Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
#MWAMBA TUVUSHE
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wanalipwa teuzii
Khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee Waziri mkuu wa walevi wa konyagi.
IGP ni mmoja wa taasisi zilizo kwenye mpango wa kunajisi uchaguzi. Ccm ndio wana imani na IGP maana wanaweza kumtumia kulinda ushindi haramu.
Ndani ya chumba uchaguzi kuna mawakala wa vyama 16 Huyo mmoja tu sijui wa chadema nani ahangaike naye.Huyo anaongelea wasimamizi wa uchaguzi na anachosema ni ukweli mtupu
Kumbuka Chadema walifungiwa mikutano ya hadhara CCM ikawa peke yakeyaaani chadema ya 2015 nkiiangalia na hii video, inatia huruma sana
Kabla ya uchaguzi, mwanasiasa kazi yake ni kuomba kura.Mbowe amesema katika saa 72 zijazo Tundu Lissu atakuwa Rais wa Tanzania na Mimi nitakuwa Rais
Chanzo: Mwananchi online
==
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, amesema ndani ya saa 72 zijazo, mgombea wao wa Urais, Tundu Lissu anakwenda kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mbowe ametoa kauli hiyo leo Jumapili Oktoba 25 katika mji mdogo wa Bomang'ombe wilaya ya Hai wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni huku akisema Mungu akipenda, yeye anakwenda kuwa Waziri mkuu.
Hata hivyo, Mbowe ambaye pia anagombea ubunge jimbo la Hai, alitahadharisha kuwa kitendo chochote cha kuwazuia mawakala wao 80,160 nchi nzima wasiingie kwenye vituo vya kupigia kura Oktoba 28, kunaweza kubadili historia ya Tanzania.
Hivyo, aliisihi Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyombo vya Usalama, kuhakikisha hakuna jaribio lolote la kuwazuia mawakala wao kuingia kwenye vituo kusimamia upigaji kura na wao watakuwa tayari kukubali matokeo kama uchaguzi utakuwa wa huru na haki.
"Uchaguzi huu sio kati ya Chadema na CCM wala uchaguzi huu sio kati ya Lissu na Magufuli (mgombea urais wa CCM) bali ni kati ya wanaopenda uhuru na haki na waliokandamiza uhuru na demokrasia," alisema Mbowe.
Mbowe amesema wamezunguka mikoa yote ya Tanzania na wananchi wapo tayari kufanya mabadiliko ya uongozi na kusisitiza kuwa kwa mwonekano na hamasa waliyoionyesha Watanzania, Lissu anakwenda kuwa Rais ndani ya saa 72 zijazo.
Hivyo, ameitaka NEC kuhakikisha uchaguzi huu hauvurugwi kwa namna yoyote kwa sababu gharama yake itakuwa kubwa na kusisitiza kuwa wako tayari kukubali kushindwa kama NEC na vyombo vingine vitahakikisha uchaguzi umekuwa wa wazi, huru na haki.
Wanalipwa teuziiHivi mawakala ni walipwa shilingi ngapi kwa siku?
Ushindi ni sayansi na sayansi ni hesabu💥
Teuzi ni nyingi tunafyeka maDC,RC,DAS,RAS,RSO,mabalozi ,MaDED ,wakurugenzi wa mashirika ya umma,Wenyeviti wa taasisi za serikali nkKwahiyo CHADEMA mnampango wa kuwa na teuzi zaidi 80,000 kwa mawakala wenu tuu?
Ndio ma D.C. 😆😆
Kama hujayaona makosa imekula kwako. Nirekebishe bure bure tu? Lete hela. Nani alikuambia usome kayumba?Ebu rekebisha tuone
We jitie mjuai
Wewe na wagombea wako mnalindwa na nani?
Zamani sana hii, sikua hata naelewa vizuri maana uchaguzi ila ndio lilikua chimbuko la neno ngunguriMaalim Seif asema msimamo wake ni "JINO kwa JINO"