Mbunge: Kwanini mwananchi akileta TV Bara kutoka Zanzibar analipia kodi wakati nchi ni moja?

Mbunge: Kwanini mwananchi akileta TV Bara kutoka Zanzibar analipia kodi wakati nchi ni moja?

Haiwezekani mwananchi amesafiri kutoka Zanzibar na TV moja used anakuja kutumia nyumbani anafika Bara anaambiwa alipe kodi na hii ni nchi moja, akini anayetoka Morogoro kwenda Dar halipi kodi, lakini anayetoka Zanzibar kuja Bara alipe kodi, hii ni kero kubwa,"- Bakar Hamad


Zanzibar kama haitaki kodi basi iweke kodi sawa na Bara bila hivyo itakuwa kichochoro. Anaye uliza swali naye ajibu swali kwanini Zanzibar ina kodi tofauti wakati ni nchi mmoja?
 
Mkuu kwa hilo nalikataa,mimi karibu kila mwezi lazima niende unguja narudi na sukari kilo tano,cjawahi hata kuulizwa na mtu.Ila kwa sasa imepanda hadi 12500-13000 ,toka 10,000 ,Hata haina haja tena ya kununua huko.Labda kama ni zaidi ya kilo 5!!ila kwa kilo tano.HAPANA.
mijitu mingi nchi hii ni wazushi, sijui wana matatizo gani, wana mapepo. Watu gani mioyo yao haina amani muda wote? Lazima wamzushie mtu, wamfitini mtu ndiyo roho zao zitafurahi.
 
Zanzibar Kuna raisi pale, hivyo Ile ni nchi.. ukileta bidhaa huku bara, tayari unakuwa umeingiza kwenye nchi nyingine ambayo ni Tanzania
Tanzania tena? Nadhani ungesema Tanganyika
 
Wakisema waache kutoza Kodi Italeta mianya ya ukwepaji Kodi , kwamba hata wamalawi watapitisha mizigo Zanzibar wakisingizia umetoka Zanzibar kumbe la
Kodi iwe ile ile bara na visiwani
 
Mkuu kwa hilo nalikataa,mimi karibu kila mwezi lazima niende unguja narudi na sukari kilo tano,cjawahi hata kuulizwa na mtu.Ila kwa sasa imepanda hadi 12500-13000 ,toka 10,000 ,Hata haina haja tena ya kununua huko.Labda kama ni zaidi ya kilo 5!!ila kwa kilo tano.HAPANA.
We jamaa mbishi.. Kwa hyo mtu unayekutana naye,ndo na yeye alikutana naye..usiwe mbishi mbishi yawkana we ni alwatan kwa Hizo Safari.. binti ni mgenigeni so wakaamua kufanya hivyoo
 
Haiwezekani mwananchi amesafiri kutoka Zanzibar na TV moja used anakuja kutumia nyumbani anafika Bara anaambiwa alipe kodi na hii ni nchi moja, akini anayetoka Morogoro kwenda Dar halipi kodi, lakini anayetoka Zanzibar kuja Bara alipe kodi, hii ni kero kubwa,"- Bakar Hamad

Lakini ndizi zikitoka bara kwenda Zanzibar hazitakiwa maana wazanzibar wa ndizi nyingi sana na hata kama hazitatosha basi hizo ni fursa za wazanzibar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mambo mengine hufanyika kwa sababu ya kukariri, uwezo mdogo wa kupambanua na kudhibiti hali kwa akili ya kawaida tu.

Vitu vya matumizi ya mtu mmoja mmoja haviathiri kodi kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na faida ya kisiasa na umoja wa kitaifa kivitendo.
KAma waziri anafika kuwa mashahidi kwenye tukio la tenga la ndizi, kuna kitu hapo?, sie tulioko mipakani huku bara vitu vidogo vidogo hata kama wanaenda kuuza TRA wanaachia tu wananchi wakakuze uchumi wao
 
Haiwezekani mwananchi amesafiri kutoka Zanzibar na TV moja used anakuja kutumia nyumbani anafika Bara anaambiwa alipe kodi na hii ni nchi moja, akini anayetoka Morogoro kwenda Dar halipi kodi, lakini anayetoka Zanzibar kuja Bara alipe kodi, hii ni kero kubwa,"- Bakar Hamad

Tanzania kama walivyo watanzania.. brains are too sloooow..
 
Kwa hiyo wabara tumekuwa wakupeleka magonjwa Zanzibar[emoji17][emoji17]
20230205_094758.jpg
 
Kero haipo Zanzibar,ukienda zanzibar huulizwi kitu,ukirudi huku Kwa wachaga unakomeshwa.Ila Kwa vile una chuki imekujaa upumbavu umekufanya mpofu.
Wachaga watakuwa wanakutafuna si bure.
Unawezaje kutoka Zanzibar Ukaingia kwa Wachaga
 
We jamaa mbishi.. Kwa hyo mtu unayekutana naye,ndo na yeye alikutana naye..usiwe mbishi mbishi yawkana we ni alwatan kwa Hizo Safari.. binti ni mgenigeni so wakaamua kufanya hivyoo
Hakuna inshu ya mgeni ama mzoefu,utaratibu ni ule ule tu kwa kilo 5 za sukari hakuna hata kuulizwa!!!kwani watu wahabebi kwa kificho,utakuta kwenye boti moja zaidi ya watu 30 wamebeba sukari,na mkifika hapo bandarini Dar,kwenye kupitisha mizigo kwenye scanners,kama hujaiweka kwenye mfuko mwingine zaidi ya ule uliyoinunulia,unapita tu.
 
Yaani mpaka leo mtu anaagiza TV zanzibar!?kwamba huku hamna?au bei?kwa tofauti gani
Hapana mkuu kwa vifaa vya electronics kule kuna unafuu sana!!pamoja na kulipia gharama za usafiri na kodi,tv ya nchi 49, brand new,unaweza save hata laki 2!!kulinganisha na ukinunua hapa dar.
 
Wachaga watakuwa wanakutafuna si bure.
Unawezaje kutoka Zanzibar Ukaingia kwa Wachaga
Ndiyo mwisho wa matusi yako?naomba utukane matusi mengine kumi mazito unayoyaweza Kisha Mimi nikutumane Moja uone nani arakayepigwa ban.
Ukishindwa nakuja kutuana Mimi.
 
Wazanzibar huwa hawana sudi na kero za wabara wanaoenda huko bali wao wanatoa kero zao na kutaka wanufaike zaidi na Muungano.

Mbara nenda kanunue plot huko zenji uone shuruba yake. Lakini wao wanamiliki mashamba na vilima bara
Wao kero kubwa wanayo ilalamikia ni kuhusu gari yenye plate number za zanzibar,kutotambulika bara!!! traffic police wakikuona una gari lenye namba za usajiri za zanzibar ni kosa,wanakwambia kama unataka litumike bara,kabadirishe!!wanajua kabisa kuwa kule magari ni bei nafuu hivyo watu wangetumia mwanya huo kuingiza magari bara,.
 
Kero ni Mzanzibari, kisiwa chenye idadi ya watu milioni 1, kuongoza Bara kwenye watu millioni 60. Tuanzie hapo kwanza.
Ila nyie wabara ni mambumbu,mngekaacha huru kazenji haya yote yasingetokea....tatizo ni kukang'ang'ania.
 
Zanzibar VAT ni 15% wakati bara VAT ni 18% .... ukileta kitu bara hiyo 3% ndo inakatwa ili kuweka uwiano sawaaa uwe umelipa 18% kama bidhaa nyingine
 
Wakisema waache kutoza Kodi Italeta mianya ya ukwepaji Kodi , kwamba hata wamalawi watapitisha mizigo Zanzibar wakisingizia umetoka Zanzibar kumbe la
Wamalawi watakatwa kodi huko huko zenje....wakifika bara wanapita tu kama ni nchi moja.

La sivyo hakuna muungano ni porojo tu na danganya toto.
 
Back
Top Bottom