Tetesi: Mbunge wa Arusha Mjini pamoja na Meya wasakwa na Jeshi la Polisi

Tetesi: Mbunge wa Arusha Mjini pamoja na Meya wasakwa na Jeshi la Polisi


Shida hapo ugomvi wao hawa wawili unachochewa na mkulu na ndio tatizo kubwa ktk mkoa huo

Inasikitisha kuona Rais mzima kukosa busara ya kuingilia kati mgogoro huu wa kipuuzi unaosababishwa na Mteule wake Gambo!
Mimi kwa kumheshimu Rais JPM napenda kumpa ushauri wa bure na sihitaji hata ukuu wa Wilaya au Mkoa! Kwamba: KWA HALI INAYOENDELEA ARUSHA KATI YA MBUNGE LEMA(Chaguo la Wananchi)na RC GAMBO(Chaguo la Rais) LAZIMA RAIS AIDHA AMUHAMISHE MTEULE WAKE GAMBO AU AMFUKUZE KAZI! Rais Magu asitegemee chembe ya maendeleo jijini Arusha kwa hali hii!Kwa vile Lema ni Mbunge wa kuchaguliwa na Wananchi Rais hana mamlaka ya kumwondosha ila kwa Gambo anaweza!
Kama Rais JPM hawezi kuchukua ushauri huu wa bure basi kuna hatari ya kuanza kuwatengeneza kina Mwamwindi wa Arusha na huyu Gambo ni mwanadamu kama wengine na huenda yaka mtokea kama yaliyomtokea Dr.Kleruu(RIP) enzi za uhai wake! It' s just a matter of time!
 
Japo mara nyingi huwa ushauri haufuatwi lakini nadhani ka ccm haitaki kujifuta yenyewe Arusha na sehemu nyinginezo Tz wateule wa rais waliopelekwa huko waende kuitengeneza ccm iliyo kwisha haribika sana machoni mwa Watz.
Picha mbaya haiondolewi kwa matendo mabaya. Wateule wa rais, hebu onesheni mambo mema saana ya ccm. Heshima, utu, na haki kwa kila mtu bila ubaguzi.
Mh Gambo, twajua kuwa una imani kuwa Chadema hawawezi lolote, sasa, tafuta mbinu ya kuonesha zaidi makubwa ya ccm. Hospitali ziongezewe uwezo, barabara zipanuliwe vizuri, projects zinazofanyika Ar sasa hivi uzisimamie zionekane kweli ni bora. Achana na kushindana kimwili na Lema, shindana naye kwa kuonesha mema ya ccm.
Kamata kamata ni kumwongezea umaarufu Lema &Co. Sikio la kufa halisikii dawa. Usiwe sikio la kufa Gambo.
Mkuu hayo ni matokeo ya elimu pasipo elimu. Sifa ya uteuzi ikiwa ni kujivika ujinga ili mradi chama dola mbele kwa mbele ndiyo matokeo yake. Bado miaka minne tutaisona namba
 
Nyie ndio hamnazo kabisa. Hata kama lema angechaguliwa na kura asilimia mia ya watu wa arusha bado yuko chini ya mamlaka ya serikali kuu inayowakilishwa na rc na dc. Chadema lazima watambue serikali kuu inaongozwa na ccm. Maneno ya kumkejeli rais au kumtakia balaa kama alivyofanya lema juzi yanaonyesha jinsi lema asivyokua na busara na alivyokua mtu wa shari.
Mbona kejeli za rais hazikukeri? Usisahau sheria ya maisha kuwa kila mtenda hutendwa
 
Lema akamatwe na afunguliwe mashitaka kwa kauli inayoashiria kutaka kumuua rais kwa kisingizio cha Mungu kumbe wao chadema ndiyo wanapanga na wanajiumbua kwa kauli zao tatanishi
 
Mm nashauri itafutwe njia ya wawili hao Lema na Gambo wakae na kuzika tofauti zao na kila kiongozi afanye majukumu yake bila kuingilia majum ya mwingine tunataka arusha isonge mbele kimaendeleo bila malumbano ya viongozi wa kuchaguliwa na kuteuliwa
Haiwezekani kwa mamlaka zao za kazi zao zinasimamiwa kitofauti.

Mimi naamini Lema analegezea kamba huyu mgambo, ila cha moto kinampata mgambo.
 
Ubaya ni kwamba labda wabadilishe sheria mbunge awe miaka kumi tuu, la sivyo lema is there to stay miaka Mia 8, Gambo hawezi kukaa hapo hata miaka mitano
 
Lema akamatwe na afunguliwe mashitaka kwa kauli inayoashiria kutaka kumuua rais kwa kisingizio cha Mungu kumbe wao chadema ndiyo wanapanga na wanajiumbua kwa kauli zao tatanishi
Hamjiamini? Fungueni mashtaka maana hamna aibu ya kushindwa.
 
Kwa taarifa yenu kuna mpango mkakati wa kuhakikisha kuwa jiji la Arusha linadhohofishwa na "rire lijiji retu kure kwetu" kupandishwa chati...

Kuna kamati maalum imeundwa kufanikisha zoezi hilo...
Wataanza na vurugu ili wazoroteshe sekta ya utalii Arusha.
Kilele kitakuwa ufunguzi wa viwanja vikubwa vya ndege Mwanza (Serengeti Intl. Airport) na Chato (Rubondo Intl. Airport)..

Wao wanasema ware jamaa wamekura sana sasa ni zamu yetu..!!
Mimi humu ni mjumbe tu kuwafikishieni hizi dondoo...
nimeanza kupata idea
 
Nahisi wewe ndo Lema mwenyewe na kama siyo basi wewe unaweza kua unawatetea watu bila kuwajua,mtu hawezi nyanyuka tu bila sababu eti akaenda kuliamulu jeshi limkamate Lema,lazima kuna shida mahala,umeeleza ukiegemea upande mmoja na kumlaumu mkuu wa mkoa lakini yamkini kuna jambo,siku hzi waTanzania tunaakili tunaweza kuyapima maneno mnayotoa
Kwahiyo wewe unadhani Lema kafanya nini hadi atafutwe hivyo? Au ndo amehisiwa kusambaza ile barua ya Mkurugenzi wa Jiji, Kihamia. Mimi na wewe hatujui tutulie. Vinginevyo basi wewe ni Gambo na unajua Lema amekutenda vipi ndo maana unamtafuta.
 
Afadhali hivyo viwanja vianzishwe manake mbuga ya Serengeti ipo huko lakini watalii wanatua KIA wanaenda kuona wanyama na kurudi hawalali huko. Kiwanja cha serengeti kikiwa kizuri basi midege itakuwa inatua huko na watalii watalala huko na ni karibu kwenda kuona fisi na nyumbu wa serngeti kwa gharama nafuu. Uchumi wa wana Serengeti utaimarika na watafaidi matunda ya maliasili aliyowamegea muumba. Nyie mtaendelea kufaidi matunda ya Mlima Kilimanjaro.
jifunzeni ngeli kwanza[emoji23] !! wafkiri watalii wanahamishwa kizembe ivoo ata mkivijenga kumii kama mnaishi kishamba don't expect tourists wafikie uko samahani lakini
 
Ka gamba bwana! Leo nimekasikia kakiwaambia Masai kule longido kuwa serikali haiwezi saidia wenye njaa .
 
Gambo ana haingaika bure Lema hamuwezi,Lema ni wananchi wa Arusha,kupambana na Lema ni kupambana na wananchi wa Arusha,Lema siyo size yake kwa chuki alizo nazo kwa Lema,Lema angekuwa mtumishi wa umma angekuwa ameshamtumbua.
 
Nadhani ni wakati mwafaka Rais achukue maamuzi sahihi.
Gambo ni mteure wake anao uwezo wakumpeleka popote hata ampe uwaziri mkuu kama ni kipenzi chake lakini hili la kupandikuza chuki si kitu kizuri.
Lema ni mwanasiasa, Gambo ni mtendaji anahitaji busara ya ziada kama atataka kufanikiwa Arusha.
Ntibenda hakuwa mjinga kuiongoza Arusha kwa akili na maarifa, alikuwa na vyombo vya dola lakini alitumia diplomasia zaidi hivyo ndg yangu Gambo ajifunze kwa aliye mtangulia itamsaidia sana. Asishindane na wanasiasa, wao wanachokiona siku zote ni uchaguzi ujao (next election), kiongozi anaona kizazi kijacho (next generation). Hivyo basi kila mmoja ajitambue kwa manufaa ya wanachi na si ya vyama vyenu.
Ntibenda aliondolewa Arusha kwa bifu za UVCCM kwa sababu alikuwa anashirikiana vizuri na Viongozi wa upinzani ndo huyu Gambo akiwa DC akapandishwe cheo kuwa Rc baada ya kutofautina na Lema kwenye kikao mbele ya Naibu Waziri Jafo akiwa kwenye ziara jijini Arusha.
Gambo anatakiwa kutumia zaidi busara kama ana bifu zake na Lema anatakiwa kuziweka pembeni kwa sasa.
 
Inasikitisha kuona Rais mzima kukosa busara ya kuingilia kati mgogoro huu wa kipuuzi unaosababishwa na Mteule wake Gambo!
Mimi kwa kumheshimu Rais JPM napenda kumpa ushauri wa bure na sihitaji hata ukuu wa Wilaya au Mkoa! Kwamba: KWA HALI INAYOENDELEA ARUSHA KATI YA MBUNGE LEMA(Chaguo la Wananchi)na RC GAMBO(Chaguo la Rais) LAZIMA RAIS AIDHA AMUHAMISHE MTEULE WAKE GAMBO AU AMFUKUZE KAZI! Rais Magu asitegemee chembe ya maendeleo jijini Arusha kwa hali hii!Kwa vile Lema ni Mbunge wa kuchaguliwa na Wananchi Rais hana mamlaka ya kumwondosha ila kwa Gambo anaweza!
Kama Rais JPM hawezi kuchukua ushauri huu wa bure basi kuna hatari ya kuanza kuwatengeneza kina Mwamwindi wa Arusha na huyu Gambo ni mwanadamu kama wengine na huenda yaka mtokea kama yaliyomtokea Dr.Kleruu(RIP) enzi za uhai wake! It' s just a matter of time!
Huyu hafai kuwa Mwenyekiti wa mtaa anafanya kazi bila kufuata utaratibu anapenda sana kuingilia mambo ambayo hayamuhusu sijui hata JPM alimleta Arusha kufanya nini?
 
Back
Top Bottom