Pre GE2025 Mbowe iokoe CHADEMA kwa kuchukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Lissu, usisubiri kesho!

Pre GE2025 Mbowe iokoe CHADEMA kwa kuchukua maamuzi mazito ya kumuunga mkono Lissu, usisubiri kesho!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.
Ushauri toka kwa wakongwe wa JF. Bwana Mbowe akiusikiliza na kuutafakari utamjengea heshima kubwa na hakika ustaafu wake utang'aa na kutukuka kama mfano bora.
 
Kwanini Lissu asikae pembeni amwachie Mbowe?
Baada ya miaka 20 kama mwenyekiti na sura ya chama kama inavyodaiwa, Chadema katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu imeambulia chini ya asilimia 1%.

Uongozi wa juu kabisa hauwezi kukwepa lawama kwa msimamo wao kuhusu uchafuzi waliokubali kushiriki kama chama.

"We cannot solve our problems with the same thinking we used when we created them", alisema Einstein.

Uongozi wa juu kabisa wa Chadema ulikuwa mwepesi kudanganyika ukiwa na imani potofu jinsi uchaguzi ungeendeshwa baada ya maridhiano...sababu?
 
Ni wakati wa Lissu
downloadfile-2.jpg
 
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.
Hadi Mag3 ameongea?
Basi asiposikia imeisha hiyo
 
Kama kuna mtu katukanwa, tena matusi ya nguoni, ni Mh. Tundu Antiphas Lissu na hakuanza kutukanwa juzi wala jana.

Lissu alianza kutukanwa toka uchaguzi ndani ya Chadema uanze katika ngazi za chini kabisa na nyakati hizo hakuna aliyemgusa Mbowe.

Kama yupo aliyeonesha uvumilivu mkubwa ni Mh. Tundu Antiphas Lissu. Kampeni dhidi yake zilianza mapema tu lakini alikaa kimya.

Hadi alipotaka kutetea kiti chake cha makamu wa mwanyekiti wa chama. Wenzake kumbe walishapanga safu zao tokea awali.
Ninatofautiana na wewe. Lissu alipotangaza tu kugombea wafuasi wake wakaanza kumbeza Mbowe na kutaka asigombee ( hapo hata hajaonyesha nia) ya kugombea. Dharau na vijembe vya Lissu vilianza zamani sana. Kuna wakati alimtumia surrogate wake Msigwa kumshambulia Mbowe). Hapakuwa na haja ya kumshambulia Lissu wakati ule kwa sababu hamna aliyepinga uamuzi wake wa kugombea urais.
Yericko alimshambulia baada ya kutoa tuhuma za uongo dhidi ya Wenje na viongozi wengine (ingawa hakumtaja ilikuwa wazi alimlenga Mbowe). Alipobanwa kutoa ushahidi akasema aliyempa amefariki! Tuhuma nyingine za Yericko mpaka leo hazijajibiwa. Kuwa alikuwa hahudumii nafasi ya Mwanasheria Mkuu wa CDM mpaka ikabidi apewe Kibatala. Kuwa alikuwa hahudhurii wala kuitisha vikao.

Ni baada ya haya maneno ndio Ntobi akamshambulia kwa maneno yasiyofaa lakini alibanwa akaomba msamaha. Hamna hata mmoja aliyemuomba msamaha Mbowe kwa kumuita kibaraka, king'ang'anizi n.k. Na wakati wote huu wa mashambulizi ya Lissu, Mbowe hajasema neno.

Mimi naamini hapo ulipo ni kuwa hautaki kusikia lolote baya dhidi ya Lissu. Hiyo ni haki yako kama vile ilivyokuwa haki yangu kukupinga. Lakini kwa vile nimetambua kuwa ni futile exercise, sitakujibu tena kwenye suala lolote linalohusu uchaguzi wa CHADEMA. Nitangojea matokeo na nitamkubali yeyeto atakaeshinda.

Amandla....
 
Mbona Kenya wanachama wa ODM hawajawahi taka Raila Odinga aachie madaraka ODM pamoja na kuunga mkono Serikali ya Uhuru Kenyata na sasa Ruto pia
kama Mbowe angekua na msimamo kama wa Raila Odinga hata yeye wanachama wangetaka aendelee kua mwenyekiti tu

But Mbowe hana msimamo,.na pia ni kama hajui kama siasa za nyakati zimebadirika, siasa za sasa sio kama za zamani, kifupi mawazo yake hayaendani na nyakati za sasa za siasa.

Lissu ni Raila wa huku Tz, wamefanana itikadi na misimamo, ndio sababi anahitajika zaidi kwa hizi nyakati ambazo watawala wanajifanya wababe.
 
Watu wa ajabu sana.
Kiongozi makini anapaswa kupima mafanikio yake dhidi ya majukumu yake na uwezekano wa uongozi mpya kuleta mitazamo mipya.

Ni wajibu wako kama kiongozi kuachia madaraka kwa namna itakayomwezesha kiongozi mpya kuendeleza na kujenga juu ya urithi wako.

Chonde chonde time and tide wait for no man!
 
Kiongozi makini anapaswa kupima mafanikio yake dhidi ya majukumu yake na uwezekano wa uongozi mpya kuleta mitazamo mipya.

Ni wajibu wako kama kiongozi kuachia madaraka kwa namna itakayomwezesha kiongozi mpya kuendeleza na kujenga juu ya urithi wako.

Chonde chonde time and tide wait for no man!
Unaweza kuwa sahihi. Wengi wetu tunasahau kuwa hiyo ndiyo hirizi ya kisiasa ya CCM kwamba baada ya Mwalimu Nyerere, kiongozi wa Chama anatumia mihula miwili tu ya miaka mitano mitano kwenye nafasi hiyo. Inasikitisha vyama vingine vyote havina utaratibu wa kurithishana hicho kiti. Matokeo yake ni kudorora kisiasa na hata umaarufu wa viongozi wake. Ni busara kujifunza kutoka CCM angalao katika hili hata kama hatufurahishwi na mambo yao mengine.
 
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.

Waleeee .. wanakuja..:

GfuY-ekXQAAK7pI.jpeg


Ngoja tuone.
 
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.
It's too late.

Sijui/sidhani kama Mbowe anao utashi wake tena katika maswala haya.
Hiyo nafasi unayo ieleza ilimponyoka ile wiki-endi aliyo waahidi kuzungumza na wahariri wakuu na waandishi wa habari hapo nyumbani kwake.
Hiyo ndiyo ilikuwa fursa murua sana ya haya unayo mshauri sasa.

Lakini hao wanao mshikilia, wiki-endi hiyo naona walimshinda nguvu; na sasa wamemwachia adhalilike.
 
. Ni busara kujifunza kutoka CCM angalao katika hili hata kama hatufurahishwi na mambo yao mengine
Lakini usisahau kuwa ni CCM hao hao wanao wajenga hawa wote. Lipumba, Cheyo, hata Mzee wa Kiraracha na TLP yake alisha angukia huko kwenye mtego wa CCM.
Mbowe, alidumu kwa muda mrefu kidogo; lakini sasa ndiye mwenyekiti wa hao wote walio naswa huko mwanzo.

Unajuwa kwa nini wananaswa hawa wote?
 
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.
Nyie jamaa bana, kwani Lissu hawezi kumuunga mkono Mbowe kukinusuru chama if that is the case.
 
Kiongozi makini anapaswa kupima mafanikio yake dhidi ya majukumu yake na uwezekano wa uongozi mpya kuleta mitazamo mipya.

Ni wajibu wako kama kiongozi kuachia madaraka kwa namna itakayomwezesha kiongozi mpya kuendeleza na kujenga juu ya urithi wako.

Chonde chonde time and tide wait for no man!

Erythrocyte, imhotep, Allen Kilewella, Ell, Retired, Fundi Mchundo, binti kiziwi nk, nini kimempata mwamba? Busara zote hizi hazina maana yoyote kwake?
 
Mheshimiwa mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe, ukitangaza leo kwamba baada ya tafakuri nzito umeamua kutogombea kwa mara nyingine uenyekiti wa Chadema leo utakuwa umeua ndege wawili kwa jiwe moja.
  1. Utaijengea CHADEMA heshima
  2. Utajijengea heshima kubwa zaidi
Kwa kuijengea CHADEMA heshima utakuwa umefuta kabisa dhana ile ya bila Mbowe hakuna CHADEMA hivyo kudhihirisha ukomavu wa CHADEMA kama chama chenye misingi imara.

Kwa kujijengea heshima utakuwa umedhihirisha ukomavu wako kidemokrasia kama mstaafu aliyeheshimu, kutetea na kulinda demokrasia kwa vitendo ndani na nje ya uongozi.

Ningependa kuwaona mmekaa pamoja wakati ukitangaza uamuzi wako huo na nakuhakikishia, utashangaa jinsi wananchi wengi wazalendo wakatavyoupokea uamuzi wako huo.

Erythrocyte, imhotep, Allen Kilewella, @elli, Retired, Fundi Mchundo, binti kiziwi nk, nini kimempata mwamba?

Busara zote hizi hazina maana yoyote kwake?
 
Back
Top Bottom