Mbowe usifanye kosa la kuachia Uenyekiti CHADEMA kabla ya 2030 vinginevyo tutarudi miaka ile myeusi (1995)

Mbowe usifanye kosa la kuachia Uenyekiti CHADEMA kabla ya 2030 vinginevyo tutarudi miaka ile myeusi (1995)

Sisi tanaangalia mzigo ufike panapohusika na sio hali ya punda! Tunakuomba sana mheshimiwa Freeman Mbowe kama unawapenda watanzania na CHADEMA usifanye kosa la kuachia uongozi wa chama kabla ya angalau 2030.

CHADEMA sio chama cha kuchukuliwa kiepesi epesi, CHADEMA ndio upinzani nchi hii na upinzani wa nchi hii ni CHADEMA. Siku CHADEMA ikifa ndio upinzani umekufa hivyo! Ikumbukwe kuwa kujenga chama imara kama CHADEMA huchukua si chini ya miaka 30.

Tafadhali sana mheshimiwa Mbowe, hatma ya upinzani na demokrasia ya nchi hii vipo mikononi mwako kuliko watu wengi wanavyojua. Hakuna kiongozi mwingine wa upinzani amebaki hai leo hii wote akina Lipumba, Mrema, Zitto, Cheyo, Shibuda, Mbatia na wengine, hao wote ni kundi moja, hawapo tena na hawana ushawishi kwa watanzania, umebaki wewe peke yako na unaangaliwa na watanzania kwa matumaini makubwa.

Siku utakapofanya kosa la kuachia uongozi wa CHADEMA kabla ya 2030, basi siasa za vyama vingi zitarudi zilipoanzia, 1995.

Usiangalie mashinikizo ya watu, kwanza wengi wa hao ni CCM wala si CHADEMA. Kumbuka wewe umetumwa kwa ajili ya Watanzania na wala hujajituma mwenyewe! Tafadhali subiri hadi 2030 na sio vinginevyo
Mbowe ni kigando aka gundi na king'ang'anizi chama ni cha mkwe wake amuachie nani ,huyu ni ruba kabisa
 
Eti apambane na CCM? Mmesahau kuwa mgombea toka ccm ndio aliwapa uhai cdm?mmesahau kuwa mzee alipata kura laki nane tu alipogombea Uraisi na hizo kura laki nane zaidi ya aslimia 90 alizipata toka Arusha na Kilimanjaro ?
Hizo takwimu alizitoa nani? wa wp? wa kabila lipi? watu wanasahau kuwa, kuna watu wanaishi na kuneemeka ktokana na hii katiba ilioitwa "kijitabu" ya 1977 ya chama 1. Woga wte wa Ktb mpya unatokana na yapatkanayo toka Ktb hiyo. Hawajui watakuwa wp katiba ikibadlishwa au pakiwa na mabadliko ya tume ya uchaguzi. Kula yao, nguvu zao, kelele zao zatokana na hicho "kijitabu". Wabadilishe waone ...nk
 
Mbowe ni kigando aka gundi na king'ang'anizi chama ni cha mkwe wake amuachie nani ,huyu ni ruba kabisa
Nilifikiri utaichukia CCM kwa jinsi walivyoshindwa kuondoa umaskini uliokithiri kwa miaka 60 sasa kumbe unamchukia Mbowe anayekupambania?!!
 
Haruhusiwi kubadilisha katiba.

Ama unakwepa kujibu hoja kwa makusudi.

Ama una tatizo la kuweza kufanya fikra za kidhahania.

Nakuuliza, ukipewa nafasi ya kurudi nyuma katika muda ukabadilishe kitu kimoja katika maisha yako, utabadilisha kitu gani?

Unanijibu kwamba, kurudi nyuma katika muda kwenye maisha yako ni kitu kisichowezekana.

Hujaelewa swali. Ama unalikwepa kwa hila tu.

CHADEMA inaamini katika kanuni ya kupishana uongozi? Au haiamini katika kanuni hiyo?
 
Mbowe, Aikael Freeman be humble Politics is a game of chance within the time framework. Unataka kuijiona wewe ndiye Siasa za Upinzani kimtazamo wa Kisiasa wewe ni Dictator leader becz you believe in yourself and not others. Unajiona Wewe ni bora kuliko Wengine kama umejiumba, Umejipa Afya, Umejipa akili, umejipa uhai, Umejipa Maisha wewe na Kwamba kile ulichojipa Wengine hawana Sidhani kama hiyo ni Demokrasia.
Mbowe toka Mwaka 2000 Wewe ni Mwenyekiti wa Chadema yaani walliozaliwa miaka 1999/2000 wote Wakiwa na umri wa miaka 24 sasa Watu Wazma lakini Bado Upo. Hizi Kitu kinachoitwa Siasa nyie mmekitafsirije Kwenye tasnia ya Siasa.
NB: Naamini Vijana Watalitafakari ili angalau Upishe Vijana Wenye Siasa zao. Yaani unazurula tu Maandamano Maandamano lakini Matokeo yake Ukitoka tu kila Mtu anakucheka. Maderva wa Bodaboda Wanajaziwa Mafuta na watu kugawiwa Elfu 10 ili kutengeneza sura ya Maandamano na wakitoka hapo Wanakucheka.
Ushauri kwako Mzee wa Gia angani umejitahidi Kwenye Siasa nakuomba tuachie ngazi na huyo Makamo wako Ambaye anallambalamba Midomo tu. Kwa Kipindi Mlichokaa kaeni Pembeni nyie na Tundu wako bakini Kwenye Ushauri Kwenye Baraza la Wazee wa Chama.
Tactically: Siasa zenu zinachekesha haxieleweki zina lengo gani. Mnaishi kwa Matukio kama vile Ugonjwa wa Kuhara unaojitokeza Kipindi cha mvua. Am tired to write ila mnaboa sana 😎😎😎😎
Pumba tupu.
 
Pumba tupu.
Kwanini ni Pumba tu! Nadhani Wewe ni Muumini wa Demokrasia je kuna Demokrasia ya kutobadilishana Madaraka kwa Vipindi au kuna Demokrasia ya Mtu kuongoza kama amefunga ndoa nacho tena ndoa ya Shida na raha ile ya Kikristo.
 
Nilifikiri utaichukia CCM kwa jinsi walivyoshindwa kuondoa umaskini uliokithiri kwa miaka 60 sasa kumbe unamchukia Mbowe anayekupambania?!!
Umasikini na masikini ni mentality hauondolewi na chama au serikali ,ndio maana ulaya kuna nchi ni masikini ,na kwenye nchi tajiri kuna masikini; umasikini unaondolewa na mtu binafsi,chukua hii itakusaidia wewe na kizazi chako mimi na kizazi changu tumevuka huko kulaumu watu,vitu serikali kwa matatizo binafsi.
 
1. Mtoto wa Rais wa kwanza ni Mkuu wa Mkoa. Mwingine aliwahi kuwa mbunge.
2. Mtoto wa Rais wa pili (aliyewahi kuwa Rais Zanzibar) alikuwa waziri na sasa ni Rais wa Zanzibar.
3. Mtoto wa Rais wa tatu ni Naibu Katibu Mkuu.
4. Mke wa Rais wa nne ni mbunge.
5. Mtoto wa Rais wa nne ni mbunge na waziri.
6. Mkwe wa Rais wa sita ni waziri.
7. Mtoto wa Rais wa sita ni mbunge.
Nasikia kuna waziri au Katibu Mkuu alikuwa ana ujamaa na Rais wa tano. Na hivi karibuni katika uchaguzi wa viongozi wa chipukizi tulisikia majina yale yale.

Endelea tuu kusubiri embe chini ya mnazi.

Amandla...
Naona ni afadhali kwa maana ni mchanganyiko wa makabila ,nyie cdm hadi viongozi wa mikoa ambayo sio ya uchaggani mmeweka viongozi wachagga,mnatia aibu aisee
 
Wewe bwege sana yaan niue niwe naandika hapa?

Nakuambia tena Mbowe Hana Muda mrefu hapo Cdm ataondoka naturally kama wengine

Mbowe sura tu inaonyesha kachoka kimwili, kiakili

Akalee wajukuu huko Nshara
Mzee Mbowe hawezi kuachia chadema labda nguvu itumike tu.
 
Umasikini na masikini ni mentality hauondolewi na chama au serikali ,ndio maana ulaya kuna nchi ni masikini ,na kwenye nchi tajiri kuna masikini; umasikini unaondolewa na mtu binafsi,chukua hii itakusaidia wewe na kizazi chako mimi na kizazi changu tumevuka huko kulaumu watu,vitu serikali kwa matatizo binafsi.
Ndio kila mtu binafsi anapaswa kuchangia kuondokana na umaskini wake, ila usisahau kuwa lazima mifumo mizuri iwekwe ili mtu aondokane na umaskini. Ulaya, America, Asia, nk umaskini umeondoka kwa kiasi kikubwa pia ni kwasababu ya mipango mizuri ya serikali. Watu binafsi hawawezi kujenga barabara, na miundombinu mingine mingi kuwaondoa kwenye umaskini. Sijui kwanini watanzania bado mnapenda kubaki na ccm hata baada ya miaka 60. Hii inaonesha jinsi mlivyo na akili mgando.
 
Naona ni afadhali kwa maana ni mchanganyiko wa makabila ,nyie cdm hadi viongozi wa mikoa ambayo sio ya uchaggani mmeweka viongozi wachagga,mnatia aibu aisee
Nashukuru kwa kunifahamisha kuwa Lissu, Heche, Sharifa Suleiman, Ruge, Mwalimu, Mnyika wote ni wachaga. Na wakristu.

Amandla...
 
Nashukuru kwa kunifahamisha kuwa Lissu, Heche, Sharifa Suleiman, Ruge, Mwalimu, Mnyika wote ni wachaga. Na wakristu.

Amandla...
Hao uliotaja ni mateka wa mzee mbowe na ndio wanaotumika kuonyesha kuwa cdm hakuna ukabila ,SHAME
 
Nashukuru kwa kunifahamisha kuwa Lissu, Heche, Sharifa Suleiman, Ruge, Mwalimu, Mnyika wote ni wachaga. Na wakristu.

Amandla...
Hivyo huna taarifa kuwa mnyika ni mpare kwa malezi kwa maana kakulia kwa mama kule upareni,manalazamisha awe msukuma labda kwa asili (baba yake ) ila hata siku moja hakuwahi kwenda mwanza kwa huo aliekuwa baba yake.
 
Hivyo huna taarifa kuwa mnyika ni mpare kwa malezi kwa maana kakulia kwa mama kule upareni,manalazamisha awe msukuma labda kwa asili (baba yake ) ila hata siku moja hakuwahi kwenda mwanza kwa huo aliekuwa baba yake.
Mnyika ni mpare

Ni Siri nzito sana

Hivi kapona umirembe??
 
Back
Top Bottom