Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Mchungaj Anna ndi tatizo pale kanisan kwetu tangu aje yy wafanyakazi wengi wanaondolewa pale Anna ni mfitini sana.
Bas usiwe unaenda njoo sinza kkkt Kama unamuona Anna ndio kichomi wa kimaro
,Kimaro alivyo na kujikweza kote huko uoni wee au ibadani unaimba Kisha nakuondoka tu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Mchungaj Anna ndi tatizo pale kanisan kwetu tangu aje yy wafanyakazi wengi wanaondolewa pale Anna ni mfitini sana.

Aisee!

Yatamshinda lakini soonest possible!

Anajaribu kupingangana na nguvu ya Mungu?!

Haya ngoja inyeshe tuone Penye kuvuka.
 
Kufuatia semina iliyokuwa imeanza katika usharika wa KKKT KIJITONYAMA ikiongozwa na Rev Dr. Eliona Kimaro imelazimika kusimama kufuatia barua aliyopewa ya likizo ya siku 60 na kupelekea kushindwa kuendelea na semina hiyo...
Hivi hawa KKT mbona migogoro yao haiishi? Kanisa linakuwa na migogoro utafikiri chama cha siasa?
 
Sijaona kosa la mch. Kimaro
Mimi kama mlutheri tunataka mchungaji wa aina yake. Wengi tumechoshwa na aina ya mahubiri ya kutafsiri Biblia kama hadithi, ibada nyingi zinapooza ndio maana watu wanakimbilia kwa mitume na pentekoste.

Lutheran kuna shida sehemu nyingi, mchungaji akionekana yuko karibu na anakubalika na waumini anahamishwa.
 
Mkuu kwan haitakiwi kusifu na kuabudu??
Hakunaga maandalizi Ndugu yangu, zile nyimbo Wala hazina hata upako. To be honest, Huwa sipendi maana mpiga vyombo na muimbaji wote ni tofauti, wakiwa na maandalizi ni sawa. Kuna muda mchungaji ameshapanda madhabahuni, bado wao wanaimba, Kuna muda sauti hata hazieleweki. Fuatilia
 
Itakuwa kuna mtu ameanza kuhisi Dr Kimaro anaweza kuwa kikwazo kwake manake kama ni Shule tayari anayo Kubwa pengine kumzidi.

Kuna Wakati Viongozi wa Kanisa wanatuhumiwa kutafutana hadi kwa njia za Kishirikina kisa Madaraka

Ni matumaini yetu huu Mgogoro utapita na Kanisa litaendelea kuwa Imara.
 
Kanisa la KKKT limemsimamisha kazi mchungaji Eliona Kimaro wa usharika wa Kijitonyama kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi, siyo mara ya kwanza wala ya pili mchungaji huyu kufanyiwa majaribio ya kuondolewa lakini ndiyo hivyo Mungu alikuwa upande wake.

Na hii ndiyo KKKT kila sehemu wanagombana na kupelekana hadi mahakamani.

Poleni washirika wote wa Kijitonyama.

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…