Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Wewe ni tabula rasa

Umesoma ila haujaelimika
Bro mbona unanitukana, kwani kosa langu lipowapi? Jamaa kasema Pepo inamaana mashetani. Sasa nikamuuliza mnaposema Peponi ina maana gani? Sasa nimekosea nini?
 
The concept of above is not real.
Sisi wanafizikia tunasema hakuna juu wala chini.
Juu ni dhana ya kuhusisha vitu viwili.
Ulimwengu una vitu viwili vikuu.
Space
Time.
Above is just a relative term(relativity theory).
Ulimwengu ni Ombwe kubwa ndani yake kuna vitu vingi vinaelea.
Bila kuzama sana kwa kuzingatia sheria za fizikia ni kwamba kila gimba moja linaweza kuwa juu ya lingine.
Kwa mujibu wa fizikia, ulimwengu huzaliwa na kufa, kuna galaxy system nyingi sana nazo huzaliwa na kufa
Pembezoni sana mwa galaxy yetu panaitwa hyperspace.
Hil jua ni sehemu ndogo sana ya galaxy na halipo juu wala chini.
Wewe ulienda juu ipi? Juu ya kitu gani.

Ndoto huwa ni imagination ya yale tuyawazayo mda mwingi wakati wa mchana.
Fikra zenu nyingi sana zimejikita kwenye ndoto na si uhalisia wa kuona,kusikia, kugusa, kunusa, kuonja.
Mnapozungumzia lugha, kiswahili ni lugha imegunfuliwa juxi tu hsta miaka 1000 hsina iweje huko mbinguni waimbe kwa kiswahili wakati dunia ipo tangu zamani, au uko wanafuata ugunduzi wa duniani.
Maelezo yako yanamashaks mengi sana na hayana logic.
 
Wanasayansi wanaenda in deep space kwa vyombo maalumu, wanadini wanaenda kwa kuota..
Mkija kuzindika mmebaki peke yenu wenzenu wapo mars wanajiandaa kwenda jupiter wakitumia roketi zenye speed kali zaidi ya mwanga.
 
Hata zumaridi the queen alisemaga hivi hivi tofauti ni aina ya maelezo tu.Ubarikiwe nabii wa kizazi cha leo.
 
Nimeona watu wengi humu JF wakimponda na kumkashfu Mwalimu Mwakasege baada ya kusema Mungu alimfunulia kuhusu mbingu na kwenda Mbinguni.

Binafsi nadeclare interest kuwa ninatumika Kanisa la TAG kama Mzee wa Kanisa huku Nyanda za juu kusini pia ni Mtumishi wa Serikali na huwa nahubiri mara moja moja. Siandiki hivi kwa kufurahisha watu au kujisifu wala kutaka kumsafisha Mwalimu Mwakasege ila naeleza kile nilichoshuhudia na kile ambacho Mungu amenitendea.

Kwa umri na muda niliomtumikia Mungu kama Mkristo nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeye binafsi na pia kuwafunulia kuhusu wengi kuhusu mbingu.

Binafsi, nashuhudia leo na kikiwa na akili timamu na dhamira njema Moyoni mwangu kuwa nimemuona mwenye haki "Yesu Kristo" si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na amenitokea kwa namna mbalimbali tofauti na watu wanavyokashfu kuwa tutatokewa na Mapepo yaliyovaa sura ya "Bryan Deacon" yule aliyeigiza "Filamu ya Yesu" Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Mafunuo haya ya kutokewa na Yesu kwangu mimi hayakuwa kwa jinsi ya kimwili "yaani kunitokea physically" ila ni katika ndoto na Maono ya usiku pia wakati nasali nikajiona tu nimekutana naye.

Leo sitaelezea kuhusu kutokewa na Yesu ila nitaelezea kuhusu ushuhuda wangu wa kuiona Mbingu ila nasisitiza katika hilo, kila maono, ndoto au mafunuo ya Kimungu yanajengwa chini ya Neno la Mungu. Neno: Ayubu 33:14-16 hapa Mungu anasema kuhusu kusema na wanadamu kuhusu ndoto ns mqono ya usiku.

Neno: Yoel 2: 28-29 Anasema kuhusu "Ndoto na Maono".

Kuhusu Mungu kuwafunulia watumishi wake mbingu, tunaona Paulo anasema namna alivyochukuliwa na kuoneshwa kuhusu Mbingu katika 2 Korintho 12: 2-9 pia Stephano naye anafunuliwa katika Matendo ya Mitume 7:56 na pia Mtume Yohana anafunuliwa kuhusu Mbingu wakati anaandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Binafsi, Nakumbuka ilikuwa 2016. Mungu alinipa Neno toka Yeremia 33:3 inayosema "Niite nami nitakuitikia na nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua" pia kwa muda mrefu nilikuwa naimba moyoni mwangu wimbo mmoja wa zamani sijui uliimbwa na kwaya gani ila kuna kipande wanaimba " Nimpeleleza nani raha ya Mbingu×2, Yesu ndiye wa Kumpeleleza"

Nakumbuka Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale kidogo ili nikiamka saa 1 hivi niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri nikaona Malaika mmoja aliye kama mwanadamu amevaa mavazi meupe yenye kung'ara huku akiwa mwenye sura inayong'ara ananiambia "nimetumwa nikufuate". Akanishika mkono, nikaona natoka kwenye mwili upande wenye moyo.

Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu huku akiwa amenishika Mkono. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani. Tukapaa juu kwa spidi nikaangalia chini tena na kuona kadunia kalivyo kadogo then tukafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kumuabudu Mungu. Nikaungana nao tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.

Binafsi, nimewasikia na kuwaona watumishi wengi wa Mungu wanaoshuhudia kuhusu Mbingu huku kwetu na sehemu myingine. Ukiacha hao maarufu, japo "Zumaridi hapana kwani inaonekana ana shida ya akili" Ukiacha Mwakasege, hata Marehemu Kulola alishashuhudia siku moja kufunuliwa kuhusu Mbingu.

Nami nimeona nishare uzoefu wangu kuhusu Mafunuo ya Mbingu. Siku nyingine nitaeleza kuhusu kutokewa na Yesu ana tutokeaje, yupoje na tunajuaje kama ni Yesu.

Asanteni.
Kapime akili yako usijekuwa una tatizo ambalo liko wazi. Kweli afya ya akili ugogoro kwa sasa duniani.
 
Inategemea na level yako ya kufikiria kuhusu utajiri kwani hakuna kipimo rasmi cha utajiri na umaskini humu duniani. Wengine wakiwa na afya njema ni matajiri, wengine wakiwa na uhakika wa kula na kuvaa ni matajiri, wengine wakiwa na watoto ni matajiri kama ambavyo wewe unajiona tajiri kwa kuwa unamchepuko mama J maana ndio kitu pekee cha thamani ulichonacho na ndio maana kutwa nzima unakitangaza humu. Kwa hiyo usiongee wala kujeneralize vitu bro.
Elimu dunia uloisoma na kuiamini na kuitumia kujibu mitihani mpk ukaajiriwa imeclassify level mbalimbali za uchumi,shida ukishapata ugali elimu dunia mnaikataa
 
The concept of above is not real.
Sisi wanafizikia tunasema hakuna juu wala chini.
Juu ni dhana ya kuhusisha vitu viwili.
Ulimwengu una vitu viwili vikuu.
Space
Time.
Above is just a relative term(relativity theory).
Ulimwengu ni Ombwe kubwa ndani yake kuna vitu vingi vinaelea.
Bila kuzama sana kwa kuzingatia sheria za fizikia ni kwamba kila gimba moja linaweza kuwa juu ya lingine.
Kwa mujibu wa fizikia, ulimwengu huzaliwa na kufa, kuna galaxy system nyingi sana nazo huzaliwa na kufa
Pembezoni sana mwa galaxy yetu panaitwa hyperspace.
Hil jua ni sehemu ndogo sana ya galaxy na halipo juu wala chini.
Wewe ulienda juu ipi? Juu ya kitu gani.

Ndoto huwa ni imagination ya yale tuyawazayo mda mwingi wakati wa mchana.
Fikra zenu nyingi sana zimejikita kwenye ndoto na si uhalisia wa kuona,kusikia, kugusa, kunusa, kuonja.
Mnapozungumzia lugha, kiswahili ni lugha imegunfuliwa juxi tu hsta miaka 1000 hsina iweje huko mbinguni waimbe kwa kiswahili wakati dunia ipo tangu zamani, au uko wanafuata ugunduzi wa duniani.
Maelezo yako yanamashaks mengi sana na hayana logic.
Wacha weeeeeeee japo huu upuuzi wako sijausoma hata punje. Nilipoona tu mwana fizikia, nikaacha.
 
Jibu kwanza mbona unayumba,unasema ulipaa juu bas nambie km unaamini mbinguni ni juu me nikupe nondo zangu unipe majibu?!!

Nataka nijue km una ufaham ama umechanganyikiwa?!
Hahaaaaaaa, haya bwana kuwa na usiku mwema.
 
Watumishi wanaotangaza kuwa wamekwenda mbinguni wanaongezeka Kila uchao, kalibia watatangaza sadaka na michango yakuwasaidia waumini nao waende mbinguni Waka msalimie Mungu.
Kwani ni kosa kufunuliwa kwenda Mbinguni? Nianze kujigunza kwako, wewe ni dini gani? Unaamini kuhusu uwepo wa Mbingu?
 
Na ulicho nacho ni kiwango cha juu cha imani
Barikiwa sana
Dunia ina mambo mengi, nimeona na kupitia mengi. Binafsi, nilikuwa kama hawa napinga uwepo wa Mungu. Ila baada ya kushughulikiwa nikamrudia Mungu naye akajifunua kwangu kwa namna ya ajabu. Toka 2012, nimeona na kujigunza mengi kuhusu Mungu. Hakuna mwanadamu wala Pepo litakalo nidanganya sasa nisiamini kuhusu Mungu.
 
Nimeona watu wengi humu JF wakimponda na kumkashfu Mwalimu Mwakasege baada ya kusema Mungu alimfunulia kuhusu mbingu na kwenda Mbinguni.

Binafsi nadeclare interest kuwa ninatumika Kanisa la TAG kama Mzee wa Kanisa huku Nyanda za juu kusini pia ni Mtumishi wa Serikali na huwa nahubiri mara moja moja. Siandiki hivi kwa kufurahisha watu au kujisifu wala kutaka kumsafisha Mwalimu Mwakasege ila naeleza kile nilichoshuhudia na kile ambacho Mungu amenitendea.

Kwa umri na muda niliomtumikia Mungu kama Mkristo nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeye binafsi na pia kuwafunulia kuhusu wengi kuhusu mbingu.

Binafsi, nashuhudia leo na kikiwa na akili timamu na dhamira njema Moyoni mwangu kuwa nimemuona mwenye haki "Yesu Kristo" si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na amenitokea kwa namna mbalimbali tofauti na watu wanavyokashfu kuwa tutatokewa na Mapepo yaliyovaa sura ya "Bryan Deacon" yule aliyeigiza "Filamu ya Yesu" Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Mafunuo haya ya kutokewa na Yesu kwangu mimi hayakuwa kwa jinsi ya kimwili "yaani kunitokea physically" ila ni katika ndoto na Maono ya usiku pia wakati nasali nikajiona tu nimekutana naye.

Leo sitaelezea kuhusu kutokewa na Yesu ila nitaelezea kuhusu ushuhuda wangu wa kuiona Mbingu ila nasisitiza katika hilo, kila maono, ndoto au mafunuo ya Kimungu yanajengwa chini ya Neno la Mungu. Neno: Ayubu 33:14-16 hapa Mungu anasema kuhusu kusema na wanadamu kuhusu ndoto ns mqono ya usiku.

Neno: Yoel 2: 28-29 Anasema kuhusu "Ndoto na Maono".

Kuhusu Mungu kuwafunulia watumishi wake mbingu, tunaona Paulo anasema namna alivyochukuliwa na kuoneshwa kuhusu Mbingu katika 2 Korintho 12: 2-9 pia Stephano naye anafunuliwa katika Matendo ya Mitume 7:56 na pia Mtume Yohana anafunuliwa kuhusu Mbingu wakati anaandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Binafsi, Nakumbuka ilikuwa 2016. Mungu alinipa Neno toka Yeremia 33:3 inayosema "Niite nami nitakuitikia na nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua" pia kwa muda mrefu nilikuwa naimba moyoni mwangu wimbo mmoja wa zamani sijui uliimbwa na kwaya gani ila kuna kipande wanaimba " Nimpeleleza nani raha ya Mbingu×2, Yesu ndiye wa Kumpeleleza"

Nakumbuka Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale kidogo ili nikiamka saa 1 hivi niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri nikaona Malaika mmoja aliye kama mwanadamu amevaa mavazi meupe yenye kung'ara huku akiwa mwenye sura inayong'ara ananiambia "nimetumwa nikufuate". Akanishika mkono, nikaona natoka kwenye mwili upande wenye moyo.

Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu huku akiwa amenishika Mkono. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani. Tukapaa juu kwa spidi nikaangalia chini tena na kuona kadunia kalivyo kadogo then tukafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kumuabudu Mungu. Nikaungana nao tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.

Binafsi, nimewasikia na kuwaona watumishi wengi wa Mungu wanaoshuhudia kuhusu Mbingu huku kwetu na sehemu myingine. Ukiacha hao maarufu, japo "Zumaridi hapana kwani inaonekana ana shida ya akili" Ukiacha Mwakasege, hata Marehemu Kulola alishashuhudia siku moja kufunuliwa kuhusu Mbingu.

Nami nimeona nishare uzoefu wangu kuhusu Mafunuo ya Mbingu. Siku nyingine nitaeleza kuhusu kutokewa na Yesu ana tutokeaje, yupoje na tunajuaje kama ni Yesu.

Asanteni.
Malaika alikuwa mwanaume au mwanamke?
 
Back
Top Bottom