TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

Kwel ndugu zangu tunatakiwa na akiba ya maneno ,, ametangulia yeye sasa , rip mchungaj mtikila
 
Mtikila amefariki dunia.chanzo Devutwa ndani ya star tv.Leo
 
Hili litakuwa ni funzo kwa walio hai,
Alianza Komba kwa kumtukana Mzee Warioba alisema ni Mzee anayesubiri kufa tu ndio maana katuletea katiba yake kafa yeye kamuacha mzee wa watu,
Tunakuja kwa Celina Kombani wakati Lowassa anahama ccm alisema bora hata uhame usije ukatuifia ccm bure na Ikulu si pakupeleka wagonjwa, kafa yeye kamuacha Lowassa,
Mtikila trh 25 star tv,
Alisema Ikulu si ICU hao waliomchukua kwann wasimchangia hele aende akatibiwa Israil, Watz hawawezi kumpeleke Ikulu Mgonjwa,
Nasema tujifunze kuwa na lugha nzuri kwa wenzetu Afya na uhai wa Mwanaadam ni Mungu pekee ndio anajua haya kafa yeye kamuacha Lowassa,
Tafakari na chunga Mdomo wako haya ni maisha tu na tunapita usimuhukumu mwenzako kwa mabaya haliyakuwa ww unapumua huku Dunian.



Celina Kombani nae kumbe alisema hayo..?? Mie nilijua Komba, alivyomtusi Warioba ni kweli... kumbe Kombani nae alimtusi Lowassa....!!!

eeehh..🏃🏃🏃🏃🏃🏃🏃

Mungu yupo aiseeee....

Afya ni NEEMA toka kwa Mungu... tuchunge sana NDIMI ZETU.... Ndimi huumba na kubomoa...!!!
 
Duh Msiba Mkubwa, RIP Mchumgaji, natoa pole kwa familia yake
 
Siamini kupitia nguvu za giza ni Mungu pekee ndiye muweza wa yote. Inaonyesha unaamini juu ya ushirikina na ndio maana akili yako imeathirika na hayo.

Mimi nimkristo mzuri sana tena zaidi yako lkn wenye hicho LA tatu,w anajua maana wa gwajina,na kazi yake,
 
Naona dalili za msiba huu kutumika kisiasa!! Mnataka kutuambia kuwa ndugu zetu wote waliokufa kwa ajali uchunguzi wao haukuwa mzuri?

Nadhani sasa tutegemee ramri chonganishi toka kwa wale wanaotaka kubebwa ktk uchaguzi huu!!!
 
Alimkashifu lowasa kuhusu ugonjwa,mpaka akatishia kumshitaki mahakamani kwamba kwa nini anagombea wakati ni mgonjwa

Sasa naamini Mungu wa Lowassa ndiye Mungu wa Ibrahim na Isaka na Yakobo. Huyu si Mungu wa Magumashi. Humuondoa mtu duniani kwa kadri ya mapenzi yake, na humuacha mtu aishi duniani atakavyo yeye. Tahadhari kwenu mnaomhukumu Lowassa alianza Kombani na sasa Mtikila.

Sasa ni wakati wa kutafakari upya tunapopanda majukwaani tuhubiri sera za vyama vyetu siyo Matusi.

RIP Mtikila.
 
Pelekeni upumbavu wako Freemason lenu linawamaliza wapinzani wake,kisa ikulu,mbwa kabisa,

usijaribu kuingilia kazi ya Mungu atakuumbua hadharani mkuu, sheikh Yahya alijaribu ona kilichompata, tar. 25 sept Mtikila alidai CDM ndio waliomuua Wangwe na yeye Mungu Amethibitisha kuwa hakuna wakuchukua nafasi yake.
 
Serikali ifanye uchunguzi mkubwa ili kubaini chanzo cha ajali iliyopoteza maisha ya Mwenyekiti wa chama cha dp mch Christopher mtikila hasa katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi. R.I.P MTIKILA
 
Serikali ifanye uchunguzi mkubwa ili kubaini chanzo cha ajali iliyopoteza maisha ya Mwenyekiti wa chama cha dp mch Christopher mtikila hasa katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi. R.I.P MTIKILA

Mtikila pumzika kwa amani,lakini mungu aliye hai atajidhiirisha huu ya taifa lake,
 
Hatari sana hii.

Karma kazini, sisi sote ni wa Mola, kwake yeye tutarejea.

BACK TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom