Hii ni JF, where we dare. Please educate me ikiwezekana hata inbox.
Mkuu check hapa, chagua ya kweli ja uwongo uyaache hapa hapa....
Mengine tuwlnaweza discuss private, ila midahalo karibu yote kwanini TL na sio FAM is more rhetorical than a reality na imejengwa kwenye chuki zaidi kuliko hali halisi .
👇
VIONGOZI WA SAUTI YA WATANZANIA WANAOPAMBANA KUITEKA CHADEMA!
Anaandika Jogoo wa Shamba
Nawaletea majina ya viongozi wa kikundi kinachoitwa Sauti ya Watanzania (SYW) ambao wamekuwa mstari wa mbele kupambana na kuhakikisha kuwa wanachukua uongozi ndani ya Chadema!
Watu hawa wako makundi matatu na ambayo hawajuani sana kiundani kwani wamekutana mtandaoni na ndio wanaosuka mkakati wa kuhakikisha wanaiteka Chadema!
Kuna ambao walijikuta wanaunga mkono kila kitu bila kujua madhumuni ya kikundi hiki, wapo watu wa mfumo na wapo wana mikakati wa CCM !
Nitaweka orodha na wasifu mfupi sana kwa leo ili watanzania mfahamu hawa watu na malengo yao!
Orodha ya Viongozi wa SAUTI YA WATANZANIA!
1.
Askofu Arthur Chilipwel - Mwenyekiti, muulizeni yeye na Kipilimba Wana uhusiano gani? Askofu huyu Kanisa lake na lile la Kipilimba yana uhusiano gani na yalianzishwa na nani? Kipilimba alikuwa Mkuu wa TISS (DGIS) wakati wa Magufuli,na ni Mchungaji Kanisa!
2.
Albini Saragu - Katibu mzaliwa wa Manyara, ndugu yake Dr.Slaa, alikuwa mhadhiri msaidizi UDSM elimu, ila alipopata fursa ya kwenda kusoma Uingereza akaamua kupotelea huko huko! Anafanya kazi maalum akiwa huko na ndio Katibu anayeratibu Kila jambo! Alipofika huko alivuruga Diaspora base ya Chadema yote, ndio maana hakuna anayehangaika naye arejee kwani kazi anaweza sana ya kuvuruga!
3.
Askofu Augustine Mpemba, huyu kafichama sana, atajitokeza mwenyewe baada ya kumtaja leo, ila aulizwe anasimamia Kanisa gani na pia anauhusiano gani na wenye mamlaka! Mtu hatari, anaogopwa sana kwenye mfumo kuliko Kipilimba!
4.
Askofu Mwanamapinduzi, huyu ni lile kundi lililoingia bila kujua liko upande gani na linafanya nini. Yupo Kanisa la Askofu Gwajima, na anasimamia Kibaha, huyu ni mwandani wa Gwajima na anapeleka taarifa zote kwake, anatokea Itilima, alishindwa Uchaguzi Itilima akagombea Kanda ya Pwani nako akashindwa!
5.
Dr. Wilbroad Slaa, - huyu mnamjua vyema, sihitaji kusema lolote ,ila jueni mission yake ni kuivuruga Chadema.
6.
Joseph Chacha, - Kijana wa mfumo ambaye anazungushwa Balozi mbalimbali Duniani, huyu huwa Afisa Mwambata na mara nyingine Afisa Itifaki, ameishi huko Duniani na watu hawamjui sana! Kijana kutoka Mara , anatimiza wajibu wake wa kulinda Dola na mambo yake! Amejitahidi kujipenyeza karibu na Lissu na kuaminika!
7.
Kaswahili Juma, - huyu Kijana wa Chadema, anatokea Magu, hajui kinachoendelea, ila ndio wale wako kwenye
_MRADI WA KUUA CHADEMA bila kujua nani wanawafadhili! Aliomba kwenda USA na alisaidiwa sana na Chadema, huko SYW Wanamuita reporter!
8.
Eliderick Kanyemela, - huyu ni reporter na hajui lolote! Anatumwa na Dr.Slaa kwani ni ndugu yake na Mushumbusi!
9.
Liberatus Mwang'ombe, huyu anatokea Mbarali, Yuko USA, huyu anafanya kazi ya mhudumu wa afya, yaani NESI ndio amekuwa mstari wa mbele kushambulia Chadema, huyu ni msaidizi maalum wa Peter Msigwa, alitumika sana kusambaza Fedha za Diaspora wakati wa uchaguzi wa Njombe na Kanda ya Nyasa! Chadema walifanya kosa kubwa sana kumuamini na alikuwa ndio kiungo kati yao na Congress ya Marekani! Walipokata mrija huo ndio ikawa vita yake na Chadema, aliwahi kushiriki vikao vya IDU, mrija ulipokatwa vita ikaanza! Chunguza yeye ni nani na Kapilimba alihusika vipi kumpeleka huko USA! Huyo ndio analipa vijana kama kina Gwamaka na wengine kufanya huo wajibu! Mfumo unamwelewa sana!
10.
Mpaluka Said aka Mdude - huyu mwanaharakati ambaye ameingizwa kwenye genge ambalo halijui! Alidhani yuko na wanaharakati, kumbe yuko na watu kazini waliotumwa na Mamlaka zinazomtesa kila siku ila alinufaika na kundi hili tangu wakati wa Maandamano na alikuwa analipwa gharama zote na kundi hili!
11.
Wakili Mwabukusi, huyu na Mdude hawana tofauti! Yuko Sasa TLS ila ana kampeni ya
"Mama Samia legal Aid" kashasahau habari za chapter four wala Mkataba wa Bandari na DP WORLD! Hasemi lolote kuhusu ahadi yake ya chapter four! Juzi kati kapokea new model Prado! Anasema hiyo ni project aliikuta! Haya arejeshe madaraka Kwa Sungusia! Huyu atakuwa TLS Kwa miaka 3! The longest serving president ever! Term limit ianze naye kwani wenzake wote walikuwa na kipindi cha mwaka mmoja!
12.
Alfa Zulu - tafuteni wasifu wake
13. Namourita Fayyene - tafuteni wasifu wake!
Naishia hapo kwa Leo!
©Jogoo wa Shamba