Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Asante ndugu yangu kwa kuliona hilo. Hawa viongozi wa Bunge kwa kweli wajipimeBunge la Tanzania halafu ndani ya Bunge hilo yupo mbunge ambaye anakana wazi wazi kuwa yeye siyo raia wa Tanzania. Na hii taarifa inaingia kwenye hansard. Na hao viongozi wa nchi wanamchekea tu huyu bwege. Hii ni hatari
Tunaelekea kwenye "state of anarchyc wallah
Alichokana ni ile taarifa ya Kunambi wala siyo Utanzania wakeSasa Mbona anakana? rejea masharti ya kuwemo humon ndani ya Bunge
Unafiki ndio unawasumbua,Mbona Viongozi karibu wote humu Tanganyika kasoro Judge Warioba Hawataitaki, hili unalizungumziaje ndugu yangu? Viongozi wa Tanganyika hawatoshi.
Hapo unamuonea Tulia!Kiti ni kiti tu haijalishi anayekikalia, kama ni cha speaker, yeyote anayekikalia naye pia ni speaker aka Subwoofer. Hivyo madhara yake yatamkumba hata kama si speaker.
Wote humo ndani ni raia wa Tanzania na wanaapa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili wapate haki ya kukaa humo ukumbini.View attachment 2991526
Mbunge anasema na au anakana kwamba yeye si Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania “Mtanzania”.
Sasa Humo Bungeni anafanya nini?
Hatuna Nchi inayoitwa Zanzibar wala nchi ya Tanganyika. Tuna Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “ Tanzania”
Sasa kama yeye ni Mzanzibar na hatuna nchi hiyo, humo ndani kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anafanya nini? Kiti cha Speaker kingefaa kimtoe nje pale pale kwa kauli yake mwenyewe kwamba hapokei taarifa ya yeye ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kiti cha Speaker mumepwaya sana maana, Hatuna dual nationality, tuna Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mtu anasema na anakana kwamba yeye sio Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ( Principle of legal estoppel), sasa kwa nini aendelee kuwemo humo Bungeni?
Hatuna dual nationality, hakuna raia wa Burundi, Rwanda au nchi ya “Zanzibar” anayeweza kuwemo Humo Bungeni.
Ni Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pekee anayeweza kukaa humo, vinginevyo ni magumashi tu, bila chenga chenga na mkosi ni Mkosi tu- Haijalishi unatokea wapi.
Povu ruksa bila Matusi.
Huo ndio uongo tulioaminishwa na hawa waliotufungisha ndoa ya mkeka. Kumbe ni uongo wa hali juu. NO THREAT.Mtu anakuja kutamba kwenye ardhi yetu? Arudi akale urojo. Viongozi wa kitanganyika wanakwama wapi? Ni kweli zanzibar ikiachwa itakuwa threat kwetu?
Kulikuwa kuna kadingi fulani bungeni, sijui kabunge kaCCM kule Nkasi, kalikuwa kanalipukaga balaa wazenji tukianza kufungua midomo bungeni kuhusu huu muungano.
Kale kadingi kangekuwepo leo hapo bungeni pasingekalika.
Mbona amekana na speaker akakaa kimya?Wote humo ndani ni raia wa Tanzania na wanaapa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili wapate haki ya kukaa humo ukumbini.
Hayo mengine yote ni muendelezo tu na matakwa ya demokrasia kwa mapana yake.