Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Nitazunguka Nchi nzima kuelezea Uongo wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
..Msigwa amekuwa kama mateka wa Amos Makala.

..anaandikiwa nini cha kuongea, na akikosea anapenyezewa notes/ vikaratasi.
Hata bungeni alikuwa anaandikiwa na Nyalandu mambo mengi πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Jibu ni HAPANA, sijaiona hiyo 'press conference' ya Msigwa, na ni muhimu kuwa sina nia kabisa ya vitu vya aina hiyo tena toka huyo jamaa ajiondoe akili kichwani.
Msigwa sikuwahi kuwa na matumaini makubwa naye sana, toka siku nyingi; pamoja na kwamba baadhi ya matukio, kama yale yaliyofanyika chini ya Magufuli, yalichanganya akili kidogo juu yake.

Sasa kinacho umiza kichwa, ni kuona dalili zile zile toka ndani ya chama kilicho tegemewa kutuondolea uozo kama huu unao utaja kufanyiwa mchungaji, udhalilishaji!

Sasa haitakuwa udhalilishaji wa mtu mmoja mmoja kama huyo Mchungaji, chama kizima kitadhalilishwa!.

Najua, wakati huo utakapo wadia, kutakuwa na tungo za ngonjera nyingi sana za kupindisha akili za wanao taka kupindisha akili.
Taratibu tunaanza kuyaona haya.
 
Ukiachana na mke au mume ukiwa unamuongelea kila mara means bado unampenda.

Tunajua kwamba Msigwa unaipenda chadema ila naungana na Dr Hashimu Rungwe alivyosema "TATIZO NJAA" na hata afande sele alisema "Adui muombee njaa atanyoosha mikono juu hata kama alikuwa shujaa".
 

..kwa hapa tulipofika tutafute namna ya ku-deal na CCM.

..maana hiki kinachotokea kwa Chadema kilishatokea kwa vyama vingine vilivyochipukia.

..Ccm itakapomalizana na Chadema itahamia kwa chama kingine kitakachoibuka.
 
Mwanamke ananongwa huyu. Kwani si amempata bwana mwingine? Sasa kwanini ana uchungu sana na bwana wa zamani?
 
CDM bado ina dhamira ya dhati kabisa kukifanya kile siku zote ichokusudia kukifanya. Nacho ni kutwaa DOLA na kuikomboa Tanzania kutoka katika makucha na nira ya mkoloni mweusi.
Maneno mazuri sana haya, ambayo wengi tumekuwa tukiyapa matumaini na uzito wake halisi.
Lakini sasa dalili za matumaini haya zinaonyesha kuwa ni hewa.
CCM wamefanikiwa kuwa na mu-arobaini juu yake. Kama ni CHADEMA hii hii, chini ya Mwenyekiti, na jinsi inavyo kwenda sasa..., sahau kabisa hizo ndoto za maneno hayo uliyo weka hapo juu.
 
Kwani ukiachana na Mkeo, Halafu ukampata mwingine lazima uanze kusimulia mabaya yake? Kwani huyo mpya yeye mabaya yake kakusimulia?
 
Ni swala la muda tu mambo yote yatakuwa wazi

Ikumbukwe Wakati Shujaa Magufuli anaichangia Chadema tsh million 38 mchungaji Msigwa alikuwa ameshalipiwa faini na wanachama na Gerezani alikuwa amebakia Mbowe Peke yake ila kesho yake alitoka

Nadhani Mchungaji Msigwa ataliweka wazi na hili

Mlale Unono πŸ˜€πŸ˜€πŸ”₯
 
Yaani kwa ule ujinga aliokuwa anaongea kuhusu ccm, anategemea kuna mtu ataelewa huo utoto wake? Yaani bora ajikalie kimya tu maana ataishia kujichoresha, na kusababisha kuonekana siasa ni mambo ya uongo. Huyo kutaka kuongea lugha ya kuwafurahisha ccm, wakati kizazi kina uelewa wa kutosha ni kujichoresha tu.
 
Mbowe aache kumsema Magufuli..aende akadhuru kaburi..huyu msigwa alikuwa babyboy wa mbowe .anajua siri nyingi za mbowe na chadema..hii si hali ya kawaida.
Cdm kuna siri gani za kuwatisha ukisema unaenda kuongea?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…