Mchakato wa kulitoa meno Bunge ulianza kitambo, haya tunayoona ni matokeo tu ya process

Mchakato wa kulitoa meno Bunge ulianza kitambo, haya tunayoona ni matokeo tu ya process

Tigershark

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2018
Posts
7,051
Reaction score
12,566
Tujikumbushe kidogo!

Wakati wa spika Sitta,serikali ilisimamiwa ipasavyo na bunge!Ilipelekea mijadala mingi kupenya bungeni na kujadiliwa!Viongozi wa CCM walimlalamikia Sitta kwa kuiruhusu mijadala bungeni ambayo inaishambulia serikali!Sitta hakusikia na akaendelea kulisimamia Bunge kwa kufuata kanuni na taratibu zake.

Ilipokuja wakati wa kuchukua form tena ili kugombea uspika,Sitta alionesha nia ya kugombea tena!Akafanyiwa zengwe na wanaCCM ili asishike kiti tena,ikaletwa kauli ya ujanja ujanja ya kwamba sasa ni zamu ya mwanamke kuwa spika,Anna Makinda akashika usukani.

Hesabu za CCM kwa mara nyingine zikawa hazijaenda sawa kama walivyotarajia,bado bunge likawa linaibua hoja zenye mashiko kuiwajibisha serikali na mijadala hiyo ikawa inapenya vizuri tu bila zile "toa nje".

CCM wakaendelea kujipanga,wakaona Ndugai angeweza kuwasaidia maana wakati akiwa naibu alionesha viashiria vya ubabe dhidi ya wapinzani wakati Spika akiwa hayupo.

Ndugai akapewa Uspika.
Ili kuipanga safu vizuri,Tulia akapenyezwa kwa namna ambayo watu wengi walibaki na mshangao!Maana alikuwa Naibu Mwanasheria Mkuu,na kimaadili hapaswi kuwa mwanachama wa chama chochote!Ghafla akapachikwa ubunge wa kuteuliwa na kupewa kugombea unaibu spika ambapo alipita.

Safu ya kuling'oa meno bunge ikawa imekamilika.

Haya tunayoona sasa ni matokeo ya mchakato mrefu sana ndani ya CCM,ila kilichoongezeka awamu hii ni kuwa mamlaka iliyojichimbia chini zaidi imeonesha dhamira ya dhati kulishika Bunge.
 
JANGA.jpg
 
Kusema bunge halina meno ni dhana potofu. Kwani wabunge wanazuiwa kutoa maoni? Wabunge wanazuia kutafuta maendeleo ya wananchi wao?.

Bunge linakosaje meno wakati wabunge hawajazuiliwa kufanya shughuli zao?.
 
Kusema bunge halina meno ni dhana potofu. Kwani wabunge wanazuiwa kutoa maoni? Wabunge wanazuia kutafuta maendeleo ya wananchi wao?.

Bunge linakosaje meno wakati wabunge hawajazuiliwa kufanya shughuli zao?.
Kwenye kipengele cha kuisimamia serikali ndio tabu!
 
Kusema bunge halina meno ni dhana potofu. Kwani wabunge wanazuiwa kutoa maoni? Wabunge wanazuia kutafuta maendeleo ya wananchi wao?.

Bunge linakosaje meno wakati wabunge hawajazuiliwa kufanya shughuli zao?.
Hii mada ipo nje ya uwezo wako wa kufikiri.
 
Kusema bunge halina meno ni dhana potofu. Kwani wabunge wanazuiwa kutoa maoni? Wabunge wanazuia kutafuta maendeleo ya wananchi wao?.

Bunge linakosaje meno wakati wabunge hawajazuiliwa kufanya shughuli zao?.
Ni swali la kijinga sana.

Ni sawa na mjinga mmoja aliambiwa kwamba kuna uhaba wa meli bandarini,zinakuja kwa uchache sana.
Unajua alisema nini?
Aliuliza;kwani bahari imehama? Kama bahari ipo....aliendelea kusema, meli zitakuja tu!

Basi mawazo yake huyu Juha siyo tofauti na yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni swali la kijinga sana.

Ni sawa na mjinga mmoja aliambiwa kwamba kuna uhaba wa meli bandarini,zinakuja kwa uchache sana.
Unajua alisema nini?
Aliuliza;kwani bahari imehama? Kama bahari ipo....aliendelea kusema, meli zitakuja tu!

Basi mawazo yake huyu Juha siyo tofauti na yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huyo huyo aliyesema kwa bahari inahama, ndiye aliyeongeza eneo la matumizi ya bandari, hakuongea tu halafu mambo yote yakaishia hapo.

Huwa anaongea halafu anaweka uhalisia wa maisha katika maongezi yake. Hafurahishi jukwaa, siku zote huenda mbali zaidi.
 
Bunge halina meno, Spika anatetea mambo ya msingi lakini anaondolewa madarakani kihuni. Hii sio haki kabisa.

Tulipaswa kuwa na Bunge lenye mamlaka ambalo nalo lilitakiwa kumkataa rais ambae anatumia madaraka vibaya kuteua mawaziri wenye harufu ya ufisadi.

Rais anakataa kuhojiwa na Bunge bila sababu? Bunge linazidiwa nguvu bila sababu. Hii ni sababu hatuna wabunge wawakilishi wa wananchi.

Aliyeharibu uchaguzi wa 2020 ndio wa kulaumiwa maana Bunge halikuchaguliwa na wananchi na halina meno.
 
Bunge halina meno, Spika anatetea mambo ya msingi lakini anaondolewa madarakani kihuni. Hii sio haki kabisa.

Tulipaswa kuwa na Bunge lenye mamlaka ambalo nalo lilitakiwa kumkataa rais ambae anatumia madaraka vibaya kuteua mawaziri wenye harufu ya ufisadi.

Rais anakataa kuhojiwa na Bunge bila sababu? Bunge linazidiwa nguvu bila sababu. Hii ni sababu hatuna wabunge wawakilishi wa wananchi.

Aliyeharibu uchaguzi wa 2020 ndio wa kulaumiwa maana Bunge halikuchaguliwa na wananchi na halina meno.
Waimba mapambio mlimpa nguvu ya kufanya uchafuzi mkuu, kwani ili kuwa ni kusifia hata uovu na kushiriki kuwahujumu watetezi was kweli wa raia.
 
Back
Top Bottom