View: https://www.youtube.com/watch?v=O6OAQjXmaXQ
Wapi hapa Mbowe kasema Lissu atachukuliwa hatua baada ya uchaguzi? Alichosema ni kuwa tatizo kubwa ndani ya Chadema ni ukosefu wa nidhamu. Ndio maana akasema uongozi utakaoingia itabidi uchukue hatua za kudhibiti hii hali bila kujali nafasi ya mhusika. Amesema hata kama yeye atashinda, Kamati Kuu mpya itakuwa na mamlaka ya kumchulia hatua kama itaona kuwa amehusika katika huo utovu wa nidhamu. Alipoulizwa kama atamchukulia hatua Lissu, alijibu kuwa huo utakuwa ni uamuzi wa Kamati Kuu na sio wa kwake. Hakusema mahali popote kuwa Lissu atachukuliwa hatua kwa sababu amemtukana. Huo ni uongo mtupu.
Amandla...