojaa ufisadi wa kutisha kila kona?

1): Ndege watu walikula cha juu (udalali) toka bilion 37 kuwa billion 85 wakaongeza cha juu 48 billion.
Na hakuna hatua walichukuliwa zaidi ya kuitwa "stupid "

2): Ngorongoro watu wamepiga mpunga mrefu Wamasai ardhi yao ikauzwa na safi tu, km hakuna kilichotokea.

3): Bandari na DP World tumeshuhudia watu wanakula Bata Dubai.
Leo wanapambana kuigawa bure bandari.
Nimengi mno yakukera na hatujasikia yakitolewa tamko lolote.

Hitimisho, hao raia wa mbeya kuna dalili zote za kuonewa na wanasiasa kutafuta kick za kijinga!
 
Mbona walikaa kimya mpk Rais aseme?
 
Wako 40,, ukipiga hesabu 450 gawanya kwa hao inakuja 11 ml,, je hiyo ni pesa kweli alafu toka mwaka 2018,,, duuu ,,, kuna mijizi mikubwa ipo tuuuu
 
Kama jambo hilo la kiharifu limetekelezwa kwenye ngazi ya halmashauri inawezekana ngazi ya TRA nako kuna uharifu wa aina hiyo.Wahusika wafanyie uchunguzi mifumo yote ya ukusanyaji mapato.
 
Ndiyo maana vijana tunataka ingia serikali i hata halmashauri tu. Mirija kama hii
 
mfumo huo wa ‘uchotaji’ fedha ulianza tangu 2018 na jumla ya Sh450 milioni zimeibiwa katika miaka mitano katika maeneo ya Mbeya, Njombe, Rukwa, Songwe na Ruvuma.

Duuuh kumbe tangu enzi za NZIRANKENDE JIKONO JANDAMA watu walikuwa wanapiga kwenye mifumo? Si tuliambiwa kulikuwa hakuna WIZI kwasababu ya Control Number?

"NALO PIA MKALITAZAME " -SSH
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…