Mbingu ni kweli ipo na huu ni ushuhuda wangu binafsi

Mchungaji naomba nikiri mimi ni mpumbavu lakini kiranga ni mpumbavu mara 700 zaidi yangu.Amina
 
Wanasayansi wanaenda in deep space kwa vyombo maalumu, wanadini wanaenda kwa kuota..
Mkija kuzindika mmebaki peke yenu wenzenu wapo mars wanajiandaa kwenda jupiter wakitumia roketi zenye speed kali zaidi ya mwanga.
Hahaaaaa, zote ni kujilisha upepo tu mkuu, hata waende Jupiter ila wakizidi sana ni miaka 80. Wataacha vyote, watawekwa pamba mdomoni na masikioni. Watakuwa kama sanamu, hawataiona tena hiyo Mars, hawataviona tena hivyo vifaa, hawatakuwa na uwezo wa kuvipanda, watafukiwa kwenye kaburi then wataoza na kuliwa na Funza. Je umilele wao utakuwa wapi? Bro, hata tufanyaje humu duniani ila kuchagua umilele wako ni jambo la msingi sasa. Umilele wa Roho yako usiyo haribika unaandaliwa sasa. Bro, Mungu ni kweli, Mbingu ni kweli na halisi, kuzimu ipo, Hukumu ya Milele ipo Mkuu. Jiandae sasa bro na umilele wako kwani hizo "science and abracadabra" hazikusaidii kitu.

Nilipomaliza Msc. Yangu pale SUA nilijiona Msomi, nikipinga uwepo wa Mungu ila niliposhughulikiwa na science isiyoonekana na nikanusurika Kufa pale hospitali ya Mpanda sasa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi tarehe 6/6/2012 ndipo nilipojua kuwa Mungu yupo. Sema sana na tamba sana ila Omba yasikukute. Hiyo sayansi haitakusaidia kitu kwani ilipoishia sayansi, ndipo Ulimwengu wa Roho ulipoanzia
 
Hao viumbe wabaya wakiwa katika miili ya kibinadamu uliwaona 'live' ?..

..natamani usimulie kidogo..
 

Mambo unayoongea ni ya rohoni sana yanatoka kwa roho uliyemjua ukamuamini.
Wanaokupinga wana roho inayowatumia kupingana na kweli.

Yesu atusaidie sana
 
Wewe hakuna malaika anaevaa mavazi meupe, malaika wote ambao ni watumishi wa mungu wanavaa mavazi meusi.
 
Binafsi naishi na nimefika hapa kwa uweza Mungu, kwa plan na akili yangu nilishafeli ila sikuacha kukuomba Mungu naamini amenifikisha hapa na zaidi ya hapa.
 
Hao viumbe wabaya wakiwa katika miili ya kibinadamu uliwaona 'live' ?..

..natamani usimulie kidogo..
Yes niliwaona na si mara moja.

Uongo mwingi sana umeenezwa kuwa roho chafu za kishetani hubeba maumbo mabaya.

Shetani ni kiumbe kisicho na mwili ambacho kina uwezo wa kuishi na kuendesha mwili wowote usio takaswa.

Shetani ana akili kuliko binadamu yeyote yule hata muwakusanye pamoja. Kiumbe ambaye amewahi kuuona UTUKUFU. Wa Mungu katika Enzi BORA kabisa ni kiumbe wa kuwa na tahadhari naye sana.

Yesu hakukosea aliposema shetani anaweza kuja kama malaika wa Nuru na watumishi wake wakaja kama watumishi wa haki.

Shetani anaifahamu Biblia kuliko tunavyodhani. Hata alipoenda kumjaribu Yesu alitumia maandiko as reference.

Nimesoma watu wengi wakisema wametokewa na malaika na hawajawahi kuthibitisha kama wale walikuwa ni malaika au la. Kuna Mkorea mmoja anaitwa Choo Nam ameandika NI KWELI MBINGU IPO lakini ukisoma kitabu chake utagundua kuwa alishindwa lupambanua roho alizokutana nazo akidai ni Yesu na kadhalika.

Mkuu. Nina hadithi ndefu sana lakini kwa ufupi Mbingu ipo. Ushahidi wa kwenda na kurudi upo lakini tambua kuwa Mungu wetu anafanyakazi kwa utaratibu na KUSUDI hata anapoamua kukupeleka Mbinguni anakuwa na kusudi. Unaendaje kupiga story Mbinguni?

Kuna mengi Roho wa Mungu anatufunilia na kusudi la mafunuo hayo ni kuthibitisha Neno lake.

Mungu hana swagga, ana majira na maongozi yake
 
Usijibu kwa mihemko na fear of unknown.
Kila kiumbe kitakufa hata uwe unamiujiza hewa.
Hio juu alioenda huyo bwana ni juu ipi ?
Sijaandika mahala kuwa mungu hayupo au umeona hilo neno?
Napingana na illogical thinking za halucination za usingizini na kuzifanya kuwa knowledge.
Watu wa dini wanaishi ktk kutisha watu, hawana cha zaidi.
Wanasayansi wangesikiliza maneno ya wahubiri leo dunia ingekuwa very primitive.
Dini ni jambo la kimazingira tu, upo hio dini kwa sababu ya watu waliokuzunguka ni wa dini hio. Ungezaliwa urusi ungekuwa mpagani, ungezaliwa India ungekuwa mbudha. Kwa nini kuwe na madini mengi wakati mungu ni mmoja?
Kama una amini maelezo ya mtoa nada ya kwenda mbinguni basi hio master rudisha vyeti hukuelewa bali ulikariri.
Mtu mwenye master hawezi amini vitu hovyo.
Science inafundisha kuamini fact sio opinion.
Kwa hio na master yako unaenda kupewa mafuta ya upako ili ufanikiwe eti?
Umewahi kumuona kiwete miguu imenyooka kwa kuombewa?
Bora usingetambulisha kuwa una master, maana ni mambo ya ajabu yanayoendelea huko mnakoamini.
Kaa ujue kifo ni natural thing design by creator sio adhabu kama mnavyofikiri.
Uogope usiogope utakufa tu.
 
Wacha weeeeeeee japo huu upuuzi wako sijausoma hata punje. Nilipoona tu mwana fizikia, nikaacha.
Hayo maandishi unayoandika ni kwa akili ya wanafizikia. Wana tiolojia wanaishia kubwabwaha tu, eti wanaruka usingizini. Wanasayansi wabaruma wakiwa macho meupe pee.
Subiri uote uruke uje utuhadithihie kesho.
Kama ni kubarikiwa basi wanafizikia ndio viumbe waliobarikiwa hapa duniani maana wanaunda wakitakacho, wanaruka mchana nyie mnaruka usiku.
Sasa hivi wameunda maroboti ya kuwasaidia nyie wanamiujiza kufikiti sawa sawa maaba akili zenu hamzitumii vizuri.
Kazi yenu kuwasema tu eti mafreemason huku mkifaidi akili yao ya ubunifu wa hali ya juu.
 
Haya bro, kuwa na usiku mwema.
 
Haya kuwa na usiku mwema.
 
mtoa mada usijichoshe, humu kuna majini, mapepo, maajenti wa kuzimu wenyewe hawana neema hivyo wanapotosha hata wale wateule wachache wapotee wakati behind the keyboard wanawacheka mipumbavu inavyojifanya ina akili kuliko MUNGU, ina pua inhisi pua ilijiwekea yenyewe ina kula na kwenda chooni,inahisi kibofu kilitokea tu kama movie ,waweza kuwa una bishana kumbe unabishana na jini unahisi utaliweza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…