Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA

Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Chadema itazunguka nchi nzma kueleza usaliti wa msigwa, shida iko wapi? Abdul alimlambisha hela ,.....itawekwa wazi soon
"Kuna Shida". Hizi siyo sarakasi za kawaida hata kidogo.

Yeye Mchungaji, akawa wa kwanza kulialia, alipoona mwenzie Sugu kaweka dau kubwa zaidi ya lile alilo wezeshwa yeye, toka kwa huyo huyo Abdul?

Shida hii huioni?
 
Alikuwepo Upendo Peneza kazunguka karibia redio zote kuisema vibaya CHADEMA ila akaona hakuna anayemfautilia ameamua kuingia mitini na CCM imemweka pembeni maana amefika bei. Peter Msigwa ajiangalie atakuja kujiaibisha mwenyewe baadala ya CHADEMA.
 
Mbowe aache kumsema Magufuli..aende akadhuru kaburi..huyu msigwa alikuwa babyboy wa mbowe .anajua siri nyingi za mbowe na chadema..hii si hali ya kawaida.
 
Kada wa CCM mchungaji Msigwa amesema atazunguka nchi nzima kuelezea uwongo na ulaghai wa Chadema

Msigwa ameomba awezeshwe Ili aungane na Wanaccm wenzake kuisambalatisha Chadem...
Mwambie binafsi si mwanachama wa chama chochote lakini nitamkabili kwa maswali popote nitakapomuona!Nitamuulixa kwanini hakutueleza huo uongo kabla ya uchaguzi aliotemwa?

Kama angechaguliwa kuwa mwenyekiti huko kanda ya Nyasa je angeendelea kutuficha uongo huo!?What is this!!!?
 
Uongo wake au wa CHADEMA?
Huyu jamaa mtu akikusanya clips zote alizosema kuhusu CCM wakati akiwa CHADEMA unaweza kufikiri ni watu wawili tofauti. Aliwahi kusema siku akienda CCM,...
Hivi, Uchungaji wake ni wa nini,,? Haoni hata haya. Ndo maana siku hizi watu wengi wameacha kwenda makanisani!
 
Kwa hivyo akizunguka nchi nzima ndio atasababisha Ajira kwa vijana?. Mjinga Sana. Akae kimya alambe asali.
Mkuu 'Econo' nadhani kuna mchezo mchafu sana hapa tunaochezewa akili toka kwa pande zote mbili, toka CHADEMA ya Mbowe; na hii CCM ya 'Chura Kiziwi'.

Naanza kuipa uzito zaidi ndharia ambayo nimekuwa nikiijenga kwa muda sasa. Mbowe na 'Chura Kiziwi' wanawachezea waTanzania akili.
Viongozi kama akina Tundu Lissu na wengine huko ndani ya CHADEMA watakuja kujikuta wamekwisha ingizwa kichakani kama mchezo mchezo vile, kabla hatujaingia kwenye shughuli za 2025.

Akina Msigwa sasa wana tangulia mbele tu, kuelekea watakakoishia sehemu kubwa ya CHADEMA wakiongozwa na Mbowe mwenyewe.

Sasa naamini kabisa, CHADEMA chini ya Mbowe haina nia kabisa ya kuiangusha CCM.
Kinacho pangwa sasa hivi ni ushirika kati ya CCM ya chura na CHADEMA ya Mbowe kushirikiana; hata kama ikiwa chini ya mazingaombwe kama "Serikali ya Umoja'. Hili ndilo linalo endelea kutengenezwa sasa hivi tukiangalia kwa macho yetu na kusikia kwa masikio yetu wenyewe.
 
Mkuu 'Econo' nadhani kuna mchezo mchafu sana hapa tunaochezewa akili toka kwa pande zote mbili, toka CHADEMA ya Mbowe; na hii CCM ya 'Chura Kiziwi'...
Umeongea ukweli. Mbowe simwamini kabisa siku hizi. Namuona Kama nduminakuwili.
 
Kada wa CCM mchungaji Msigwa amesema atazunguka nchi nzima kuelezea uwongo na ulaghai wa Chadema

Msigwa ameomba awezeshwe Ili aungane na Wanaccm wenzake kuisambalatisha Chadem...
amechiz hahaha

nani atamsikiliza sasa?

Badala ya kutoa sera za kuwapatia vijana ajira anambela mbela tu
 
Mbowe hana sababu yoyote ile ya kuiangusha serikali ya CCM ambayo anaiongoza Samia; hakuna.

Anaye bisha juu ya hili anitajie sababu hizo muhimu, (visiwe visababu vya uongo na kweli).

..sijui kama umeona press conference ya msigwa.

..kilichofanyika ni udhalilishaji na aibu kubwa kwa msigwa na watanzania.

..mwenezi wa ccm alikuwa na makaratasi aliyokuwa akimpa msigwa ayasome.

..wakati mwingine alikuwa akiongeza notes na kumkatisha msigwa na kumpa aongee kwa waandishi.

..hawa watu hawana aibu. ni watu wa hovyo, wa ajabu.
 
Kada wa CCM mchungaji Msigwa amesema atazunguka nchi nzima kuelezea uwongo na ulaghai wa Chadema

Msigwa ameomba awezeshwe Ili aungane na Wanaccm wenzake kuisambalatisha Chadem...
Lazima ujifunze siasa kupitia kwa wanasiasa wazoefu kama vile Ngoyayi na Sumaye. Huwezi kunyea kambi! Ashakhum si matusi.

Wengi sana wamepita CDM na kwenda CCM, lakini hatima zao za kisiasa zinafahamika vizuri sana. Huyu si wa kwanza wala wa pili, msururu ni mrefu sana! Makapi ni lazima yajichuje ili ngano yenye thamani iweze kupatikana.

Nenda kwa amani Mch. Msigwa, kwani hukuwahi kuwa wa kwanza kufanya hivyo. CDM bado ina dhamira ya dhati kabisa kukifanya kile siku zote ichokusudia kukifanya. Nacho ni kutwaa DOLA na kuikomboa Tanzania kutoka katika makucha na nira ya mkoloni mweusi.
 
Hii ndio Taarifa ya kada mpya wa CCM komredi mchungaji Msigwa

Kwamba baada ya Kupokea mialiko lukuki ya Vyombo vya habari sasa atamwaga mboga tarehe 10/06/2024 mwembetogwa Iringa mjini

Makamanda Wote mnakaribishwa

Msigwa ametoa Taarifa ukurasani X

Mlale Unono 😀😀🔥
 
Hii ndio Taarifa ya kada mpya wa CCM komredi mchungaji Msigwa

Kwamba baada ya Kupokea mialiko lukuki ya Vyombo vya habari sasa atamwaga mboga tarehe 10/06/2024 mwembetogwa Iringa mjini

Makamanda Wote mnakaribishwa

Msigwa ametoa Taarifa ukurasani X

Mlale Unono 😀😀🔥

..Msigwa amekuwa kama mateka wa Amos Makala.

..anaandikiwa nini cha kuongea, na akikosea anapenyezewa notes/ vikaratasi.
 
Hivi kuna mtu aliyeeleza uovu wa CHADEMA mpaka akauza sela za Chama kama Dk.Slaa lakini CHADEMA iliendelea kubaki na ikafanya vizuri kwenye uchaguzi wa 2020?

Kwa hiyo hata Msigwa hakuna atakachobadili.
 
Back
Top Bottom