Mbunge Saashisha Mafue adaiwa kuwalipa vijana walioajiriwa kazi ya muda ya Postkodi Tsh. 15,000 kwa siku mkataba wa siku 15

Mbunge Saashisha Mafue adaiwa kuwalipa vijana walioajiriwa kazi ya muda ya Postkodi Tsh. 15,000 kwa siku mkataba wa siku 15

Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia.

Kituko cha pili Mbunge huyo Amewaambia vijana hao kuwa ajira hiyo ni ya muda wa siku 15 badala ya siku 45 kama ilivyoainishwa na serikali ili zoezi lifanyike kwa Uangalifu na kwa umakini mkubwa.

Vijana hao wameamua kufanya kazi hiyo bila ufanisi kutokana na kulipwa malipo tofauti na mpango wa serikali, ila siku ya jumamosi tarehe 19.3.2022 wataandamana kumpokea mwenyekiti wa chadema Taifa ambaye atahutubia Jimbo la Hai mjini ikiwa ni mara ya kwanza tangu atoke gerezani na watafikisha kilio hicho mbele yake kwa mabango.

Mkuu wa Wilaya ya Hai alivyotafutwa kuzungimzia malipo hayo na siku za kufanya kazi hakutaka kusema chochote bali alisema hausiki na zoezi hilo na hakushirikishwa .

Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Hai , Dionis Myinga alivyotwafutwa ofisini kwake palikuwa pamefungwa .​

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, tulivyompigia simu ,kumuuliza kuhusu stahiki ya malipo kwa hao vijana wanaofanya kazi kwa mkataba, kwa kila siku na muda wa kazi hadi kumalizika alisema yuko kwenye kikao.

Vijana hao wanakiomba Chama cha mapinduzi ngazi ya wilaya ,mkoa,Taifa kuingilia kati hatima ya malipo yao na siku za kufanya kazi hiyo kama ilivyopangwa na serikali ya CCM. Vijana wamekata tamaa iliyosababishwa na mtu mmoja au kikundi cha watu.​

 
Siasa zimelemaza akili za waTanzania na kufifisha uwezo wa UBONGO kutafakari......

Watanzania imefikia hatua ya kubeba jambo linalotendwa na mpinzani wako kisiasa linaloonekana kubeba kisiasa pasi na kulichambua au kulipembua kiuyakinifu......

Wanasiasa wamevifanya vichwa vya waTanznia kuwa mabox ya kuhifadhia matamko, maneno na ajenda zao na sio chem chem ya tafakuri......
 
Aisee JF imevamiwa kwa kweli. Hata kama ni propaganda za kisiasa hizi ni za hovyo kabisa kwani zinaonekana zimebeba chuki binafsi kwa mbunge wa Hai kitu ambacho ni hatari sana kwa ustawi wa taifa na amani ya taifa hili. Nao hao vijana waliopewa kazi ya kuweka anwani za makazi wanapaswa watimuliwe mara moja kwa sababu kama tu hawamjui mwajiri wao sahihi ni halmashauri na sio mbunge wataweza vipi kuifanya hiyo kazi kwa usahihi? Mbunge na anwani za makazi wapi na wapi?

Huyu aliyeleta madai yao hapa ndio anaonekana mwelewa kuliko wenzake lakini ni kilaza kiasi hiki sasa hao waliopo huku "field" si ndio balaa kabisa. Watu wanajaribu kumwelewesha hapa mbunge hahusiki lakini wapi anakomaa mwanzo mwisho eti wao wameelezwa mwajiri wao ni mbunge. Halafu eti madai yao watapeleka kwa Mbowe siku akifika Hai. Kwa ninavyomjua Mbowe ni kuwa ameshavuka mbali sana siasa hizi za ovyo ovyo za kuchafuana na kujengeana chuki zisizo za msingi.

Mleta mada pamoja na wenzako pelekeni madai yanu kwa siri kwa mkurugenzi wa halmashauri wa wilaya ya Hai. Ikishindikana nendeni kwa Mkuu wa wilaya Hai, takukuru Hai, au takukuru mkoa wa Kilimanjaro kote huko utapokelewa vizuri na taarifa zako zitafanyiwa kazi kwa siri tena kwa haraka sana. Hapo inaonekana kuna watu wameshafanya yao halafu wanamtupia jumba bovu mbunge ambaye hahusiki kwa namna yote ile labda kwenye uhamasishaji tu.
 
Aisee JF imevamiwa kwa kweli. Hata kama ni propaganda za kisiasa hizi ni za hovyo kabisa kwani zinaonekana zimebeba chuki binafsi kwa mbunge wa Hai kitu ambacho ni hatari sana kwa ustawi wa taifa na amani ya taifa hili. Nao hao vijana waliopewa kazi ya kuweka anwani za makazi wanapaswa watimuliwe mara moja kwa sababu kama tu hawamjui mwajiri wao sahihi ni halmashauri na sio mbunge wataweza vipi kuifanya hiyo kazi kwa usahihi? Mbunge na anwani za makazi wapi na wapi?

Huyu aliyeleta madai yao hapa ndio anaonekana mwelewa kuliko wenzake lakini ni kilaza kiasi hiki sasa hao waliopo huku "field" si ndio balaa kabisa. Watu wanajaribu kumwelewesha hapa mbunge hahusiki lakini wapi anakomaa mwanzo mwisho eti wao wameelezwa mwajiri wao ni mbunge. Halafu eti madai yao watapeleka kwa Mbowe siku akifika Hai. Kwa ninavyomjua Mbowe ni kuwa ameshavuka mbali sana siasa hizi za ovyo ovyo za kuchafuana na kujengeana chuki zisizo za msingi.

Mleta mada pamoja na wenzako pelekeni madai yanu kwa siri kwa mkurugenzi wa halmashauri wa wilaya ya Hai. Ikishindikana nendeni kwa Mkuu wa wilaya Hai, takukuru Hai, au takukuru mkoa wa Kilimanjaro kote huko utapokelewa vizuri na taarifa zako zitafanyiwa kazi kwa siri tena kwa haraka sana. Hapo inaonekana kuna watu wameshafanya yao halafu wanamtupia jumba bovu mbunge ambaye hahusiki kwa namna yote ile labda kwenye uhamasishaji tu.
Mleta mada pamoja na wenzako pelekeni madai yanu kwa siri kwa mkurugenzi wa halmashauri wa wilaya ya Hai.(Siri)
 
Tatizo ni jimbo lililotajwa,ametoka mahabusu anataka akabidhiwe jimbo Kwa msamaha wa Rais.
 
Hizi pesa huenda baadhi ya halmashauri zinaiba hizi pesa.


Kwanini kuwe na utofauti wa malipo wa hizi pesa?

Kwanini baadhi ya halmashauri ziweke wazi malipo yatakuwa ya sh. 30000 kwa siku huku zingine zishindwe kutangaza kiasi watakacholipa na idadi ya siku?

Taasisi za usalama wa Taifa zifuatilie hili na zipelekwe taarifa kwa amri jeshi mkuu kwa hatua zaidi kwa. halmashauri zote zinazotaka kukwamisha zoezi hili la postkodi
.

Ila mleta mada Mbunge hahusiki na kuajili au kuwalipa hao vijana.Mhusika mkuu ni mkurugenzi wa halmashauri.
Kila halmashaur Ina Muundo wake so ni vile walivyokubaliana kufanya Kazi. Mf Kuna halmashaur imeona itangaze nafasi nyingi Kwa malipo kidogo Ili Kazi imalizike mapema... Pengine 10000 Kwa siku lakn wametoa Ajira Kwa watu 400. Wengine wametangaza nafasi chache ila watachukua siku nyingi zaidi pengine watu 150 ila watalipwa 30000.
 
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mafue anadaiwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya Rais Samia.

Pili, Mbunge huyo anadaiwa amewaambia vijana hao kuwa ajira hiyo ni ya muda wa siku 15 badala ya siku 45 kama ilivyoainishwa na serikali ili zoezi lifanyike kwa Uangalifu na kwa umakini mkubwa.

Vijana hao wameamua kufanya kazi hiyo bila ufanisi kutokana na kulipwa malipo tofauti na mpango wa serikali, ila siku ya jumamosi tarehe 19.3.2022 wataandamana kumpokea mwenyekiti wa chadema Taifa ambaye atahutubia Jimbo la Hai mjini ikiwa ni mara ya kwanza tangu atoke gerezani na watafikisha kilio hicho mbele yake kwa mabango.

Mkuu wa Wilaya ya Hai alivyotafutwa kuzungimzia malipo hayo na siku za kufanya kazi hakutaka kusema chochote bali alisema hausiki na zoezi hilo na hakushirikishwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Hai , Dionis Myinga alivyotwafutwa ofisini kwake palikuwa pamefungwa.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, tulivyompigia simu ,kumuuliza kuhusu stahiki ya malipo kwa hao vijana wanaofanya kazi kwa mkataba, kwa kila siku na muda wa kazi hadi kumalizika alisema yuko kwenye kikao.

Vijana hao wanakiomba Chama cha mapinduzi ngazi ya wilaya, mkoa, Taifa kuingilia kati hatima ya malipo yao na siku za kufanya kazi hiyo kama ilivyopangwa na serikali ya CCM. Vijana wamekata tamaa iliyosababishwa na mtu mmoja au kikundi cha watu.
Nilishakukataza kutoa taarifa za umbea humu, tangu lini Mbunge akahusika na malipo kwa wafanyakazi wenye ajira za Halmashauri?
 
Back
Top Bottom