Wanaukumbi.
Halafu mtu anachukua form kukupinga Eti ni Demokrasia,hiyo siyo Demokrasia huo ni uchimbi kabisa, Lissu katumwa.
---
“Nimetoka mbali na Lissu. Nilikuwa ninamlipia Lissu tiketi za ndege ninamgharamia safari zake kwenda Tarime kuwatetea wachimbaji Wadogo. Wakati huo hakua hata Mwanachama wa CHADEMA na nilikuwa nina mfadhili kwa mfuko wangu”.
View attachment 3194365
Unajua kuna vitu unaweza ukawa unavitoa au kuviongea watu ukawa unajichoresha bila wewe mwenyewe kuelewa kama unajichoresha.
Kwa pamoja tutafakari mambo yafuatayo:-
Kauli ya Mbowe siku Lisu anachukua fomu ya kwamba naona ndani ya chama kuna fahari hii ni uhalo ambao ulimtoka bila kipima uzito wake, yaani kwamba yeye hatakiwi kushindana na mtu ndani ya chama kwa kuzingatia misingi ya kidemokrasia ambayo imekuwa kilo chake muda mrefu? Kauli hii inasadifu kwamba ameshajibadilisha na kuwa mmiliki wa chama na kwamba hakuna mwingine yeyote anaeruhusiwa kuwa mwenyekiti.
Sasa kama ndivyo kwa nini hata CHADEMA na vyama vingine visikae pembeni visiendelee kupambana na CCM kuitoa madarakani kwa dhana yako ya fahari wawili.
Chadema na vyama vingine vilipofikia sio tena mali ya mtu mmoja ni vyama vya watanzania/wananchi.
Haiwezekani unapokea luzuku ya chama tena ambayo huenda ingefanya mambo ya msingi kitaifa chini ya mfumo wa chama kimoja halafu leo unaleta ubabe wa kutaka kuonekana wewe tu ndo unafaa kuiongoza chadema, huu ni ujuha.
Nina imani unatambua kabisa kiasi cha watu walioumia wakipambania chama akiwemo Lisu, akina Mawazo, Ben, Mdude, n.k hivi unawezaje kukosa hata busara za kumpongeza Lisu kwa maamzi ya kugombea nafasi kubwa kama hiyo ndani ya chama chako, sio kwa sababu alipigwa, "hapana", ila ni kwa sababu anayo nia ya dhati kukupokea majukumu kama kaka au mlezi wake kama unavyosema kwamba umemtoa mbali, hukutoa watu mbali kuja kuwa mashuhuda bali kuwa wapambanaji hivyo Lisu hapaswi kuonekana kama mhaini kisa anagombea uenyekiti.