Mchanganuo tozo za LUKU kuanzia August 20-2021

Mchanganuo tozo za LUKU kuanzia August 20-2021

Ndio maana watu wakapendekeza iitwe kodi ya luku/ umeme/ meter kwa sababu inatozwa kwa meter sio jengo.

Jengo lenye meter 2 litatozwa 2,000 kwa mwezi wakati kimsingi kodi ya jengo inatakiwa iwe 1,000/- kwa jengo.
Kwa nini jengo moja ulete mita 2? Utavuta nyaya ngapi toka nguzo kuu kama unataka mita 6?
 
Ukinunua Umeme utalipia Kodi nne:
1. VAT - 18%
2. Ewura - 3%
3. REA - 1%
4. Kodi ya Jengo (Tsh 1000- Tsh 5000)

Awamu ya sita, tozo ziendelee!

2872779_Screenshot_20210806_102721.jpg
 
Sasa nyumba yenye luku zaidi ya moja itakuwake?
Jana nilimsikia mmoja wa watu wa TRA akisema,"mmiliki wa nyumba yenye wapangaji tu na mwenye nyumba haishi hapo anaweza kwenda Tanesco na kuainishi mita zinazotakiwakukatwa kodi "
 
Amang'ana ghenu!

Naomba niende kwenye maada moja kwa moja,

Wakuu naomba kuelimishwa/kufafanuliwa kuhusu hili Tangazo la TRA na TANESCO kupitia maswali ninayotaka kuuliza hapa kwa sababu kuna vitu Tangazo halijaweka wazi pengine ndo ikapelekea mimi kutokuliewa vilivyo na kuibua mswali kichwani mwangu,

Maswali yangu ni kama ifutavyo

1) Swala la wapangaji kuhusu hii kodi ya majengo likoje? Na wao ni wahusika wa kulipa hii elf1 kila mwezi kama sivyo TANESCO na TRA wanaliweka vipi?

2) Nyumba moja inazo Luku zaidi ya mbili, hili nalo likoje? Jengo moja litakuwa linalipiwa kodi zaidi ya elf2?

3) Je kuna maelekezo yoyote tukilipa hiyo wenye nyumba wawarudishie hicho kiasi walicholipa? Kama yapo kuna utaratibu gani umeweka kwa hizo hela kurudi kwa wapangaji!

Nb, Nimepita kwenye moja ya page zao kwenye mitandao hakuna majibu ya maswali yangu.

Hata kama sio wao watajibu naomba mwanaJF alieliewa Tangazo majibu yako tafadhali.
Mwenye nyumba wa kuwarudishia hio pesa labda ni kwa wale ma Don ila wapangaji wa Manzese, Vingunguti na Kiwalani mjiandae kisaikolojia😅😅😅
 
TRA wafunguka anayetakiwa kulipa kodi ya majengo kupitia Luku, kati ya mpangaji na mwenye nyumba
Udaku Special / 1 hour ago





Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo.



Hayo yameeleza na Lazaro Lucas katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo ameongeza kuwa kwa sasa kuna changamoto wa kutofautisha mnunuzi wa umeme kama ni mwenye nyumba au mpangaji, hivyo kwa mwanzoni mpangaji anaweza kukatwa kodi hiyo kimakosa.

“Hiyo kodi inapaswa kulipwa na mwenye jengo lakini kwa mwanzo kumekuwepo na changamoto ya kujua ni yupi mwenye jengo ni yupi mpangaji kwa hiyo mwanzoni [mpangaji] unaweza ukapata ‘bill’… mwenye jengo afike ofisini aseme nyumba zangu ni moja, mbili, tatu, ili wenye zile mita ziondolewe,” amesema Lucas.

Lucas ameongeza kuwa mwenye jengo anaweza kulipia kodi ya nyumba za wapangaji taslimu shilingi 12,000 kwa kila nyumba ya kawaida kwa mwaka na namba za mita za wapangaji zitaondolewa kwenye mfumo, au kodi hiyo itahamishiwa kwenye mita yake.

Aidha, TRA imesema kuwa endapo mwenye jengo hatowasilisha taarifa za wapangaji TRA, wapangaji wanaweza kupeleka malalamiko yao kwamba wanatozwa kodi ya jengo kimakosa.

Viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa kila jengo la kawaida ndani ya kiwanja kutoka shilingi 10,000 iliyokuwa ikitozwa awali, na shilingi 6,000 kwa kila sakafu ya ghorofa kutoka 5,000. Hata hivyo kwa upande wa halmashauri za wilaya na miji midogo nyumba za ghorofa bila kujali idadi ya sakafu zitatozwa shilingi 6,000.

Kwa utaratibu huo kila mnunuzi wa umeme atakatwa shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa. Kwa wanaotumia mita za ankara watalipa kodi hiyo kwa pamoja katika Ankara zao za mwezi.

Source : Swahili Times
Kwahio ishu ni kuwapata wenye nyumba kumbe😅😅😅 hapa kimeeleweka
 
Hapa inabidi waongeze Kodi kwa ajiri ya kutunisha mfuko/bodi ya mikopo Ili vijana wetu wawe na uhakika wa kupata mikopo ya Elimu ya juu
Hio Elimu ya juu inawasaidia nini zaidi ya kwenda kugombania kazi nafasi 5 watu elfu 20
 
Kuna wapumbavu wanaamini kutokulipa kodi au kulipa kodi ndogo zaidi ndio maendeleo kwa wananchi...hamna nchibiliyoendelea ambayo wananchi wake wanalipa kodi ndogo...hamna, na hayo maendeleo yanachangiwa ktk hizi tozo...
Ila pia hamna nchi ilioendelea kwa kukumbatia katiba ya kipuuzi kama tulionayo ambayo wanasiasa wanajilimbikizia mali kifisadi na kuachiliwa huru tu wazurure mitaani!

Hakutakuwa na maendeleo kama hio mitozo itakuwa haisimamiwi vilivyo na ikaenda kufanya yale yaliokusudiwa. Kama watu watagawana hizo tozo kwenye sandarusi na katiba hii tulionayo kuna kipi mtakifanya 😅😅😅
 
matumizi ya kodi zetu yataonekana wazi, tutaona mabadiliko ya barabara, maji, elimu, matundu ya vyooo, zahanati, dawa hospitalini, n.k
Una uhakika gani katika hili? Je, miaka yote hio huko nyuma ambapo serikali ilikuwa ikifanya majukumu yake bila tozo mbona majengo yalijengwa mengi tu? Shule zilijengwa, hospitali zilijengwa why today?
 
Ila pia hamna nchi ilioendelea kwa kukumbatia katiba ya kipuuzi kama tulionayo ambayo wanasiasa wanajilimbikizia mali kifisadi na kuachiliwa huru tu wazurure mitaani!

Hakutakuwa na maendeleo kama hio mitozo itakuwa haisimamiwi vilivyo na ikaenda kufanya yale yaliokusudiwa. Kama watu watagawana hizo tozo kwenye sandarusi na katiba hii tulionayo kuna kipi mtakifanya 😅😅😅
Kuna mahali katiba imeruhusu watu kujilbikizia?
Katiba mpya ni chaka tu linatimiwa wala sio mwarobaini wa changamoto zilizopo
 
Back
Top Bottom