Mchungaji Kimaro: Matajiri ndio Walimzika Yesu, akina Petro na wenzake waliokula bure miaka 3 walimkimbia!

Mchungaji Kimaro: Matajiri ndio Walimzika Yesu, akina Petro na wenzake waliokula bure miaka 3 walimkimbia!

Mchungaji Kimaro wa KKKT Kijitonyama amesema Tajiri Yusuf wa Almathaya ndio aliyemzika Yesu katika kaburi lake la kifahari

Kimaro amesema Kanisa linawahitaji Matajiri kwa sababu ndio wanaoliondolea Kanisa aibu Wakati wa uhitaji

Hivyo tusiwape majina mabaya Matajiri kwa kuwaita Mafisadi, Wahujumu Uchumi au Freemason Kwani utajiri ni baraka hata katika level ya familia Kwani ndio wanaofuta aibu za familia, amesisitiza mchungaji Kimaro

Kimaro amesema Watu wengi ni walinzi tu wa makaburi kama wale Walinzi wa Pilato waliotumwa kulinda kaburi la Yesu, hivyo wewe kama mkristo usikubali kuwa Mlinda makaburi

Nawatakia Pasaka Njema!
hii haimaanishi hawakupenda kumzika au walimtelekeza, kimaro ni mpotoshaji sana, anatafuta kufungiwa tena. kumiliki kaburi enzi hizo halikuwa jambo dongo manake lilihusisha kumiliki ardhi hapo unapochimba kaburi. wanafunzi wa Yesu hawakuwa matajiri, wengi walikuwa wavuvi na watu wa kawaida na walipoteza muda wao mwingi kuhubiri na Yesu hawakuwa matajiri, Yesu mwenyewe hakuwa tajiri ndio maana hata walipoombwa kodi ya kaisari alimwambia petro akavue samaki atakuwa mdomoni mwake kuna dinari ya fedha wakatoa sadaka kwa kaisari.

huwezi kuchimba tu popote, ndio maana Yusufu tajiri alishanunua kipande pale na akachimba kaburi lake, na kwasababu alikuwa mwanafunzi wa siri wa Yesu, aliamua kuuomba mwili akazika kwenye kaburi alilokuwa ameshalichimba. kina petro na wengine wangechimba lingine la nini sasa wakati tayari limetolewa?

na hata petro na wenzake wangekuwa wamemkimbia nisingeshangaa manake Yesu alikufa kifo cha aibu mno na wanafunzi wake walikuwa terrified, kama kweli walikimbia haimaanishi hawakupenda kumzika. alikufa kifo cha aibu na cha kutisha na wanafunzi nao walihofia kukamatwa kuwekwa msalabani. kimaro awe makini na mahubiri matamu ambayo hayaokoi, no wonder walimsimamisha. anawaza tu hela hela all the time. kwani kuzikwa ni nini hata angezikwa kimasikini unafikiri asingefufuka?

vilevile, Yesu kuzikwa na tajiri ilishatabiriwa na Isaya 53, pale lilikuwa linatimia Neno tu la Mungu. manake kama Neno lisingeandikwa, basi pengine masikini wangemzika. msimsikilize kimaro, Yesu alizikwa na tajiri ili kutimiza unabii wa Isaya 53 na kila maisha aliyoishi alikuwa anaishi akitimiza aliyoandikiwa. makanisani hatuhitaji tajiri, tunahitaji watu walioamua kumfuata Mungu, tunahitaji watu wanaomwabudu Mungu, awe tajiri au masikini wote mbingi inatuhitaji.

shida kubwa ya kimaro ni kwamba hajaokoka na mahubiri yake anatumia elimu ay dunia hii na akili ya kibinadamu, hahubiri kwa Roho Mtakatifu ndio maana siku zote anahubiri mahubiri ya kupendezesha watu na motivations, hayo yanajenga mwili ila sio roho.
 
Huyu jamaa hafai,sisi padri katuambia aliyepeleka habari za kufufuka Yesu aliyekuwa anajulikana Kama kahaba,Maria Magdalena ndio alikuwa wa kwanza kusambaza habari za ufufuko wa Yesu,so hata nasi tusijione wanyonge pamoja na madhaifu yetu tukitubu tunaanza upya na kuwa wasambazaji injili waziri🙏wajumbe wa Mungu,yeye kimaro anawasujudu matajiri na kuwadharau watunza makaburi🤔kila mmoja ana nafasi yake,moyo wake umejaa tamaa ya mali na amepotoka.
Kutunza makaburi ni ajira halali kama ajira zingine watu wameajiriwa kutunza makaburi na serikali naye kaanza dharau kama Godblless lema kusema kazi ya bodaboda ni laana

Huyu naye kaanza kuponda watunza makaburi.Watu wanaishi kwa mishahara hiyo anawaponda .Wengine hao watunza makaburi ni waumini wa KKKT anawapelekea ujumbe wa dharau hivyo Hawatendei haki
 
Mimi wewe hunisumbui kwakua nakufahamu vyema tu.

Namna ulivyopata hiyo ajira uliyonayo kwa Sasa hapo ofisi ya mawakili jinsi ulivyoo maskini.

Yaani kama sio yule Rafiki Yako aliyepo serikalini kukutafutia ajira bado ungebakia pale mwenge kwenye ile ofisi walikua wanakulipa laki tatu kwa mwezi wakili mzima.
Niko peramiho karibu tulime. Naona tangu tuzike chato hujawa sawa hadi leo
 
Kutunza makaburi ni ajira halali kama ajira zingine watu wameajiriwa kutunza makaburi na serikali naye kaanza dharau kama Godblless lema kusema kazi ya bodaboda ni laana

Huyu naye kaanza kuponda watunza makaburi.Watu wanaishi kwa mishahara hiyo anawaponda .Wengine hao watunza makaburi ni waumini wa KKKT anawapelekea ujumbe wa dharau hivyo Hawatendei haki
Wapi kawadharau? Acha chuki za kimaskini
 
Endelea kuishi kwa kukariri. Ndo mana maskini hadi leo na unachukia tajiri akisifiwa
Nakariri wapi kijana.

Usidhani unavyoandika andika hapa Kuna watu hawakujui.

Tunakujua sema tunakausha tu.

Haya endelea kudanganya watu hapa JF.
 
Aliposema wakristo wasikubali kuwa walinda makaburi hizo ni dharau

Wakristo wengi wameajiriwa na serikali kwa kazi ya kulinda makaburi nchi nzima

Kadharau kazi ya kulinda makaburi na wenye kazi hiyo ambao ni wakristo
Umesoma biblia kujua walinda makabuli walikuwa kina nani? Au unaropoka tu
 
Back
Top Bottom