Mbinu nayotumia kumlea mwanangu anayesoma private awe mjanja, awe na furaha, asigeuke kuwa kuku wa kisasa

Mkuu ni heri ukae kimya tu. Nani kasema nampeleka mtoto Wangu huko kwa bibi yake kwa lengo la kumfunza aogelee au kuwinda ndege? Hivi vitu nimeandika ni mchezo tu wanayochezaga na wenzake na kuna mdingi zaidi ila kubwa kuliko yote saizi ni mcheshi, muongeaji, ana charisma, n.k na hivi ndivyo inavyotakiwa.

Kuna shule kama IST vyote hivyo kuanzia kuogelea ni karibia kila siku ila sasa watoto wengi wa pale hadi uraibu wa kucheza games za ps uwaishe wanakuaga wakubwa tayari huku social skills zikiwa zimedumaa.

Hao watoto kwenu endeleeni kuwalea kizungu zungu wawe wanacheki katini sijui siku wakishikwa hata t*ako nadhani wataona ni kawaida maana hata cartoon siku hizi zina haya mambo, kitu lipo ndani tu na mi home work ndio hawa wanakuaga masomo zege wazazi wanalalamika mbona hawana wachumba au watoto kumbe mtu hata skills za kuimbisha hana.

Nawatakia maisha mema katika malezi ya kuku zenu za kisasa, mkizitoa nje zijimix na za kienyeji subirini mkute zimedanganywa kuona vitu ndani au kuonewa
 
Mkuu Dude jeupe nakupa big up sikupingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hujamuelewa mzee.yeye kasema haamini katika kufaulu darasani au kuwa wa kwanza kwake yeye mtoto wake akiwa kumi bora inatosha

Hittin Blunts and Bustin Nuts
 
mwanae anaruka salakasi za kinyume nyume!

hivi ukiruka salakasi za kinyume nyume ni moja ya social skills??

mwanae sasahiv amepata vikesi viwili vitatu huko shuleni

kumbe kupata vikesi viwili vitatu ni moja ya social skills?!
Wanaita "kuruka back" kati ya utundu wote nilofanya utotoni hii sarakasi ilinishinda.kwakweli ukiiweza hii unapata umaarufu sana dhidi ya watoto wenzako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Dude jeupe nakupa big up sikupingi

Sent using Jamii Forums mobile app
Wanachosahau ni kwamba katika makuuzi ya mtoto kuwa na company ya wenzake ni kitu muhimu sana, Hebu tumkumbushe michezo ya utotoni ambayo kuku wa kisasa hwaijui na wanakosa uhondo wa aina yake.

-Kutengeneza manati na kuwinda ndege porini na shabaha
-Kuunda magari ya waya au udongo
-Kidali poo
-Kibabababa na kimamamama
-kombolela
-Kushona makambakamba vidoleni na kuyachezesha kwa mitindo mbalimbali
-kujifunza kugawana - ukija na kimbama,kisheti,gimbi au muwa marafiki zako lazima wapate.
-Mchezo wa kuzungusha betri kwa mijeredi
-Kupuliza kimhwepelo
-kukimbiza malingi ya baiskeli
-mpira wa chandimu
-Mchezo wa goroli

Hii michezo ina umuhimu mkubwa sana katika makuuzi ya mtoto kumfanya awe nafuraha na hata kujenga marafiki na kujifunza kuishi na jamii.

Kwa bahati mbaya kuku za kisasa hii michezo hawaijui wanachojua ni kuchezea simu, kushinda kwenye tv au computer wanacheza gemu na kufanya home work.
 
Mkuu mi hapo tu (siku hizi anaruka sarakasi za nyuma)hii life Mimi kidogo nivunje mgongo udogoni,tulikuwa tunaweka jiwe Na unakuja mbio jiwe linakupa sapoti ukilikanyaga,niliena juu sana nikajikuta nimerudi eneo hilo hilo militia kwa mgongo nikawa mashindwa hata kuhema,mbona wenzangu walinikimbia,that y ulibyosema sarakasi imebidi nicheke

mwongo atofautiani Na mchawi
 
Kama wewe sarakasi zilikushinda ni "wewe" mkuu sio "wote"

Dah mkuu sarakasi kujifunza lazima uumie umie ndio uwe imara, Nakumbuka zamani nilijifunza kuchana msamba kuna mtu aliniambia nikae ule mkao kama wa msikitini alafu akaweka miguu yake juu ya magoti akaruka juu alivyotua nilitembea kwa shida siku 2 ila baada ya hapo niliweza kupiga msamba.

Sijajua nyie mlijifunzaje hizo sarakasi ila kujifunza sarakasi za nyuma kama kuna wanaoziweza wakikufundisha sidhani kama kuna shida, sarakasi pekee ambayo labda kuna hatari ni ile cherehani
 
Wanaita "kuruka back" kati ya utundu wote nilofanya utotoni hii sarakasi ilinishinda.kwakweli ukiiweza hii unapata umaarufu sana dhidi ya watoto wenzako.

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu mimi izo sarakasi zote nimeruka utotoni, kuna mkatiko, chempu, izo za kinyuma nyuma nimeruka sana watoto wenzako wanakuona wewe mkali

lakini nilivyo kua kua nikajikuta sipendi social interaction na watu! mpaka saiv nimekua njemba nafanya maamuzi na natenga na mda wakujichanganya na mda wakuwa pekee yangu

haya mambo muda mwengine yanakua asili (ayana budi kutokea) unaweza kufundisha mwanao awe mtundu mtundu atajichanganya lakin akifika kwenye balehe ataamu mwenyew jinsi ya ku sosholayzi na watu!

mtoto anaweza akawa boya boya
utotoni lakini akikua anakumjanja na mwingine anaweza akawa mchangamfu sana utotoni lakini akikua anakuja kuwa mpoole

watu tulikuwa watundu, kwenye ugomvi tupo, mpira tumecheza, kombolela, kidali, kula mbakishie baba, kombolela utundu kama wote lakini pale secondary kama form 2 mapepe yote yakakata....
to be continue...
 
dunia ya leo sio ya jana, mambo yamebadilika sana sio kama zamani,
ni bora uchunge mwanao usimuache akazagaa kisa unataka achangamke sijui social skills utakuja kulia na kusaga meno.
acha kabisa lea mwanao na kaa nae. Elimu ya msingi ya kuishi na jamii inaanzia kwa mzazi mwenyewe,
kuna wazazi hawana muda wa kuwalea watoto wao na kuwaachia wazagae na wenzao wengi wao wameingia au wamefanyiwa vitendo vya kubakwa au kulatiwa, tuchukue tahadhari kwa watoto wetu tusiwaache wachangamane na watoto wasio funzwa na wazazi wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Heri nusu ya shari kuliko shari kamili.
 
Inapendeza mkuu, Mfungiage ndani mnunulie na game awe anachezea umuwekee na dstv ya katuni, Maisha ni kwenda shule, games na katuni

Sijaandika popote namruhusu mwanangu acheze na watoto wahuni, watoto anaocheza nao wengi wapo na maadili mema tu kama yeye, Hayo mambo ya kubakana na kulawaitiana huko kwa bibi nakompeleka sijwahi kusikia hii kesi na binafsi nimekulia huko anakoenda kwa hiyo nayajua mazingira na huu uamuzi sijafanya kwa kukurupuka
 
Nakuunga mkono sio toto la kiume mpaka linakuwa kubwa unakuta bado zembe zembe tu.
Shule kama anaweza kwenda kwa miguu au daladala afanye hivyo.
Mambo ya kuchangamana na kucheza na wenzio ni mambo ya msingi sana katika malezi.
Unakuta eti mtoto wa kiume hata kuchinja kuku hawezi.
 
Pongezi kwako
 

Unafeli sana unapochukulia elimu enzi zako na dhima yake kwa kipindi hicho na today’s education

Unazidi kufeli zaidi unajifananisha ulichosoma wewe na mazingira yako na sasa hivi

Whoever studied whatever ndani ya hii republic zamani au near past,tulikua tunasoma madudu matupu nothing worthy tukiwnda kwenye real standards

Mpeleke mtoto wako shule nzuri kabisa,na vyuo,mpeleke vyuo vyenye world’s rankings huko West au hata East,acha kufananisha ka degree kako ka uhasibu na vinavyoendelea leo kwenye elimu

Elimu inaenda kwenye finest level,kwenye nchi zenye maana,sio hizi vurumai za hii republic


“Maisha ni Safari Ila Sio Wote Wana Nauli”
 

Ucheshi na uongeaji ni tabia ambayo si lazima ijengwe kwa mtoto kwenda shule zenye watoto wengi darasani au wachache. Siamini kuwa shule zenye watoto wachache au wale watoto wanaokaa kwenye mageti hakuna watoto ambao ni karismatiki.

Kuna shule kama IST vyote hivyo kuanzia kuogelea ni karibia kila siku ila sasa watoto wengi wa pale hadi uraibu wa kucheza games za ps uwaishe wanakuaga wakubwa tayari huku social skills zikiwa zimedumaa.

Una uthibitisho gani kuhusu hili? Kuna baadhi ya mambo ni vizuri kuwa tunakuwa na msingi ya kuongelea kuliko kuhushisha hisia zetu kuzifanya kuwa uhalisia.

Tatizo la kuwaleo kizungu liko wapi? Hebu onyesha malezi ya kizungu ni yapi na ubaya wake ni upi? Mambo unayosema wakifanyiwa watoto wataona kawaida, kwa maoni yangu ni mtazamo wako sidhani kama yanaakisi hali halisi.
Sina hakika kama una takwimu kushawishi kuwa hao watoto unaosema wanalelewa kizungu wanashindwa kuoa kwa kuwa hawana ujuzi wa kuwapata wachumba.

Mtizamo wangu, furaha ya mtoto hailetwi na kufanya mambo yanayompa furaha mzazi/wazazi wake bali yale anayopenda kufanya. Ucheshi/ukimya ni tabia na haifundishwi kwa kubadilisha mazingira ya mtoto, na kati ya hizo, hakuna tabia iliyo bora kuliko nyingine, bali kila tabia ina mazingira ambapo inafaa zaidi.

Unapopata nafasi nakala za MBTI, Emotional Quotient na Social Quotient, zipo nyingi tu mtandaoni.
 
Mkuu uwe unaongea vitu ambavyo unajua kabisa ni kawaida kwenye jamii ya Tz.

Huko kwenye elimu ya ulaya naona umekula ugali kwa shangazi hapo umeshiba upo na toothpick unachokonoa nyaman mkono mwengine ndio unaandika huu upuuzi.

Tukianza hapa hapa tu ndani, Shule kama walizosoma kina pfunk na mo dewji ada ni milioni 30 na elimu ni hadhi ya juu ila ukicheki sasa, watanzania unakuta ni wawili tu darasani kati ya wanafunzi 25, na hao wazazi wao wana pesa sio mchezo.

Uwe unaongea vitu parallel kidogo ambavyo vimeendana kidogo na maisha ya mtz, Huko ulaya uanafkiri mtoto anasomeshwa kwa mapera au???

Kuhusu elimu ya hapa kwetu sioni utofauti kabisa kati ya elimu niliyosomea mimi na hii anayosomea mambo ni yale yale na huwa namfundisha mwenyewe.
 
Ucheshi na uongeaji ni tabia ambayo si lazima ijengwe kwa mtoto kwenda shule zenye watoto wengi darasani au wachache. Siamini kuwa shule zenye watoto wachache au wale watoto wanaokaa kwenye mageti hakuna watoto ambao ni karismatiki.
Mkuu shule zenye watu wachache ni kama shdarasani mpo watu wawili tu mkikosana hamsemeshani ila mkiwa wengi alternatives zinaongezeka, Darasa lina watu 18 unakuta una marafiki wawili tu ila darasa likiwa na watu 50 uwezekano wa kuwa na marafiki hata 8 upo hata wawili wakiumwa bado kuna wengine, Kuwa mcheshi kunategemeana sana na idadi ya watu waliopo kwenye circle yako


Una uthibitisho gani kuhusu hili? Kuna baadhi ya mambo ni vizuri kuwa tunakuwa na msingi ya kuongelea kuliko kuhushisha hisia zetu kuzifanya kuwa uhalisia.
Ushahidi wa gaming addiction upo mkuu cheki huyo youtube kuna kitu kinaitwa gaminga addiction na ni tatizo kubwa mno kwenye nchi za ulaya kiasi kwamba kuna rehabs kabisa, Hawa watoto wa ist wapo exposed sana nagames na kuna mtu nadhani alikuwa staff pale ist alitoa maoni jinsi games zinavyoharibu watoto pale.



Tatizo la malezi ya kizungu mkuu ni kwamba malezi yao na yetu tofauti, Mtoto wako wa kike akianza kuvaa visketi na vijinsi vinavyoishia mapajani wakati wenzake wanavaa kiheshima hapo anaonekana malaya na jamii, Pia wenzetu wazungu mtoto kuwa shoga ni kawaida ila nahisi na wewe huna tatizo mtoto wako wa kiume akipigwa miti maana huna tatizo na haya malezi utafurahia kabisa, Siwezi kulea mtoto kizungu yaani kitoto kipo 15 kinaniletea eti boyfriend wake no, no, no. Situmii sana mdomo kwenye matatizo serious huwa natia mboko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…