Unakuta kuna bwege anajifanya anawajua anavyowatetea huwa nasema wewe fuga siku waje wakamate shingo ya mtoto wake aone walivyo hatari ndipo sasa ataiona ile kauli ya msiba usikie kwa jirani.Huwajui breed hii ya mbwa mzee!
Hawa hata wafugwe na malaika na wamzoee toka akiwa mdogo bado watamnyofoa mapumbu siku 1.
Hii breed hii ya mbwa hawanaga kumbukumbu, uwezo wao wa kufikiri haujafikia GB, siyo MB, ana memory capacity ya KB 11
Hapana huyo anajua kila kitu, jambo la kwanza kwa mtu yoyote anapokwenda nunua kitu lazima ataulizia model ili ajue anafuga nini.Hilo limbwa ni pitbull, haya mambwa hajawahi kua na akili timamu. Inaonekana jamaa alishikishwa kwa ni juavyo mimi bulldog ana miguu mifup na mkia mfupi. Sasa inaonekana jamaa aliangalia uso tu akajua ni bulldog kumbe ni pitbull jibwa wehu lilo pigwa marufuku kufugwa na nchi zaidi ya 50 ulimwenguni.
Sifa tu mimi watu wanaokuwa nayo haya maumbwa huwa naona ni wapenda sifa na hawana akili sawa sawa.Cheki dude hiliView attachment 2866051
Umeambiwa huwa wanawapaga chakula it means wameshachangamana nao. Mbona watu wengine mnakuwa na vichwa vizito kuelewa, unatetea vitu ambavyo ni hatari.Mbwa hawezi kupoteza kumbukumbu. Inawezekana hao wanafamilia hawajazoea kuwa nje muda huo hivyo kupelekea mbwa kutowatambua badala yake wameonekana kama wavamizi, wezi n.k
Wewe ndio huelewi nini kimefanyika hapo. Mbwa anaposhambulia watu especially wanaomfuga anatakiwa kuuwawa mara moja maana ni hatari ameshajifunza disobedience hatotii tena.Afrika ni zero brain,badala wapige risasi za usingizi kisha wachunguze kwa nini wamebadilika ghafla-wao wanaua.
Waliosema akili ni mali hawakubahatisha-kwa kweli.
Usiku wa kuamkia leo Tarehe 8/1/2024 majira ya saa Nne usiku Familia ya Ndugu Nicholaus Kunju ilishambuliwa na Mbwa na kuisababishia madhara Kwenye sehemu mbalimbali za miili yao,walio shambuliwa ni Mke wake pamoja na watoto.
View attachment 2865985
Walikuwa Mbwa aina ya Bull dog ambao anawafuga kwa ajili ya ulinzi nyumbani kwake Usagara, Mbwa hao walimshambulia binti yake wakati ametoka nje usiku huo wa saa Nne akiwa amesindikizwa na kaka yake, mara baada ya uvamizi huo kijana mwingine na mama yao walitoka kutoa msaada lakini Mbwa hawakuwatii na kuwashambulia wote.
Wote walioshambuliwa na Mbwa sio wageni kwa Mbwa hao kwani wamekuwa wakiwahudumia kwa chakula, baada Familia hiyo kujinusuru na kukimbilia ndani Mbwa waliendelea kuwa wakali na hapakuwa na uwezekano wa kuwapatia huduma majeruhi kwani hakuna alieweza kuingia wala kutoka ndani ya uzio.
Wakati haya yanatokea Kunju alikuwa kazini zamu ya usiku na alipigiwa simu kujulishwa juu ya tukio huku na kuambiwa mmoja wa majeruhi ana hali mbaya, Tulibahatika kufanya mawasiliano na Polisi kituo cha Misungwi ili waweze kufika eneo la tukio waue Mbwa ili msaada kwa majeruhi Upatikane.
Kwa ushirikiano na Zombwe na Lenox tulifanikisha kumtoa Kunju Kazini ili akashiriki uokoaji. Polisi walifika Nyumbani kwa Kunju majira ya saa saba usiku wakitanguliwa na watu wa Maliasili na wafanikiwa kuwapiga risasi Mbwa wote wawili na Majeruhi wakapelekwa Hospilali ya Cf kwa Matibabu.
Majeruhi wote wanaendelea vizuri, Shukrani kwa wote walioshiriki Kwenye utatuzi bila kumsahau Sheik Abdallah Omari.
C & P FROM X
- Pdizaina05
Afrika ni zero brain,badala wapige risasi za usingizi kisha wachunguze kwa nini wamebadilika ghafla-wao wanaua.
Waliosema akili ni mali hawakubahatisha-kwa kweli.
Kama livuta bangeJibwa kama hili unalifuga ili iweje?
View attachment 2866035
Kwa Rottweiler ndio kayatimba kabisa yani....Yaani unashauri rottweiller we jamaa unatania
Wewe ndio kichwa kizito kuelewaUmeambiwa huwa wanawapaga chakula it means wameshachangamana nao. Mbona watu wengine mnakuwa na vichwa vizito kuelewa, unatetea vitu ambavyo ni hatari.
Haya si ndiyo yalimwua mwanasoka wa zamani wa Zambia kule South Africa? Mnafuga madude gani haya? Bwana mdogo naye liliwahi kumgeuka bahati yake mafunzo ya kijeshi yakamwokoa akalidhibiti kama anadhibiti gaidi kwenye vita! Ilikuwa hatari sana!Kwani hawakuwa na risasi za kuwafanya wasinzie hawa maliasili.
Sema haya mabulldog inaelekea si ya kuyaamini maana nishasikia story nyingi za hata kuwageuka wenye nayo
Wangechukuliwa na polisi kwa mafunzo na utafiti siyo kukimbilia kuwaua tuUkimpiga ya usingizi then, hao mbwa washaathirika kisaikolojia hawafai tena for domestication.
Ni wa pambo ama anakusaidia ulinzi?Nina German Sherphard mkuu huyu hana madhara kabisa...
Hivi hii inawezekana mkuu? Mimi napenda mbwa ila koko tu, hii kujifanya mjuzi sana wa haya ma mbwa breed zingine hapana.Koko ukimfuga kizungu na mafunzo juu anakuwa mbwa poa tu 😀
Mzee Kinguge Ngombale MwiruNi Tanzania?
Hao mbwa si ndo wale waliomshambulia yule baba yake nanii hadi wakamuua?
Angalieni na mbwa wa kufuga, wengine ni chui.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]eti mara mia ufuge Simba [emoji23]Huyo sio Bull dog, hiyo ni jamii ya Pitbull. Bull dog wanamashavu kama ya mzee msaafu. Huyo ni Pitbull, maumbwa ya hovyo sana hayo. Ukitaka kuweka rehani usalama wa familia yako fuga hayo matakataka, mara mbili ufuge simba ujue unafuga mnyama wa porini ila sio hayo matakata.
Mimi binafsi siyapendi hata kuyasikia na mtu nikiskia yamemdhuru huwa nasema bora ili watu wajifunze maana kuna watu kuelewa hadi wapate madhara.
Ndugu sio hao sijui Bulldog/pitbull. Hao ni mbwa wa hovyo kabisa kufuga na anayefuga huwa namshangaa sana. Yaani huwa sijui wanapataga wazimu maana kikinuka hata wewe mfugaji mwenyewe wanakujeruhi kama sio kukuua kabisa. Nikijua una hao mbwa kwako hautaniona milele hata uwe ndugu yangu wa damu siji kabisa. Mbwa gani ukikaa na mwenyeji anakuwa mpole kabisa anachezesha tu mkia kama rafiki subiri sasa mwenyeji ajisahau aingine ndani labda kuchukua simu yake inaita wee akirudi anakuta unavuja damu.Ukifuga mbwa unatakiwa umzoeshe watu tokea akiwa mdogo, na uwe unampa mazoezi ya kutosha, haswa mbwa wakubwa wenye nguvu.
Watu wanakariri kufuga mbwa wa kizungu fashion, kama unamnunua ili akae bandani atoke usiku tu bora uache.