Mbowe: Utawala wa Magufuli uliwatesa sana watu wa Kilimanjaro na Arusha!

Mbowe: Utawala wa Magufuli uliwatesa sana watu wa Kilimanjaro na Arusha!

Wewe wana ukabila acha

Chadema Zanzibar waliweka mbunge viti maalumu mchaga hebu fikiria Zanzibar ambako Chadema hata mjumbe wa nyumba Kumi hawana mbunge viti maalumu wakaweka mchaga

..Wachaga wapo mpaka Kenya.

..ipo siku mtasikia Mchaga kawa mbunge wa Kisumu, Kitale,...

Cc MK254
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
nyie kwavile mliekewa runway muanikie mpunga hamuwezi kuliona hilo
 
MoseKing,

..Mchaga askari wa Marekani.

..wao maisha na kazi ni popote pale.


Vipi wala sio hoja huyo! Hata Obama wajaruo walidanganyana ni mkenya mwisho wa siku hakuna alichovuna! Best kila kabila linawatu kibao wako nje ya nchi kadanganye mataahira huko!
 
Vipi wala sio hoja huyo! Hata Obama wajaruo walidanganyana ni mkenya mwisho wa siku hakuna alichovuna! Best kila kabila linawatu kibao wako nje ya nchi kadanganye mataahira huko!

..nendeni basi mkawazibie na ktk jeshi la mmarekani.🤣🤣
 
..Zanzibar wakati wa Karume waliwahi kuwa na mkuu wa polisi [ edington kissasi] ana asili ya Uchagani. Je, hiyo nayo utasema ni ukabila?

..Kukusaidia tu, Wachaga ni kati ya makabila ya kwanza kutoka ktk maeneo yao ya asili na kusambaa Tanzania nzima kutafuta fursa.

..Sijui kama unamkumbuka Waziri mmoja mwanamama akiitwa Shamsa Selengia Mwangunga. Yule mama asili yake ni Uchagani, wazazi wake walilowea Dodoma na siasa alikuwa akifanyia huko.

..Mtanzania kama huyo unaweza vipi kumbagua asishiriki siasa ktk eneo alilokulia? Na ukimbagua kwenye siasa utaishia hapo au utambagua ktk fursa nyingine?

..Mwisho, Wachaga hawachagui mahali pa kuishi. Wachaga hawajitengi. Pia ni wameoleana na jamii nyingi hapa nchini. Huo ndio UTANZANIA.
Basi itakuwa ni coincidence, popote pale alipo mchagga ataunganishwa na kupewa nafasi ndani ya CHADEMA.

Hiki Ni kitu cha kipekee sana ambacho huwezi kukikuta uchaggani.
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
Nini Hujuwi na nn unajuwa?
 
Kuna watu wanadhani wakiendelea kumtuhumu JPM itawafanya wakubalike tena kumbe sivyo. Inaonekana JPM hawezi kusahaulika kiraisi na ataendelea kuwatesa watu wengi sana.
Tatizo Mbowe na Chadema sera hawana Mbowe hajui siasa nini anadhani ni personal attacks!!
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
Magufuli alikuwa mbaguzi kweli. Ushahidi huu hapa

1749052_mwananchi.jpg
 
Basi itakuwa ni coincidence, popote pale alipo mchagga ataunganishwa na kupewa nafasi ndani ya CHADEMA.

Hiki Ni kitu cha kipekee sana ambacho huwezi kukikuta uchaggani.

..kuna mfano wa Shamsa Mwangunga na Asseri kwa upande wa CCM.

..halafu kuna mfano wa Devota Minja kwa upande wa Chadema.

..sasa kwanini unakerwa na Wachaga walioko Chadema, huwaoni hao walioko Ccm?

..kuna wakati Makamu wa mwenyekiti, Katibu Mkuu, na Naibu Katibu mkuu, wa Chadema walikuwa Wasukuma. Je, ina maana Chadema ilikuwa chama cha kikabila cha Wasukuma?

..Binafsi nadhani tuwe macho na hila na propaganda za Ccm.

..Chadema sio chama cha kwanza cha upinzani kutuhumiwa na Ccm kwamba kina ukabila au udini.

..Cuf ilipoonekana kwamba ni tishio kwa Ccm kilituhumiwa kuwa chama cha Waislamu.


..Udp ilipoanzishwa na John Cheyo alipoonekana ni tishio chama chake kikapakaziwa kuwa ni cha Wasukuma.

..Kwa hiyo tuwe macho na propaganda za Ccm kuchonganisha jamii moja dhidi ya nyingine.
 
Back
Top Bottom