Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Hajawahi kunibabaisha kwani najua ana shida gani? Waliopinga uwepo wa Mungu walikuwepo na watakuwepo hadi mwisho wa dahari. Hana mpya na Biblia inawaita "Wapumbavu" kwa umri wangu, hanipati, hanibabaishi, haniyumbishi wala hanipotezei muda wangu kujibizana naye kuhusu uwepo wa Mungu kwani macho yangu yameshuhudia mengi yanayothibitisha pasi na shaka uwepo wa Mungu na wala sina mashaka naye. Najua alikuwepo, yupo na atakuwepo milele na milele. Poleni kwa huo "Upumbavu" uliowajaa ila samahani kwa hilo mkuu.
Mchungaji naomba nikiri mimi ni mpumbavu lakini kiranga ni mpumbavu mara 700 zaidi yangu.Amina
 
Wanasayansi wanaenda in deep space kwa vyombo maalumu, wanadini wanaenda kwa kuota..
Mkija kuzindika mmebaki peke yenu wenzenu wapo mars wanajiandaa kwenda jupiter wakitumia roketi zenye speed kali zaidi ya mwanga.
Hahaaaaa, zote ni kujilisha upepo tu mkuu, hata waende Jupiter ila wakizidi sana ni miaka 80. Wataacha vyote, watawekwa pamba mdomoni na masikioni. Watakuwa kama sanamu, hawataiona tena hiyo Mars, hawataviona tena hivyo vifaa, hawatakuwa na uwezo wa kuvipanda, watafukiwa kwenye kaburi then wataoza na kuliwa na Funza. Je umilele wao utakuwa wapi? Bro, hata tufanyaje humu duniani ila kuchagua umilele wako ni jambo la msingi sasa. Umilele wa Roho yako usiyo haribika unaandaliwa sasa. Bro, Mungu ni kweli, Mbingu ni kweli na halisi, kuzimu ipo, Hukumu ya Milele ipo Mkuu. Jiandae sasa bro na umilele wako kwani hizo "science and abracadabra" hazikusaidii kitu.

Nilipomaliza Msc. Yangu pale SUA nilijiona Msomi, nikipinga uwepo wa Mungu ila niliposhughulikiwa na science isiyoonekana na nikanusurika Kufa pale hospitali ya Mpanda sasa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi tarehe 6/6/2012 ndipo nilipojua kuwa Mungu yupo. Sema sana na tamba sana ila Omba yasikukute. Hiyo sayansi haitakusaidia kitu kwani ilipoishia sayansi, ndipo Ulimwengu wa Roho ulipoanzia
 
Mwska 1984 nilipelekwa mahala pazuri sana ssna. Sikuchukuliwa ndotoni bali nilipelekwa nakumbuka ilikuwa kabla ya usiku wa saa sita.

Nimewahi kuwaona viumbe wabaya wskiwa katika miili. Malaika, majini na mapepo wote ni roho. Huwa wanavaa miili kukamilisha mission zao.

Majini nimeona
Mapepo nimeona
MAlaika humtokea mtu kwa hali isiyomletea taharuki mja wa Mungu.

Ni story ndefu sana
Hao viumbe wabaya wakiwa katika miili ya kibinadamu uliwaona 'live' ?..

..natamani usimulie kidogo..
 
Dunia ina mambo mengi, nimeona na kupitia mengi. Binafsi, nilikuwa kama hawa napinga uwepo wa Mungu. Ila baada ya kushughulikiwa nikamrudia Mungu naye akajifunua kwangu kwa namna ya ajabu. Toka 2012, nimeona na kujigunza mengi kuhusu Mungu. Hakuna mwanadamu wala Pepo litakalo nidanganya sasa nisiamini kuhusu Mungu.

Mambo unayoongea ni ya rohoni sana yanatoka kwa roho uliyemjua ukamuamini.
Wanaokupinga wana roho inayowatumia kupingana na kweli.

Yesu atusaidie sana
 
Nimeona watu wengi humu JF wakimponda na kumkashfu Mwalimu Mwakasege baada ya kusema Mungu alimfunulia kuhusu mbingu na kwenda Mbinguni.

Binafsi nadeclare interest kuwa ninatumika Kanisa la TAG kama Mzee wa Kanisa huku Nyanda za juu kusini pia ni Mtumishi wa Serikali na huwa nahubiri mara moja moja. Siandiki hivi kwa kufurahisha watu au kujisifu wala kutaka kumsafisha Mwalimu Mwakasege ila naeleza kile nilichoshuhudia na kile ambacho Mungu amenitendea.

Kwa umri na muda niliomtumikia Mungu kama Mkristo nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeye binafsi na pia kuwafunulia kuhusu wengi kuhusu mbingu.

Binafsi, nashuhudia leo na kikiwa na akili timamu na dhamira njema Moyoni mwangu kuwa nimemuona mwenye haki "Yesu Kristo" si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo na amenitokea kwa namna mbalimbali tofauti na watu wanavyokashfu kuwa tutatokewa na Mapepo yaliyovaa sura ya "Bryan Deacon" yule aliyeigiza "Filamu ya Yesu" Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Mafunuo haya ya kutokewa na Yesu kwangu mimi hayakuwa kwa jinsi ya kimwili "yaani kunitokea physically" ila ni katika ndoto na Maono ya usiku pia wakati nasali nikajiona tu nimekutana naye.

Leo sitaelezea kuhusu kutokewa na Yesu ila nitaelezea kuhusu ushuhuda wangu wa kuiona Mbingu ila nasisitiza katika hilo, kila maono, ndoto au mafunuo ya Kimungu yanajengwa chini ya Neno la Mungu. Neno: Ayubu 33:14-16 hapa Mungu anasema kuhusu kusema na wanadamu kuhusu ndoto ns mqono ya usiku.

Neno: Yoel 2: 28-29 Anasema kuhusu "Ndoto na Maono".

Kuhusu Mungu kuwafunulia watumishi wake mbingu, tunaona Paulo anasema namna alivyochukuliwa na kuoneshwa kuhusu Mbingu katika 2 Korintho 12: 2-9 pia Stephano naye anafunuliwa katika Matendo ya Mitume 7:56 na pia Mtume Yohana anafunuliwa kuhusu Mbingu wakati anaandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

Binafsi, Nakumbuka ilikuwa 2016. Mungu alinipa Neno toka Yeremia 33:3 inayosema "Niite nami nitakuitikia na nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua" pia kwa muda mrefu nilikuwa naimba moyoni mwangu wimbo mmoja wa zamani sijui uliimbwa na kwaya gani ila kuna kipande wanaimba " Nimpeleleza nani raha ya Mbingu×2, Yesu ndiye wa Kumpeleleza"

Nakumbuka Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale kidogo ili nikiamka saa 1 hivi niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri nikaona Malaika mmoja aliye kama mwanadamu amevaa mavazi meupe yenye kung'ara huku akiwa mwenye sura inayong'ara ananiambia "nimetumwa nikufuate". Akanishika mkono, nikaona natoka kwenye mwili upande wenye moyo.

Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu huku akiwa amenishika Mkono. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani. Tukapaa juu kwa spidi nikaangalia chini tena na kuona kadunia kalivyo kadogo then tukafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kumuabudu Mungu. Nikaungana nao tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.

Binafsi, nimewasikia na kuwaona watumishi wengi wa Mungu wanaoshuhudia kuhusu Mbingu huku kwetu na sehemu myingine. Ukiacha hao maarufu, japo "Zumaridi hapana kwani inaonekana ana shida ya akili" Ukiacha Mwakasege, hata Marehemu Kulola alishashuhudia siku moja kufunuliwa kuhusu Mbingu.

Nami nimeona nishare uzoefu wangu kuhusu Mafunuo ya Mbingu. Siku nyingine nitaeleza kuhusu kutokewa na Yesu ana tutokeaje, yupoje na tunajuaje kama ni Yesu.

Asanteni.
Wewe hakuna malaika anaevaa mavazi meupe, malaika wote ambao ni watumishi wa mungu wanavaa mavazi meusi.
 
Binafsi naishi na nimefika hapa kwa uweza Mungu, kwa plan na akili yangu nilishafeli ila sikuacha kukuomba Mungu naamini amenifikisha hapa na zaidi ya hapa.
 
Hao viumbe wabaya wakiwa katika miili ya kibinadamu uliwaona 'live' ?..

..natamani usimulie kidogo..
Yes niliwaona na si mara moja.

Uongo mwingi sana umeenezwa kuwa roho chafu za kishetani hubeba maumbo mabaya.

Shetani ni kiumbe kisicho na mwili ambacho kina uwezo wa kuishi na kuendesha mwili wowote usio takaswa.

Shetani ana akili kuliko binadamu yeyote yule hata muwakusanye pamoja. Kiumbe ambaye amewahi kuuona UTUKUFU. Wa Mungu katika Enzi BORA kabisa ni kiumbe wa kuwa na tahadhari naye sana.

Yesu hakukosea aliposema shetani anaweza kuja kama malaika wa Nuru na watumishi wake wakaja kama watumishi wa haki.

Shetani anaifahamu Biblia kuliko tunavyodhani. Hata alipoenda kumjaribu Yesu alitumia maandiko as reference.

Nimesoma watu wengi wakisema wametokewa na malaika na hawajawahi kuthibitisha kama wale walikuwa ni malaika au la. Kuna Mkorea mmoja anaitwa Choo Nam ameandika NI KWELI MBINGU IPO lakini ukisoma kitabu chake utagundua kuwa alishindwa lupambanua roho alizokutana nazo akidai ni Yesu na kadhalika.

Mkuu. Nina hadithi ndefu sana lakini kwa ufupi Mbingu ipo. Ushahidi wa kwenda na kurudi upo lakini tambua kuwa Mungu wetu anafanyakazi kwa utaratibu na KUSUDI hata anapoamua kukupeleka Mbinguni anakuwa na kusudi. Unaendaje kupiga story Mbinguni?

Kuna mengi Roho wa Mungu anatufunilia na kusudi la mafunuo hayo ni kuthibitisha Neno lake.

Mungu hana swagga, ana majira na maongozi yake
 
Hahaaaaa, zote ni kujilisha upepo tu mkuu, hata waende Jupiter ila wakizidi sana ni miaka 80. Wataacha vyote, watawekwa pamba mdomoni na masikioni. Watakuwa kama sanamu, hawataiona tena hiyo Mars, hawataviona tena hivyo vifaa, hawatakuwa na uwezo wa kuvipanda, watafukiwa kwenye kaburi then wataoza na kulowa na Simba. Je umilele wao utakiwa wapi? Bro, hata tufanyaje humu duniani ila kuchagua umilele wako ni jambo la msingi sasa. Umilele wa Roho yako usiyo haribika unaandaliwa sasa. Bro, Mungu ni kweli, Mbingu ni kweli na halisi, kuzimu ipo, Hukumu ya Milele ipo Mkuu. Jiandae sasa bro na umilele wako kwani hizo "science and abracadabra" hazikusaidii kitu.

Nilipomaliza Msc. Yangu pale SUA nilijiona Msomi, nikiponga uwepo wa Mungu ila niliposhughulikiwa na sciemce isiyoonekana na nikanusurika Kufa pale hospitali ya Mpanda sasa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi tarehe 6/6/2012 ndipo nilipojua kuwa Mungu yupo. Sema sana na tamba sana ila Omba yasikukute. Hiyo sayansi haitakusaidia kitu kwani ilipoishia sayansi, ndipo Ulimwengi wa Roho ulipoanzia
Usijibu kwa mihemko na fear of unknown.
Kila kiumbe kitakufa hata uwe unamiujiza hewa.
Hio juu alioenda huyo bwana ni juu ipi ?
Sijaandika mahala kuwa mungu hayupo au umeona hilo neno?
Napingana na illogical thinking za halucination za usingizini na kuzifanya kuwa knowledge.
Watu wa dini wanaishi ktk kutisha watu, hawana cha zaidi.
Wanasayansi wangesikiliza maneno ya wahubiri leo dunia ingekuwa very primitive.
Dini ni jambo la kimazingira tu, upo hio dini kwa sababu ya watu waliokuzunguka ni wa dini hio. Ungezaliwa urusi ungekuwa mpagani, ungezaliwa India ungekuwa mbudha. Kwa nini kuwe na madini mengi wakati mungu ni mmoja?
Kama una amini maelezo ya mtoa nada ya kwenda mbinguni basi hio master rudisha vyeti hukuelewa bali ulikariri.
Mtu mwenye master hawezi amini vitu hovyo.
Science inafundisha kuamini fact sio opinion.
Kwa hio na master yako unaenda kupewa mafuta ya upako ili ufanikiwe eti?
Umewahi kumuona kiwete miguu imenyooka kwa kuombewa?
Bora usingetambulisha kuwa una master, maana ni mambo ya ajabu yanayoendelea huko mnakoamini.
Kaa ujue kifo ni natural thing design by creator sio adhabu kama mnavyofikiri.
Uogope usiogope utakufa tu.
 
Wacha weeeeeeee japo huu upuuzi wako sijausoma hata punje. Nilipoona tu mwana fizikia, nikaacha.
Hayo maandishi unayoandika ni kwa akili ya wanafizikia. Wana tiolojia wanaishia kubwabwaha tu, eti wanaruka usingizini. Wanasayansi wabaruma wakiwa macho meupe pee.
Subiri uote uruke uje utuhadithihie kesho.
Kama ni kubarikiwa basi wanafizikia ndio viumbe waliobarikiwa hapa duniani maana wanaunda wakitakacho, wanaruka mchana nyie mnaruka usiku.
Sasa hivi wameunda maroboti ya kuwasaidia nyie wanamiujiza kufikiti sawa sawa maaba akili zenu hamzitumii vizuri.
Kazi yenu kuwasema tu eti mafreemason huku mkifaidi akili yao ya ubunifu wa hali ya juu.
 
Hayo maandishi unayoandika ni kwa akili ya wanafizikia. Wana tiolojia wanaishia kubwabwaha tu, eti wanaruka usingizini. Wanasayansi wabaruma wakiwa macho meupe pee.
Subiri uote uruke uje utuhadithihie kesho.
Kama ni kubarikiwa basi wanafizikia ndio viumbe waliobarikiwa hapa duniani maana wanaunda wakitakacho, wanaruka mchana nyie mnaruka usiku.
Sasa hivi wameunda maroboti ya kuwasaidia nyie wanamiujiza kufikiti sawa sawa maaba akili zenu hamzitumii vizuri.
Kazi yenu kuwasema tu eti mafreemason huku mkifaidi akili yao ya ubunifu wa hali ya juu.
Haya bro, kuwa na usiku mwema.
 
Usijibu kwa mihemko na fear of unknown.
Kila kiumbe kitakufa hata uwe unamiujiza hewa.
Hio juu alioenda huyo bwana ni juu ipi ?
Sijaandika mahala kuwa mungu hayupo au umeona hilo neno?
Napingana na illogical thinking za halucination za usingizini na kuzifanya kuwa knowledge.
Watu wa dini wanaishi ktk kutisha watu, hawana cha zaidi.
Wanasayansi wangesikiliza maneno ya wahubiri leo dunia ingekuwa very primitive.
Dini ni jambo la kimazingira tu, upo hio dini kwa sababu ya watu waliokuzunguka ni wa dini hio. Ungezaliwa urusi ungekuwa mpagani, ungezaliwa India ungekuwa mbudha. Kwa nini kuwe na madini mengi wakati mungu ni mmoja?
Kama una amini maelezo ya mtoa nada ya kwenda mbinguni basi hio master rudisha vyeti hukuelewa bali ulikariri.
Mtu mwenye master hawezi amini vitu hovyo.
Science inafundisha kuamini fact sio opinion.
Kwa hio na master yako unaenda kupewa mafuta ya upako ili ufanikiwe eti?
Umewahi kumuona kiwete miguu imenyooka kwa kuombewa?
Bora usingetambulisha kuwa una master, maana ni mambo ya ajabu yanayoendelea huko mnakoamini.
Kaa ujue kifo ni natural thing design by creator sio adhabu kama mnavyofikiri.
Uogope usiogope utakufa tu.
Haya kuwa na usiku mwema.
 
mtoa mada usijichoshe, humu kuna majini, mapepo, maajenti wa kuzimu wenyewe hawana neema hivyo wanapotosha hata wale wateule wachache wapotee wakati behind the keyboard wanawacheka mipumbavu inavyojifanya ina akili kuliko MUNGU, ina pua inhisi pua ilijiwekea yenyewe ina kula na kwenda chooni,inahisi kibofu kilitokea tu kama movie ,waweza kuwa una bishana kumbe unabishana na jini unahisi utaliweza
 
Back
Top Bottom