Mchakato wa kupata Dada wa kazi za ndani unapaswa kuwa vipi ili watoto wawe salama?

Mchakato wa kupata Dada wa kazi za ndani unapaswa kuwa vipi ili watoto wawe salama?

Mimi naona hakuna tatizo na dada wa kazi. Yote yanayotokea yamesababishwa na upotevu wa maadili mema kwenye jamii nzima. Ndio maana baba anamuua mama, mama anaua mtoto, mtoto anaua yule etc.
Wote tumekuwa wahanga wa malezi maovu. Wadada hawa mnaowazungumzia wametoka kwenye jamii yetu ya mauaji kwa hivyo wamebeba roho mbaya. Ukifanya utafiti wala wadada wa kazi hawaongozi kuua ukilinganisha na wazazi.
Tubadilike tumrudie Mungu wetu wa haki na siyo kung'ang'ania Mungu wa waamori.
Message sent
 
Sasa ww kwann unamnyanyapaa wakat umemleta akulelee watoto wako

Ishi nae vizur hata yeye hawez kua nahasra na mtoto wako
Lakin ww unamuona kama hafai
Kukaa na ww meza moja na bado unataka akae na Wanao kweli
Nimeelewa usemayo mkuu,lakini akiona hatendewi mema achague kurudi kwao
 
Mi naona wewe ukiona huwezi kuishi nae kwa wema ni bora usitafute dada wa kazi maana ukimfanyia ubaya huwezi kujua ataulipa kwa namna gani huenda asiue mtoto tu anaweza hata kuwawekea sumu nyumba nzima au awachomee ndani siku 1
Aisee😭
 
Tunafosi uhalisia wa maisha hauturuhu mshahara elf 30 sijui 50 Tena kumpa Kwa masimango mtoto wa watu anafanya kazi km mbwa.

Mwingine ana mtoto Mchanga hamshiki zaidi ya mda wa kumnyonyesha ni dada mbadilishe,dada Mpe maziwa ,mfulie kabint la miak 16 uvumilivu huo anautoa wapi

Hunatime nae Wala kujali ukute nyumba inawatoto wengi ndio balaa Kila mda dada hiki dada kile
Walipe vizuri ishini nao km familia wasikilizeni shidazao
Wewe unalipwa sh ngp kazini kwako mkuu..unahalalisha mtoto afanyiwe ukatili kwa sababu dada aligombezwa na mwenye nyumba? Kwa nini asiondoke badala ya kudhuru mtoto mdogo?
 
Mbona zipo kampuni zilizosajiliwa na kutambulika zinatoa hao "dada wa kazi". Tatizo wengi wanakwepa gharana ndiyo hayo unachukua mtu humjui unaishi naye.
Serikali inazitambua? Au
Mbona zipo kampuni zilizosajiliwa na kutambulika zinatoa hao "dada wa kazi". Tatizo wengi wanakwepa gharama ndiyo hayo unachukua mtu humjui unaishi naye.
serikali inazitambua? Au ndo zile akifika kesho tena simu anahitajika kwingine.
realMamy haitaji Dada wa kazi, anapangilia ratiba zake vizuri kuhakikisha Mwanae anapata malezi na huduma za Mama kwa 100%
😅
 
Fanya utafiti ili kumpata house girl anayekufaa
1.Ukimpata mhesabu kama ndugu au mtoto wako,Usimbague!
2.Unachokula naye ale hicho hicho
3.Mpe mshahara wake kwa wakati.
4.Usimkemee mbele ya watoto au wageni wako au hata akikosea tumia hekima kumuonya kwa upendo ukijua hakuna asiyekosea.
5.Akienda likizo tuma zawadi kwa Wazazi au Walezi wake.
5.Mpe muda wa kupumzika au hata kutoka.

NB Ma house girl wengi ni watoto wa maskini unamnyanyasaje?
 
Wewe unalipwa sh ngp kazini kwako mkuu..unahalalisha mtoto afanyiwe ukatili kwa sababu dada aligombezwa na mwenye nyumba? Kwa nini asiondoke badala ya kudhuru mtoto mdogo?
Hakuna sehemu nimesema afanye ukatili Kwa watoto
Nalipwa elf 20 mkuu
 
Kuna situation zinakulazimu uajiri msaidizi, nadhani hoja iwe ni kwa namna gani kupunguza hayo matukio?

Hakuna jinsi ya kupunguza mkuu ,mbona wanandoa wanachinjana ,wanasalitiana ,wanaachana wakati hapo awali walipendana na kuchunguzana kabla ya kuanza uhusiano? Binadamu hatabiriki ,binadamu hubadilika kulingana na muda na mazingira ,so hakuna jinsi ya kufanya kupunguza ukatili...asipofanyiwa na Hg atakuja kufanyiwa na walimu shuleni.

Kupunguza ukatili kwenye Jamii ni kwamba Serikali ipunguze ukali wa Maisha kwa watu kwa kupunguza kodi,tozo ,kuwawezesha kwa mikopo yenye riba nafuu ,kujenga mazingira wezeshi ya biashara ,serikali kutanua soko la bidhaa ,serikali isubsdize baadhi ya huduma kupunguza ukali wa maisha...Watu wanafanya matukio ya ukatili kwasababu ya stress za maisha tu lakini wakiwa stress free matukio yatapungua.
 
Ishi naye kama mmoja wa familia yako na usimfanye mfanyakazi 24/7. Kuna binti nilimchukua mkoa X to cut story nilikaa naye miaka 5 tuliishi naye vizuri sana Akapata mchumba nikaona ni kheri naye akayaanze Maisha Take Akaolewa
 
Hili sio suala la kulipuuzia kabisa kwa sababu asilimia kubwa sana linawahusu hata kama sio leo ni kesho.
Mchukue eneo linalojulikana vizuri kwako na nduguze au nduguzo au watu unaowaamini wanaomjua vizuri .Hao ndio wanakuwa wadhamini wake in case of anything wana details zake zote A to Z kuanzia tabia nk
Kama umeletewa na kampuni omba msainishe mkataba asaini kwa sahihi na dole gumball yeye na mwakilishi wa hiyo kampuni ulikomtoa na picha zao

Pili akupe nba ya nida na uihakiki mfano mwambie asajili laini uyamlipia kama ile namba kafoji akiweka dole gumba wakati wa kusajili line ya simu itakataa ila kama ni yake itakubali Chukua details zote za kwenye kitabulisho cha NIDA hifadhi
 
Mi naona akiona hapamfai bas achague kurudi kwao na siyo kuua watoto
Ana huo ubavu wa kukwambia anaomba arudi kwao umpe nauli na madai yake??

Dogo wa miaka 13 aliekulia bush huo ujasiri anautoa wapi kumface boss mkali kama pilipiki muda wote??

Kikubwa kama binti mdogo ishi nae kama mwanao, mfokee kama unavyomfokea mwanao, hii inafanyaga hata mwanao na binti wanakua marafiki kabisa hata hawezi kumdhuru maana ndo faraja yake.
 
Hili sio suala la kulipuuzia kabisa kwa sababu asilimia kubwa sana linawahusu hata kama sio leo ni kesho.
Leeni watoto wenu msitafutie watu lawama, kuzaa uzae wewe kulea alee mwengine, acheni tamaa za ulimwengu.
 
Back
Top Bottom