Mchakato wa kupata Dada wa kazi za ndani unapaswa kuwa vipi ili watoto wawe salama?

Mchakato wa kupata Dada wa kazi za ndani unapaswa kuwa vipi ili watoto wawe salama?

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
3,925
Reaction score
8,853
Hili sio suala la kulipuuzia kabisa kwa sababu asilimia kubwa sana linawahusu hata kama sio leo ni kesho.
 
Hakuna mchakato acheni dhulma mnawadhulumu watoto wa watu mishahara yao, mnawanyanyasa wengine hamli nao meza moja nyie mkiwa sebuleni wao wanakula jikoni, wakiugua mnawasimanga mnawaona wavivu mnaishi nao kama watumwa alafu unaenda kazini unamuacha amlee mtoto wako unategemea nini? Lazima hasira zake atazimaliza kwa mtoto wako, tenda haki kwake muonyeshe upendo nae atakulipa wema kama unavyo mtendea
 
Hakuna mchakato acheni dhulma mnawadhulumu watoto wa watu mishahara yao, mnawanyanyasa wengine hamli nao meza moja nyie mkiwa sebuleni wao wanakula jikoni, wakiugua mnawasimanga mnawaona wavivu mnaishi nao kama watumwa alafu unaenda kazini unamuacha amlee mtoto wako unategemea nini? Lazima hasira zake atazimaliza kwa mtoto wako, tenda haki kwake muonyeshe upendo nae atakulipa wema kama unavyo mtendea
Mi naona akiona hapamfai bas achague kurudi kwao na siyo kuua watoto
 
Kabla ya kujadili huo mchakato wako.....
Unadhani nini hasa chanzo cha wadada kubadilika na kuanza kufanya ukatili kwa watoto ambao sio watesi wao...??
Minadhani tunatakiwa kuangalia root cause kabla ya kulewa...😑
 
Hakuna mchakato acheni dhulma mnawadhulumu watoto wa watu mishahara yao, mnawanyanyasa wengine hamli nao meza moja nyie mkiwa sebuleni wao wanakula jikoni...
Kwa kweli huwa inanishangaza sana...mtu anayekupikia chakula unamnyanyasa, una hakika gani na chakula anachokutengea? Hata asipoweka sumu, akitemea makohozi je? Unaishi na mdada wa kazi na kumtenda kama mnyama, kisha unamkabidhi 'Junior' au "Princess' wako akulelee; kweli..? What goes around comes around..!
 
Na bado watauwa hivyo vitoto vyenu had mkomeee, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Toa recommendations basi boss, mimi naona familia waishi na dada wa kazi kama mwanafamilia mwenzao, na wapate wadada wakazi wenye utimamu..afya ya akili.
 
Kwa kweli huwa inanishangaza sana...mtu anayekupikia chakula unamnyanyasa, una hakika gani na chakula anachokutengea? Hata asipoweka sumu, akitemea makohozi je? Unaishi na mdada wa kazi na kumtenda kama mnyama, kisha unamkabidhi 'Junior' au "Princess' wako akulelee; kweli..? What goes around comes around..!
Alafu wanawake ndo wanaongoza kuwanyanyasa wadada wa kazi we mwanaume ukimtetea dada wa kazi unaamsha vita utaambiwa unatembea nae
 
Mi naona akiona hapamfai bas achague kurudi kwao na siyo kuua watoto
Mi naona wewe ukiona huwezi kuishi nae kwa wema ni bora usitafute dada wa kazi maana ukimfanyia ubaya huwezi kujua ataulipa kwa namna gani huenda asiue mtoto tu anaweza hata kuwawekea sumu nyumba nzima au awachomee ndani siku 1
 
Mi naona akiona hapamfai bas achague kurudi kwao na siyo kuua watoto
Sasa ww kwann unamnyanyapaa wakat umemleta akulelee watoto wako

Ishi nae vizur hata yeye hawez kua nahasra na mtoto wako
Lakin ww unamuona kama hafai
Kukaa na ww meza moja na bado unataka akae na Wanao kweli
 
Alafu wanawake ndo wanaongoza kuwanyanyasa wadada wa kazi we mwanaume ukimtetea dada wa kazi unaamsha vita utaambiwa unatembea nae
😄😄😄😄😄 Yaaaan ndo Kwa hapo
Inabid unyamaze
 
Fanyeni kama watu wa Oysterbay wanaajiri dada wa kazi 300k

Mtu professional kabisa na hapo anafanya usafi kwa mashine anafulia mashine , kupika anapewa kitabu cha vyakula chenye maelekezo ya hatua kwa hatua pamoja na mashine za upishi wa hapa na pale 😅... na marupurupu chungunzima.

Kama huna hio ela au naww mwanamke ndo mshahara wako huo 300k we kaa ulee watoto kwanza mana hujafikia kuajiri msaidizi wa nyumba.

Mtu unamlisha maharage yale yanayokaa kwa fridge mwezi bado unamsimanga! Akulelee mtoto/mtumetume kama pia/akupikie/akufanyie usafi eeh hapo watoto zenu mtawakuta sana wametiwa sindano za utosi.

Unamlipa afu 50 punguza mdomo mhudumie ishi nae kama mdogo wako kuna mtu anaishi na dada wa kazi kama mdogo ake mpaka anasema usinilipe /watu wanawasomesha wadada wa kazi/wanawapa haki sawa na watoto wao hapo msichana atakuulia mtoto kweli??

Hapa jirani kuna dada wa kazi saizi yuko chuo mwalimu Nyerere anasomeshwa na boss! Mana kawalea watu wamefika O level na yy akaanzishwa QT
 
realMamy haitaji Dada wa kazi, anapangilia ratiba zake vizuri kuhakikisha Mwanae anapata malezi na huduma za Mama kwa 100%
 
Malezi ya mtoto ni jukumu la Mama na Baba(Kama wako hai wote).

Hallelujah!!!
 
Yan ndo uhalisia rafikiyngu aliniomba nimtafutie msichana wa dukani mshahara elf 50 nikamtafutia bint jirani anasema ni Mkubwa anatak ambae anaweza kuamka akaosha vyombo ndipo aende dukani Yani ahudumie familia ndipo akauze duka
Nikajiuliiza ni WA dukani au msichana wa kazi za nyumbni
Yani mtu ahudumie wateja huko arudi et umwambie osha vyombo pika 😀😀 yeye angeweza anawatoto wanne inamaana siku akiwa yupo mwenyew dukani hapa home bint anakuwa msichana wa kazi kwakweli sikutaka dhambi nikamwambia apambane na familiayake sio kutesa watoto wa watu
Ni unyanyasaji mkubwaa! Wao hawawezi halafu utasikia mimi binti wa hivyo siwezi mvivuuu!
 
Katika vitu sivipendi kuwa na House Girl(Hg) ,kwanza siwaamini katika mapishi ,pili wana ushirikina sana ,tatu ni rahisi sana kutumika maana wengi hawajielewi.

Mimi napika vizuri kuliko house girl ,tatu muda mwingi sipo home ,tatu nikiwa home kazi nyingi nafanya mwenyewe sipendi kukaa kizembe...bora nikae na ndugu tu kuliko washirikina hao wanaotoka Iringa kama Hg.
 
Back
Top Bottom