Mbowe ashikiwa bango kutafuna milioni 800 za ujenzi wa ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA

Mbowe ashikiwa bango kutafuna milioni 800 za ujenzi wa ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA

Jamaa ni mpigaji mzuri,halafu sijui kwanini kama hana maslah binafsi ndani ya chama kwanini asiachie wengine nao wakiongoze chama especially wakati huu chama kikiwa kwenye crisis
 
Dubai huwezi kununua nyumba kama wewe si mzawa.
Mnataka kumtoa kiongozi wetu kwenye mwelekeo wa kukijenga chama.
 
View attachment 886186

Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

View attachment 886175
Kila mkija na karakasi zenu mnakuta Wanachadema wako IMARA. Tuhuma mnazoandika leo mbona zilishatolewa karibia miaka 20 nyuma na zikatolewa ufafanuzi. Hivi vigazeti uchwara zingefungiwa lkn kwa vile anaevifungia ndio kawatuma waandike tunasubiria muda wake cjui atawaeleza nini watanzania, hiyo cku inakuja
 
Magazeti mengine kama haya ndo kijijini uwa wanaenda kujisafishia toilet
 
Janvi la habar, tanzanite, Tazama tanzania, uhuru, haya yooote hayana cha kuandika cha maana zaidi ya Mbowe na chadema huyu mtu ni mwamba kwelikweli.
 
Ni upumbavu kabisa kuletaleta habari kama hizi wakati vyombo vya sheria vipo. Hao wanaomshikia bando kama wana ushahidi wa kutosha kwanini wasimshitaki kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake?!
 
Haya madai hayakuanza leo kwani hata aliyekuwa kaimu mwenyekiti wa CDM. Marehemu Chacha Wangwe aliwahi kuliongelea hili na akatoa uthibitisho akaonekana mbaya na msaliti.
Ama kweli jicho linalopenda Upofu huuona kengeza.
Swali linakuja, kama mpaka udhibitisho mnao, kwaninni huyo mbowe hakamatwi ili sheria ichukue mkondo wake? Tumechoka na hizi habari kila siku mbowe kala hela ya chadema, mbowe kaua huyu na yule. Mkamateni tujue moja
 
Wakati mwingine ukweli unauma sana
Sasa ukweli utakuwa mara ngapi? magazeti yenu yasiyo na credibility yameandika sana. Mlianza na mla ruzuku wanachama ambao ndio wenye chama wakawapuuza, mkaja kamuua Chacha Wangwe mkapuuzwa na wote mahakama hadi familia ya marehemu, mmekuja na kalmia kwenye chanzo cha maji hadi mkafyeka shamba lake huku mnapiga selfie ili mpande vyeo na ikajulikana sio chanzo cha maji.
Hamkuishia hapo mmebomoa ukumbi wenye hadhi East and central Bills bado hajatetereka na chama kimesema kinamuamini leo mnasema kala 800m za kujenga jingo la ofisi. Hivi Mbowe angekuwa kazaliwa ukoo wa kimasikini kama huyo munayejaribu kumpendeza ingekuwaje? Huu mufanyao ni uduanzi wa kiwango cha reli ya SGR
 
Hili Gazeti ni witty mlmm nini linapenda kutumia neno "inadaiwa" kama habari zake ni za kweli? Ni kwa nini wasiseme kwamba wao kazi yao ni kuandika habari za 9swekn888kuqqhfikirika!q?
Hongera mkuu kwa kuwa mteja mzuri was hili gazeti
 
View attachment 886186

Gazeti la Fahari Yetu limeandika tuhuma dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, likimhusisha na matumizi ya milioni 800 za ujenzi wa jengo la ghorofa la Ofisi za Makao Makuu ya Chama hicho, Mtaa wa Ufipa, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Gazeti hilo limedai kuwa, Mbowe alikiuka Azimio la Kikao cha Kamati Kuu ya Chama na kuamua kutumia fedha hizo kwa matumizi yake binafsi. Inaelezwa kuwa:
  • Mbowe alinunua nyumba Dubai kwa fedha za Chama.
  • Michango ya watu binafsi kwa Chama kama akina Mzee Sobodo haijulikani zilichukuliwa lini na kwa mfumo gani na hatimaye kutumikaje.
  • Fedha zilizopatikana kupitia "Fund Raising Events" mbalimbali kama za Dar na Mwanza hazijawahi kuonekana.
  • Malalamiko kwa Mbowe kujilipa fedha kwa mnadai ya kukikopesha milioni Chama milioni 700.
  • Malalamiko dhidi ya Mbowe kukiuzia Chama magari chakavu kwa zaidi ya milioni 600 ambapo kabla ya kuyauza kwa Chama, alikuwa akiyakodisha kwa Chama.
  • Malalamiko kwa Mbowe kununua LandCruiser V8 VX 2 kwa pesa za Chama na kisha kukiuzia Chama.
  • Ripoti ya CAG ya 2016/2017 imeonyesha namna fedha za CHADEMA zinavyotafunwa na wajanja wachache.
Kulingana na Gazeti la Fahari, kila anapojitokeza Kiongozi yeyote ndani ya CHADEMA kuhoji juu ya matumizi ya fedha za Chama, wanajitokeza wapambe wake wa kumtetea kwa kutumia hoja za nguvu badala ya nguvu ya hoja. Hivyo kwa mtaji huo wa kujichotea fedha bila kuhojiwa ama kuulizwa chochote, Mbowe hawezi kuachia nafasi ya Uenyekiti wa Chama.

View attachment 886175
So what🙁🙁
 
Back
Top Bottom