Zakaria Lang'o
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 2,593
- 2,768
Uliambiwa na nani kuwa Mch. Msigwa huwa anaishi kwa misaada ya Magufuli!!!?Ila naona hata undugu utapungua sana sasa, Msigwa akipata tu shida kuanzia sasa Mh. Rais hawezi kabisa msaidia kwa hili lililotokea, na hata ingefaa Msigwa angetoa neno la shukrani kwa Mh. Rais, sasa hizo hela zikirudishwa kwa Mh. Rais navyojua hatakubali tena kutoa msaada hata huko kwao nyumbani, sbb atasema niliingiwa na huruma nikatoa msaada baada ya ndugu zenu kunijia, ila nikapata fedheha. Yaani Msigwa shauri yake
Kiufupi ni kwamba, mtoto wa JPM ameoa mtoto wa dada yake Msigwa. Inaonekana ndugu wa Msigwa wameenda kuomba msaada kwa JPM wakiwa na kianzio cha 2M.
Great thinking, thanksKosa kubwa kafanya rais. Ukishakuwa mtu mkubwa, kiongozi wa nchi hupaswi hata kidogo kuonyesha upendeleo kwa familia yako na ndugu zako. Nyetere alikemea sana hili. Rais ni baba wa watanzania wote na teye ndite custodian wa hazina yote ya nchi. Sasa akianza kufanya vitendo kama hivi inatilia madhaka uadilifu wake. Kwa nafadi yake alipaswa haya kama ni kusaidia afanye kimya kimya isijulikane. Lakino yeye kaona kutangaxa ni sifa kumbe inamharibia. Ni watanzania wangapi wapo magereza wakiwa wameshindwa kulopa faini? Kwa hiyo wao wataozea magereza kwa sababu hawana undugu na rais? Hii ilikuwa move ya hovyo sana.
By the way, mbona michango ilokuwa inaenda vizuri tu huko chadema na hakina mahali walitangaza wameshindwa kipata pesa ya kutosha kuwatoa. Hiki kihetehere cha nini? Kwa kweli washaurivwa rais wamemuaibisha!
Yaani mnifunge halafu mtake kuchukulia ujiko kutoka kwangu!!!!
Mbona CCM ina michezo ya kitoto sana?? Hii CCM inaelekea wapi?
Na iweHahahaha Meko huko aliko aibu aliyonayo nahisi wamchunge asije akajitosa baharini.😅😅😅
Ile chapa ya nambà 666😁Kagoma kuusujudia msalaba ili apigwe chapa aibu kwa ccm hii,
Kama ndivyo ile convoy ya gari za serekali na polepole walifuata nini segereaHii habari imeishachuja! Rais ALIOMBWA NA NDUGU WA MSIGWA awasaidie mchango wa kumlipia ndugu yao kutoka jera! Rais alikuwa anatekeleza ombi la hao wazee hivyo mambo ya alikuwa kaishalipiwa hama la!! hayamuhusu Rais!
Ukweli ni upi, CHADEMA ndio wamelipia faini au Rais Magufuli? Je, kuna ushahidi CCM ilipeleka gari la Serikali kumchukua Msigwa kutoka gerezani, kiongozi akiwa Polepole? Taarifa ifuatayo inatoa jibu.Mbunge wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa amekataa kupanda gari la serikali lililopelekwa gerezani Segerea ili kumchukua baada ya kulipiwa faini.
Awali kulitokea mzozo kati ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na Ndugu Humphrey Polepole ambao walitaka Msigwa apande gari ya serikali kwa madai kuwa amelipiwa faini yake na Rais JPM, lakini wafuasi wa Chadema wakamtaka apande gari aliloandaliwa na Chadema kwa kuwa chama hicho ndicho kimemlipia faini kupitia michango ya watanzania.
Wafuasi hao walidai kwamba wakati Rais JPM anapeleka fedha tayari Chadema ilikua imeshamlipia Msigwa na hivyo fedha hiyo irudishwe kwa Rais ili ikafanye shughuli nyingine za maendeleo.
Kufuatia mzozo huo wafuasi wa Chadema walizuiwa kuingia gerezani humo na wafuasi wa CCM wakiongozwa na Polepole waliingia wakiwa kwenye magari ya serikali tayari kumlaki Msigwa.
Lakini Msigwa alikataa kupanda gari ya serikali aliyoandaliwa na kutembea kwa mguu hadi nje ya gereza walikokuwa wafuasi wa Chadema ambao wamemlaki kwa shangwe na sasa anaelekea makao makuu ya Chadema, eneo la Kinondoni ili kufanya mkutano na wanahabari.!
😂 makamanda wanaweza kushusha mafuriko ya matusi.
Ushahidi mwingine nani kalipa faini ya MsigwaUkweli ni upi, CHADEMA ndio wamelipia faini au Rais Magufuli? Je, kuna ushahidi CCM ilipeleka gari la Serikali kumchukua Msigwa kutoka gerezani, kiongozi akiwa Polepole? Taarifa ifuatayo inatoa jibu.
Mheshimiwa Waterloo umeniacha hoiCCM wanakata viuno ngoma inapigwa Chadema [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Matumizi mabovu ya mamlaka na Mali za umma.Magari ya serikali ya nini huko na Polepole ni kiongozi wa chama au?
Hongera Mch.Msigwa,huo ndiyo uzalendo unaotakiwa,siyo hao waigizaji.Hii inaonyesha mikakati iliyoandaliwa kupitia kesi hii na hukumu yake.Wameshindwa na kulegea.Aibuuu!
Wasio na chapa upelelezi utawakutia ndani hadi watakapo nunua uhuru wao au kwa huruma ya dpp,wenye chapa upelelezi unakamilishwa kwanza ukiwa njeIle chapa ya nambà 666😁
Hakupaswa kwenda kumpokea wakati anafahamu kuwa ingeleta sintofahamu ,mchango wa jpm Kama good gesture ulitoshaDuh, ccm hatari.polepole amebaki kituko
Kwanini unawaza matatizo kwa Msigwa tu?Huyo JPM mwenyewe hawezi kupata shida?Halafu msaada gani wa masharti namna hiyo?Ingetosha tu kulipa na kutoa taarifa kwa wahusika,ila unalipa unaita vyombo vya habari,unamtangaza kuwa umemlipia,unaenda gerezani na makamera kumpokea pamoja na makada wa CCM !Sasa huo ni msaada au unataka umtumie ndugu yako kwa malengo yako binafsi?Hata mimi ningekuchenga!!!Ila naona hata undugu utapungua sana sasa, Msigwa akipata tu shida kuanzia sasa Mh. Rais hawezi kabisa msaidia kwa hili lililotokea, na hata ingefaa Msigwa angetoa neno la shukrani kwa Mh. Rais, sasa hizo hela zikirudishwa kwa Mh. Rais navyojua hatakubali tena kutoa msaada hata huko kwao nyumbani, sbb atasema niliingiwa na huruma nikatoa msaada baada ya ndugu zenu kunijia, ila nikapata fedheha. Yaani Msigwa shauri yake