toriyama
JF-Expert Member
- Feb 18, 2014
- 1,139
- 2,223
Kizza Besigye alikuwa daktari binafsi wa M7. Uswahiba wa Uhuru na Ruto ulikuwa haukamatiki. Raila na ODM wakati ule ngoma inogile!
Ghafla bin vuu akaja Gachagua ndiye akawa bafa mkinga shari ili kumlinda na kumwinua Ruto.
Trump na Mike Pence walikuwa ni rais na makamu wake same as Joe na Kamala same as urafiki wa ENL & JK.
Haji Manara ulikuwa humwambii kitu kuhusu Simba. Na MO daima alihuzunikia mkwanja wake aliouwekeza Msimbazi!
Wema alikuwa kipenzi halisi cha Diamond. Dar ilikuwa makao makuu ya nchi. Juliasi na Sokoine walikuwa wazalendo wa Azimio la Arusha.
Nasari alikuwa shabiki kindakindani wa CDM. Na Waitara hakuisha kukinanga chama tawala kabla ya kutimkia huko kama Msigwa hivi karibuni.
Dkt. Slaa aliwahi kugombea urais chini ya CDM. Zitto Kabwe na CDM, CDM na Zitto Kabwe enzi hizoo!
Airtel ilikuwa Zain, Zain ilikuwa Celtel na Tigo imegeuka kuwa Yas. Elon Musk alikuwa Democrat, lakini sasa hivi yeye ndiye almost usukani, tairi na injini ya serikali ya Marekani!
Hivi unaweza kuamini kwamba kuna wakati hapo zamani ambapo Wapalestina na Waisraeli walikuwa wakiishi kwa amani na utulivu?
Juzi Anko Joni alikuwa rais, leo Sa100 ndiye fundi wa kuapisha viongozi wateule.
Must I continue?
Mhubiri 3:1-8
Mhubiri 3:1-8 Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake: Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa; wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa; wakati wa kuua na wakati wa kuponya; wakati | Biblia Habari Njema (BHN) | Pakua
Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake: Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa; wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa; wakati wa kuua na wakati wa kuponya; wakati
www.bible.com