Pre GE2025 Mchungaji Msigwa atangaza kukata rufaa kupinga Ushindi wa Joseph Mbilinyi (Sugu) Kanda ya Nyasa

Pre GE2025 Mchungaji Msigwa atangaza kukata rufaa kupinga Ushindi wa Joseph Mbilinyi (Sugu) Kanda ya Nyasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)


Akiongea na Waandishi wa Habari leo, Peter Msigwa amesema kwamba Ushindi wa Sugu ulijaa makando kando na Mchezo Mchafu (Hakufafanua)

Ametangaza kukata rufaa kwenye Kamati Kuu ya Chama chake kupinga ushindi huo wa Sugu, bado haijajulikana kama Kamati Kuu ikiridhishwa na Madai yake nini kitatokea, Sugu atanyang'anywa Ushindi na kupewa Msigwa au Uchaguzi utarudiwa

Binafsi nampongeza Mchungaji huyu kwa uamuzi wake huu, maana hii ndio njia Sahihi iliyowekwa na Chama chake ya kudai haki.

Pia soma

Huko ndiko kukomaa kisiasa kwa Chadema, jambo ambalo CCM ni marufuku kukata rufaa.
 
Ni AIBU kubwa kwa CHADEMA kumchagua Sugu badala ya Peter Msigwa. Hata mukiniambia kuwa Sugu alikuwa na fedha chafu na kagawa kwa wajumbe, fedha unapokea lakini kura unapiga kwa kutumia akili yako.

Naiombea hiyo rufaa ipite ili IWASAFISHE CHADEMA.

Unamuachaje mtu kama Msigwa ana madini, amenyooka, hanunuliki na ana VISION na kwenda kumpa kura mvuta bangi, mtu wa matusi, mvaa mlegezo??

Mimi SIYO CHADEMA ila you people ARE NOT SERIOUS!!

Kwa taarifa yenu, mukirudia makosa haya kwenye Ubunge wa Mbeya Mjini mkamismamisha SUGU 2025, JIMBO MNALIPOTEZA.

TULIA hakubaliki Mbeya ukiacha maeneo ya Uyole, Itezi, Igawilo na Iduda anakogawa hela na T-shirt. Lakini zile kata asilia za Mbeya Mjini yaani kuanzia Mwakibete hadi Iyunga, Sisimba, Mwansekwa Tulia Ackson si lolote.

Tafuteni mtu anayeuzika ila siyo SUGU
Hapo Mbeya nani anauzika zaidi ya Sugu mtaje hapahapa. Kwamba huyo mtu wako akisimama dhidi ya Sugu anamshinda
 
Uongozi ni kama mbio za kupokezana vijiti, yule Sugu unayemzungumzia wewe si huyu wa leo, hata hivyo hatuwezi kuzuia Msigwa kukata rufaa kwenye Chama maana huko ndiko katiba inaelekeza.

Hata hivyo napinga dharau zako kwa Sugu kwa vile hazina tija, Hospitali nyingi za Mbeya zilifanyiwa marekebisho kwa ushawishi wa Sugu kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Ulisubisya, yaani Sugu kamkalisha Mpoki chini na kumueleza umuhimu wa kuboresha Hospitali ya Rufaa na Ile ya Meta (Martenity Hospital) zinazohudumia Mkoa wa Mbeya na Mpoki akafanya mchakato, sasa hata akivaa mlegezo lakini akatufanyia haya shida iko wapi?
Kadanganye wajinga wenzio huko kwenye vijiwe vya mama John na Ilemi na Mabatini. Sugu hana mchango wowote kwenye upanuzi wa hizo hospitali na hakuwa na uwezo wa kumshawishi ULISUBISYA.

Yeye ni mtu wa yoyo man tu na kugongesha bangi vijiweni
 
Sidhani kama Chadema inaweza kuwaacha domant watu kama Msigwa watapewa post za teuzi, ninachokiona kuna watu wanaamini wao ndio wanastahili.

Itapendeza pia mtu kama Sugu aambiwe afanye kazi za chama alizoomba swala la ubunge wagombee watu wengine yeye asimamie mchakato wa kupata wagombea ubunge.
Hapa tunaongea lugha moja. Akigombea ubunge Mbeya mjini hatiboi
 
Alichofanya Msigwa ni haki yake, kama hajaridhishwa na namna Sugu alivyoshinda na ana sababu za mantiki kupinga ushindi wake, sioni ubaya wowote kwa Msigwa kukata rufaa.

Simply anachofanya Msigwa anataka haki ifuatwe, kama KK itaamua kumpa ushindi Sugu au kumpoka, bado sioni kama kuna jambo zito la kupigania hapo.

Sijui huko Chadema labda mwenyekiti wa kanda anapokea mshahara kwa hiyo nafasi, lakini kwa namna navyoona mambo yanaenda, binafsi sioni sababu yoyote ya kuwepo na ugomvi kati ya hao wawili, nachokiona ni muendelezo wa kuonesha ukomavu wa demokrasia.

Demokrasia haipo tu pale kwa Msigwa kukubali kushindwa, atakubali kushindwa kama kweli anaona ameshindwa kihalali, lakini kama anatilia shaka ushindi wa mwenzake sioni sababu kwanini asipiganie haki yake.
 
Alichofanya Msigwa ni haki yake, kama hajaridhishwa na namna Sugu alivyoshinda na ana sababu za mantiki kupinga ushindi wake, sioni ubaya wowote kwa Msigwa kukata rufaa.

Simply anachofanya Msigwa anataka haki ifuatwe, kama KK itaamua kumpa ushindi Sugu au kumpoka, bado sioni kama kuna jambo zito la kupigania hapo.

Sijui huko Chadema labda mwenyekiti wa kanda anapokea mshahara kwa hiyo nafasi, lakini kwa namna navyoona mambo yanaenda, binafsi sioni sababu yoyote ya kuwepo na ugomvi kati ya hao wawili, nachokiona ni muendelezo wa kuonesha ukomavu wa demokrasia.

Demokrasia haipo tu pale kwa Msigwa kukubali kushindwa, atakubali kushindwa kama kweli anaona ameshindwa kihalali, lakini kama anatilia shaka ushindi wa mwenzake sioni sababu kwanini asipiganie haki yake.
Kukata Rufaa ndio unaitisha Press nyumbani kwako?

Huyo ameshaaga 🐼
 
Hapo Mbeya nani anauzika zaidi ya Sugu mtaje hapahapa. Kwamba huyo mtu wako akisimama dhidi ya Sugu anamshinda
Wangekuwa hawapo basi kusingekuwa na zoezi la kuchukua fomu za uteuzi ndani ya chama. Yaani mtu angepita tu. Siwezi kuwataja sasa wenye uwezo bali subiri wakati mwafaka utawaona. Kuwataja sasa hivi ni kuwaharibia
 
Katiba ya Chadema inatakiwa kuzingatiwa kama hamjui kuendesha chama mkodi watu kutoka CCM wawasaidie uchaguzi ndani ya Chadema ni suala la kikatiba kukata rufaa sio kitu Cha kwenda kwenye vyombo vya habari
Yaani cdm wakafundishwe na hicho chama kinachoprint fomu Moja?! Siku cdm watakosea eti wajifanye wanapewa darasa la uongozi na ccm, nitawadharau kupita maelezo.
 
Yaani cdm wakafundishwe na hicho chama kinachoprint fomu Moja?! Siku cdm watakosea eti wajifanye wanapewa darasa la uongozi na ccm, nitawadharau kupita maelezo.
Mumeshindwa kuweka ukomo wa mtu kushika Cheo kikubwa Ona Sasa Msigwa anawasumbua mngeweka ukomo.miaka kumi mfano Msigwa angepisha Wengine mjifinze CCM kuweka ukomo wa mtu kushika cheo
 
Katiba ya Chadema inatakiwa kuzingatiwa kama hamjui kuendesha chama mkodi watu kutoka CCM wawasaidie uchaguzi ndani ya Chadema ni suala la kikatiba kukata rufaa sio kitu Cha kwenda kwenye vyombo vya habari
Wakati Membe amefukuzwa ccm na dhalimu Magu na kuitisha press, mbona hao walimu wa siasa huko ccm hawakujitokeza na kumpa utaratibu wa kukata rufaa?
 
Kukata Rufaa ndio unaitisha Press nyumbani kwako?

Huyo ameshaaga 🐼
6208957_square.jpg

Endelea tu kucheka ukitarajia Mkono utadondoka, akili za kuvimbewa Mifupa hizo.

MaFisiem ni MaFisiem tu.
 
Mumeshindwa kuweka ukomo wa mtu kushika Cheo kikubwa Ona Sasa Msigwa anawasumbua mngeweka ukomo.miaka kumi mfano Msigwa angepisha Wengine mjifinze CCM kuweka ukomo wa mtu kushika cheo
Ccm ukomo uko kwenye cheo cha mwenyekiti tu, na lengo ni Ili mwenyekiti awe rais, Wala sio suala la demokrasia kama unavyotaka tuamini. Ingekuwa Kuna demokrasia tusingeona mwenyekiti wa ccm akaipata kura 100% kinyume na uhalisia.
 
Back
Top Bottom