Mbunge wa Iramba Magharibi, Dkt. Mwigulu Nchemba ateuliwa kuwa Waziri wa Katiba na Sheria

Utawala huu tutaona mengi.Ila hongera Mwaya kijiwe kigumu mpaka jimbo karibu lichukuliwe na wahamiaji
 
Sasa bunge la bajeti si ndo lipo linadadavua mambo ya 2020/2021 nani wa kuisemea wizara? Lazima pawe na waziri kwenye wizara ndo maana Mh.Kamchagua mh Mwigulu Nchemba ili aweze kuisemea wizara so ww ulitaka wizara ibaki hidow?
Duh, umebaki mwezi mmoja bungeni kuvunjwa, hakukuwa Na haja kuteua waziri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Endelea na stress zako tayari jamaa ni Waziri wa Sheria na Katiba na huna cha kufanya!
 
Somo: Jilinde usife na korona, acha kuilalamikia serikali. Ukifa cheo chako anapewa mwingine na mkeo/mumeo anapata mtu mwingine na maisha yanaendelea. We usivae barakoa, wala usinawe mikono mara kwa mara ukafikiri unaikomoa serikali. Utakufa wewe, utazikwa wewe, kilicho chako tutagawana, kwisha habari yako.
 
Huyu Mwigulu mzee angemuacha tu aje mtaani awe mjasiriamali, alitakiwa aje kuonyesha PHD yake namna inavyofanya kazi kama mfano kwa vijana walioko mtaani huku..

Vijana wengi wako bench huku, Mkuu angetusaidia kuibua vipaji vipya na huyu angemuacha tu maana tayari anamtaji wa hela na maarifa angeweza tu kujiajiri..
 
Endelea na stress zako tayari jamaa ni Waziri wa Sheria na Katiba na huna cha kufanya!
Kama ambavyo uwaziri wake haunisaidii mimi , kama wewe sio mkewe au mumewe basi Huli mshahara wake ....so tujadili kwa picha pana ,hakuna mtu mwenye haki ya kupata stress na kazi yake zaidi ya familia yake ....au pengine mchepuko wake
 
Hongera sana mh Mwingulu unastahili sana kuvaa viatu vya Dk Augustine ,Hongera pia Raisi Magufuli kwakurudisha hili jembe katika kabineti

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…