MBEZI: Rais Magufuli azindua kituo kikuu cha Mabasi ya Mikoani

MBEZI: Rais Magufuli azindua kituo kikuu cha Mabasi ya Mikoani

Nimefatilia sehemu hotuba, Bus terminal eti anafuraha sana, awali hawakuwepo wa kuomba( Wabunge upinzani) leo anaombwa kwa unyenyekevu mbuge Mtemvu. Kwamba Dar yote ni raha tupu.

Ushauri wangu kauli hizi za kibaguzi hazijengi taifa, ni bora awatumie ccm wabadili katiba, endapo ni kweli serikali ya wapinzani( mjumuisho) ilikwamisha maendeleo. Pia kauli miaka 60, kwanini hawakujenga stand kama hii? Ndege? Reli? Hizi kauli hazina afya kwa taifa.
 
Mzungu kakuzidi ndo maana ukaweza kua hapa jf otherwise ungekua unaandika kwenye makaratasi ambayo nayo yaliletwa na mzungu
Akili mbovu kabisa kila kitu eti mfano Marekani nk.... huwezi ata jisifia kutoa mifano hai ya waafrika wenzanko tabia hii hua inanikwaza sana kila kitu mzungu, mzungu .........................
 
Instagram media - CLrD_CKnmJi ( 640 X 640 ).jpg
 
Mbona hiki kituo cha mabus kinaonekana bado hakijakamilika..haraka zote za nn
 
Hio stand imepewa jina gani la swahiba Ili tuanze kujizoeza
 
Mbona hiki kituo cha mabus kinaonekana bado hakijakamilika..haraka zote za nn
Usishangae SGR Dar Moro ikafunguliwa mapema kwq demo kutest behewa kuacha legacy, phase 2 kitu SA hakina masihara.
 
ila mheshimiwa hajui kamari inayochezwa hapo kupata eneo la biashara ni mtihani mkubwa hapo ni shimo la RUSHWA hakika walio nacho wataongezewa hizo zabuni watashinda wakina bakrhessa, then kunakuwa na vipandikizi akina sisi eneo ni kubwa ni fursa kwa wajasiriamali but kama huwezi kumtoa adui MDUDU RUSHWA. hata korido ya kuuzia vocha hupati naomba viongozi waliangalie kwa mbali....japo nia kuu ni kuongeza mapato.
 
Hii tuifungulie uzi wake mkuu. Nilimskia pia akiongelea hii nikabaki mdomo wazi.

Katka yote nimevutiwa na mbunge wa kibamba alivyopewa nafasi akaitumia vizuri kuyaelezea matatizo ya wananchi wake kwa njia inayompendeza mtukufu Jiwe.
Ila kanyenyekea Sana.
 
Kauli hii ya mkuu wa nchi yetu ameitoa leo wakati anafanya ufunguzi rasmi wa stendi mpya ya mabasi ya mbezi mwisho ambayo kwa sasa inaitwa stendi ya Magufuli.

Huku akishangiliwa kwa furaha na akina mama na vijana ambao kwao sasa inaonekana kuwa ni fursa . Rais Magufuli ametoa agizo kwa waziri wa Tamisemi kuwa machinga na mamalishe waruhusiwe kufanya biashara kwenye stendi hiyo ili nao wanufaike.

Kwa sababu rais Magufuli amepewa jina la stendi hiyo na yeye hapendi kuona wanyonge wananyanyaswa ameagiza Waziri Jaffo kuhakikisha raia wanyonge wananufaika na mradi mkakati huu.

Stendi hii itakuwa inahudumia mabasi 3000 kwa siku hivyo abiria watakuwa wanahitaji chakula na kununua bidhaa muhimu. Kwa hiyo ni fursa kwa raia wanyonge hasa mamalishe na wamachinga.

My take; Rais Magufuli amekuwa mstari wa mbele kutetea wanyonge na wanaoonewa, tumpongeze kwa hili.
 
KWA KAULI YA JPM,

Nawaskitikia sana
Waliochukua fremu za biashara ndani ya stend kwa gharama kubwa IMEKULA KWAO.

Machinga watauza bidhaa ile Ile kwenye kibaraza cha frem uliolipia mwenyewe,

Wateja hawataona umuhimu wa kuingia ndani ya frem lako,
Na watauziwa biadhaa ile ile kwa Bei ya chini zaidi,

na huna Cha kuwafanya kwasababu mweshimiwa tayari keshasema[emoji1]

MUHUDUMU[emoji1635], MITANO TENA TAFADHALI[emoji1]
 
Akili mbovu kabisa kila kitu eti mfano Marekani nk. Huwezi ata jisifia kutoa mifano hai ya waafrika wenzanko tabia hii hua inanikwaza sana kila kitu mzungu, mzungu.
Tatizo lako unatumia muda msingi sana kwenye korido za CCM Lumumba, ukienda mitaa ya Kinondoni utajua kuwa South Africa iko Afrika siyo Marekani wala Ulaya.
 
Baada ya kufungua daraja la juu la Kijazi sasa Rais Magufuli amewasili Kituo kikuu kipya cha mabasi ya mikoani tayari kabisa kwa kukifungua rasmi.

Watu ni wengi sana.

Up dates;

====

WAZIRI JAFO AAGIZA MKURUGENZI WA JIJI KUANDAA BANGO LA STENDI YA MAGUFULI

Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI, Selemani Jafo amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam kuandaa bango litakaloitambulisha Stendi ya Magufuli

Jafo amesema hayo katika uzinduzi wa Stendi mpya ya mabasi yaendayo Mikoani na Nchi jirani iliyoko Mbezi Luis

Pia, amemuomba radhi Rais Magufuli kwa kutumia jina lake kwenye stendi hiyo kabla ya kumuomba ridhaa

BAADHI YA ALIYOZUNGUMZA RAIS MAGUFULI:

Maendeleo hayana chama, lakini lazima kuwepo na chama kinachotoa maelekezo. Wananchi wa Kibamba hamkukosea, tembeeni kifua mbele

Sifurahii sana majina yangu kutumika kwenye vitu namna hii. Kwa sababu mnaweza kuita Magufuli Stand, halafu Wamachinga na Mamalishe wakawa wananyanyaswa hapa

Nitaumia sana kama Wananchi hawa wanyonge watakuwa wanafukuzwa, halafu pameandikwa Magufuli. Maana yake itakuwa ni Magufuli anayewafukuza, kwa hiyo sitakubali

Katika stendi hii kuna vitu vingi vizuri ambavyo sijui kama watu wa kawaida wataingia. Kuna Hoteli ambayo sijui kama Machinga ataruhusiwa kuingia

Nakubali hii stendi kuitwa jina langu. Kwahiyo nataka stendi itakapoanza hawa Wamachinga wasifukuzwe kwa sababu ni kwao

Jengeni utaratibu kwa hawa wafanyabiashara ndogo ndogo ili mabasi yakiingia wanunue chakula kwa Mama Ntilie. Watakaokuwa na hela watanunua kwenye mahoteli lakini mihogo na matikiti maji yanunuliwe

Miaka 60 tangu tupate Uhuru hakujajengwa stendi nzuri kama hii. Miaka 60 baada ya Uhuru hakujajengwa 'flyovers' kama ile ya Ubungo. Ni lazima Watanzania mtembee kifua mbele

Najua hii ni 'challenge' kwa Viongozi, kwamba hapa tutafanyaje. Ni kazi ya Viongozi kutatua changamoto. Kwahiyo mjipange mpige bongo vichwa vyenu kujua hawa wengine ambao wameshalipa elfu 20 watafanyaje biashara zao hapa

Ile barabara ya njia nane tuliomba Wafadhili wakaturingia, nikamuita Mfugale nikamuuliza hatuwezi kujenga hii? Akasema tunaweza. Nikamwambia tengeneza njia nane ili hasira yangu iwapate kabisa

=====

RAIS MAGUFULI: MAENDELEO HAYANA CHAMA, LAKINI LAZIMA KIWEPO CHAMA KINACHOTOA MAELEKEZO

Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amesema unapokuwa Kiongozi, ni lazima upate watu wanaowakilisha watu kwakuwa bila 'connection' kazi haziendi

Ametoa kauli hiyo leo Jijini Dar es Salaam wakati akizindua stendi ya Mabasi ya Mbezi Luis ambayo imepewa jina la Magufuli Bus Terminal

Amesema, "Dar es Salaam karibu yote ilikuwa watoto wa jirani, sasa mmenizalia watoto asilia. Maendeleo hayana Chama lakini lazima kiwepo chama kinachotoa maelekezo"

View attachment 1710840

View attachment 1710913

View attachment 1710841

View attachment 1710910
View attachment 1710895

View attachment 1710896
Wananchi wakishangilia baada ya Rais kusema jambo lililowafurahisha
Mzee huyu!!! Kwani kituo kilianza wakati wa mbunge gani? Watu mna shangilia ujinga tuu.
 
Wabongo tujitahidi kuwa wasafi basi
Wakuangaliwa sana sana ni wamachinga na mama lishe...

Ova
 
Back
Top Bottom